Habari, leo nilitembelea moja ya makanisa ya kiroho hapa Dar. Ibada ilikwenda vizuri ila mwishoni mama mchungaji ambaye ni binti wa miaka kati ya 30-32 alitoa neno.
Huyu ni binti mweupe, mrefu na mwenye shape yake, ni mzuri kiukweli, tena sana kwenye kila angle.
Kikubwa ni binti asiyeringa na hana majivuno, kuanzia kwenye kuongea na watu mpaka maisha yake kwa ujumla.
Sasa lililonishangaza na kuamini kuna wanawake warembo wana misimamo ni hili,
Anasema alipokuwa chuo kikuu(UDSM) alipata usumbufu mno kutoka kwa Wahadhiri wake, sana. Pia baada ya kumaliza na kuanza kazi ofisini alisumbuliwa mno na mabosi na watu wazito baadhi wa nchi hii.
Anasema alikataa ofa ya 100m TZS kwa wakati huo ili akubali ku date na don fulani. Hapa ndipo pamefanya nimpe credits 98% mrembo huyu.
Aisee kuna warembo hawanunuliki kwa chochote.