Kuna Video iliyokuwa ikionesha Polisi/traffic wa Inyala, Mbeya wakimshusha kwa nguvu dereva wa lori. Polisi wadai amekufa kwa homa ya mapafu

Wameonekana wakimburuta.

Huyo dereva, walimfikisha hospital amefariki kwa vidogo wao wamesema alifia hospitali. Madereva wamechachamaa. Wanajua ukweli.
Kwamba police wa Tanzania ni wauajo na watesi wakuu. Unajua kisha unasema huyu chadema yananisha.

Mkuu wa Mkoa anaunda tume. Anaipa siku tatu itoe majibu yapi sijui aliyekufa kafa wenzake wanasema wameuwawa kwa vidogo na Mateso. Polisi wa mbeya wameua dereva wa lory na wakisema wameuwawa hospital.

Angekuwa mwanasiasa wa upinzani yangesemwa mengi kuzusha uongo.lama kwa akwilin, ben na wengine siwakumbuki, nakumbuka tukio la kinyama la Tundu Lisu. Hapakuwa na haraka wala karaha kuchunguza. Walikataa hata wa nje. Ati twajiweza wenyewe
Haki itendeke, Saudi wa dereva wa lory washtakiwe, wahukumiwe haki itendeke na tuone

Source. ITV habar
 
Hili tukio halina tofauti na lile la mauji ya Mwangosi enzi za Kikwete na msishangae kuona hakuna askari ataechukuliwa hatua.

Nashangaa sana watu wanapomkubuka Kikwete na si ajabu watakuja tena kumkumbuka Magu kwani wanadamu tumeumbwa kusahau.
 
Tulia ulete habari ieleweke sio kila mtu anaangaliaga habari. Umechanganya Mambo mengi kwa mpigo.. trafiki,Askari,akwelina,Lissu,Ben,Dereva,lorry nk mpaka umechapia chapia, elezea ilikuwaje kisa kilianzaje ikibidi weka picha au video ili watu waweze kutoa maoni. Umeandika Kama mtu anayekimbia baada ya kufumaniwa...
 
mi kuna siku nilipanga hiyo kitu ila mungu aliye juu aliniepusha.kidogo nipite na kibanda chao

ungekuwa umekosea maana baadhi ni innocent , kuna mmoja alipitiwa na fuso aise alafu alikuwa anasolve ajali iliyotokea eneo hilo
 
Yule mmarekani mweusi alivyouawa na polisi kule marekani, hapa kwetu watanzania walipiga sana kelele lakini kifo cha huyu dereva watu wapo kimya.
Ndio kusema kwmba watanzania hatuthaminiani au uwoga?
 
Siku zote nalalamika askali wetu kukosa elimu.
Sijui wanawafundisha nini hawa askari.
Askali anatakiwa kujua kua ndio awe wa kwanza kuwa smart,
Lakin askali wetu wakivaa nguo za uaskari wanaona raia sawa na mifugo yao.


Lakin pia inaoneka hawa askari watakua wanalazimishwa kufanya haya.
Mfano:-
Kiongoz anaewatuma/anaewapanga askari hawa labda kuna hesabu anaitaka imfikie kila jion,hapa askari analazimika kufanya chochote ili hesabu yake ifike iende kwa mkubwa.

Tumeona askari wanafukuza bodaboda hadi bodaboda wanaanguka wanaumia hadi wengine kufa kabisa.
Hali hii lazima kunatatizo kutoka kwa waliojuu yao.

Mm naona kitengo cha usalama wa taifa kiunde time ya kuchunguza kitengo choote cha usalama barabarani.
Lasivyo watu wataumia sana.

Maana askali wa sasa hawapendi ufuate sheria inaonekana ukifuata sheria wanakasilika kwa kukosa chochote.

Unakuta trafik kasimamisha bas ambalo linaenda mbali anamshusha dereva bila ya kuwaambia abilia hata nususaa inaisha na hana shaka.


Ila kikubwa zaidi,askari wetu waelimishwe kwa kiwango cha juu kabisa.Maana hawajitambui hawajitambui na hawatambui wajibu wao.
 
Serikali iwachukulie hatua kali kabisa traffic hao
 
ALAFU KUNA WATU AKIULIWA MTU MWEUSI
HUKO MAREKANI UTAWASIKIA BLACK LIVES MATTER....WAKATI NI ALL LIVES MATTER
NA KWA TUKIO HILI UTAWASIKIA WAKO TULI KAMA MAJI YA MTUNGINI HAPA BONGO

OVA

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobil

Hilo tukio ni zaidi ya lile la I can't breathe
 
Wazungu wengi wana ka msemo "fu** De police" nadhani Hawa jamaa hawapendwi dunia nzima
 
KUSANYA TAARIFA URUDI TENA MAANA HUJATAJA MBEYA ENEO GANI? DEREVA NI NANI ALIKUWA NA KOSA GANI? BAADA KIFO KUTOKEA WANANDUGU WAMEPEWA MWILI QU HAPANA AU WAMEZIKA WAPI. USIPANDE CHUKI BUREEEE.
Mmmh ndugu au ndo ushabiki hupofusha?[emoji849][emoji849]
 
Kesi ngumu sana hii ila haiondoi kosa ka askari hao.

Tatizo watu wengi wanaendekeza shida binafsi kwenye masuala yanayohitaji weledi, polisi wengi wanachangamoto za kimaisha hali inayopelekea kufanya maamuz yenye kusukumwa na mihemko ndani yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…