Kuna utaalamu wowote unaweza kufanywa kwenye mti ili mti usizae matunda?

Loimata

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2022
Posts
749
Reaction score
1,741
HERI YA MWAKA MPYA.

Ndugu zangu wataalam wa kilimo,hivi kuna utaalamu wowote unaweza kufanywa kwenye mti ili mti usizae matunda?

Nauliza hivi kwa sababu kuna sehemu nimepanda miti ni mizuri ila tatizo lake inazaa vitunda vidogo vyekundu ambavyo vinapendwa na popo na popo hao wakishakula hivyo vitunda wanajisaidia ukutani.

Majengo ya hilo eneo yamepakwa rangi hata mwezi haujaisha lakini ukiona popo walivyochafua hutaamini.

Ushauri wa dawa ya kuwaua popo hautanisaidia sbb as long as miti itaendelea kuzaa watarudi tu.

Kitakachosaidia ni kama kuna kitu tutafanya miti isizae hivyo vimatunda tu.

Natanguliza shukrani
 
Labda uwasiliane chuo kikuu cha sokoine wanautaamu kwenye maswala ya miti japo hilo laki sidhini kama litawezekana kutokana na aina na asili ya mti
 
Labda uwasiliane chuo kikuu cha sokoine wanautaamu kwenye maswala ya miti japo hilo laki sidhini kama litawezekana kutokana na aina na asili ya mti
Nitawatafuta mkuu
 
Bora hiyo rangi utapaka nyingine, hiyo miti unayoizungumzia pia inapendwa sana na mbu na usipokuwa makini kama unaishi na familia hilo eneo kila siku utakuwa unahangaika na kununua mseto. Kata hiyo miti haraka panda miti ya aina nyingine.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Cheki pia hapa





Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app

Ooh kumbe!

Sio eneo la kuishi watu ila nawaonea huruma walinz wetu wa usiku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…