Kuna umuhimu?



Lakini kweli unafanyaje akikupa hili tena akiongezea sioni unachoringia wangapi nimewaona zaidi yako.... Uwiiii ntamtafuna
 
B_E
Ningejikaza kisabuni..halafu ningemjibu.." uliona wengi baba, lakini hapa kwangu ndo breki yako..mwisho wa njia! "
Ila uongo si kazi..ningeumia sana rohoni na ningemchukia sana!

Na mimi nilimjibu hivyo hivyo but in a very outrageous way! hiyo text nyekundu hapo juu replace neno baba na neno mama!
 
kila mtu anapenda kujua historia ya mwandani wake,tatizo ni kwamba utaweza kuhimili utakayoambiwa?kuna ishu moja ilitokea siku ya harusi mke alimuuliza mume wake....mume wangu leo tumefunga ndoa naomba niambia mimi ni wangapi kwako coz siwezi kukataa tena kuolewa na wewe.jamaa akakaa kimya anawaza,mkwewe akamuliza mbona hujibu?jamaa akawa anasikika anahesabu kimya kimya akisema 172,173.....17...4!ikabidi mkewe azirai kwa mshtuko.Jamani historia sio nzuri.
 
Nimeipenda hii thread. Kweli ishi ili uone, watu wana historia tofauti sana, ndio maana mara nyingi busara huambata na umri. Asante B-E kwa mchango wako.
 
Hapo hakuna faidam yoyote zaidi naona ni kujiongeze stress zisizokuwa na mpango wowote so hapo mnakwenda kimya kimya kama kawaida!!
 

Hakuna umuhimu kuambizana vitu kama hivyo pia hata kama umedate wanawake 16 kabla ya uliyenaye,utakuwa mstaarabu kidogo kusema nilikuwa na wanawake wanne kabla yako.
Kama huna kifua cha kubeba mambo mazito usitake kujua kabisa.Haisaidii sanasana hubomoa tena mkikwaruzana kwa hasira.
Cha muhimu ni kuenjoy to the fullest with the current lover/partner!..
 
Sasa mkeo akuambie mtu kama Masanilo alikuwa bf wake zamani si utapigana.....utajua tIGO ilishaliwa imeshaliwa
 
Kitale,inategemea ukowapi, kama uko TZ ni muhimu sana. Kwanza ninavyojua asilimia kubwa ya wa TZ ina VVU. Kwa hiyo kama sijamgusa itakuwa bora nijue historia yake na ikiwezekana nimpime. Kama ni dada ni bora nizijue vizuri team alizocheza nazo ili niweze kuhakikisha kama kuna zinazochezea TIGO lazima na mimi niende huko. Mwisho kuna msemo wa kabila fulani kuwa kama unyasi haujangolewa basi hauwezi kukauka,hivyo lazima niwajue waliomlamba kusudi wakimkaribia au nikiwaona wanaelekea sehemu hatarishi namfuata nakumtoa. Nawakilisha!
 
Asanteni kwa hii mada maana naona imelenga kwangu kabisaaaaaa...hivi unajua haya mambo huwa hivi hivi kimchezo chezo tuu. Kama mimi kuna siku tulikuwa na fight na mr. khs maswala ya unyumba hanilidhishi na fwezaaa. Kwanza nikamuliza vp khs something mbona cku hizi imekuwa hadimu na mimi nahiitaji! mweee, nililoambiwa kama nimeona hanilidhishi nikatafute wakunilidhisha, yeye anaona kama hawezi...mbona palikuwa hapakaliki. Kwa mahasila niliyokuwa nayo nikamwambia cjawahiiii toka nianze kutembea na wanume (yani nikamwambia talehe na mwaka nilioanza kujua wanaoume) ckuwahi kusikia hilo tamko. Nyie acheni kabisa na haya maswala yanaletaga matatizo hivi hivi.
 
Vipi asa hali imetulia au unataka usaidizi?
 


Ili historia hiyo iwe na manufaa kwako ni vema ukaifahamu (kwa kuelezwa na yeye mwenyewe au kuipata kwa njia nyinginezo) kabla hamjaamua kuoana. Kama alikuwa na mahusianao jaribu kupata ukweli ni kwa nini mahusiano hayo yalivunjika. Historia hiyo itakusaidia kumfahamu vizuri zaidi mchumba wako.Historia inaweza kutoa mwanga kuhusu tabia za mwenza wako na kukusaidia kufanya maamuzi iwapo ni mtu sahihi kuwa nae katika maisha yako kama rafiki na mwenza.

Nadhani ni hatari kujaribu kuipata historia ya mwenza wako wakati mmeshaoana tayari. Katika wakati huu historia (kama ni mbaya) itaongeza tensions badala ya kuisaidia ndoa yenu.

Cha muhimu zaidi kujua ni kwamba binaadamu tunabadilika (we are dynamic) na hivyo si vema kumuhukumu mtu kwa historia yake pekee ni lazima uzingatie ukweli uliopo sasa. Kwa mfano, kama ukiangalia historia ya mtu wakati akiwa 'teenager' na kufikiri bado ana tabia hizo wakati akiwa in his/her 30's utakuwa humtendei haki.

.........................

Wazo mbadala:

Nafahamu tunapoenda kuomba kazi waajiri mara nyingi wanazingatia uzoefu, umri, uwezo na maarifa mengine ya mtu anayeomba kazi. Sasa katika mapenzi, si vizuri pia kumpata mtu mwenye uzoefu🙂?
 
 
mie nilikuwa cpend kweli haya maswali, nilikuwa nikiulizwa tu naona kabisa huyu man sio type yangu! muongelee tu mengine kuhusu nyie mana hapo ni kudanganyana tu hakuna cha zaidi.
 
what if ukimwambia " kwani na wewe unawatongozaga akina nani?" atajibu

nini?
ni bora ukimjibu." hakuna mtu ananifuataga" utasikia " haiwezekani, unanificha tu..... plsss niambie basi nijue tu wala sifanyi kitu!"


na hilo ndio jibu la kumtosheleza, coz ukimwambia ni fulani atamweka kichwani hata ukisalimiana nae tu tayari ishu.... haaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…