Kuna watu walichonga majeneza yao wenyewe Serikali ya Awamu ya Tano

Kuna watu walichonga majeneza yao wenyewe Serikali ya Awamu ya Tano

Joined
Mar 14, 2015
Posts
85
Reaction score
105
Wasalaam wadau,

Wakati fulani katika awamu ya tano, kiliibuka kikundi cha kusifu na kuabudu viongozi hata kufikia kutaka kubadili katiba ili kuwaongoza muda viongozi walio madarakani, sio nia ya bandiko langu kutweza utu au legacy ya hayati mwenyekiti wangu Dkt. JPM bali kuwakumbusha waabudu wale kuwa vichwa vina matumizi yake zaidi ya kufugia nywele na kwamba hakuna tumbo la kiumbe yoyote lenye ubongo uamuapo kuliendekeza litakupoteza.

Swali la msingi sana waliloshindwa kujibu mumiani wale ni je, tulikua tunarekebisha katiba zetu za chama na nchi kwa ajili ya Dkt John Pombe Magufuli au Rais Dkt. John Pombe Magufuli?

Kimsingi mumiani wale hawakujua nia ya dhati ya kile wakitakacho na matokeo yake leo hii wamebaki kubweka baada ya kuona dalili za kufa kwa matarajio yao yote, mfano mmojawapo unaoatoa kamasi ndugu zangu hawa ni utaratibu wa upatikanaji wa wagombea wa nafasi za ubunge na ndani ya chama ambapo baada ya kubadilika kwa kanuni za uchaguzi za chama, sasa kikao chenye mamlaka ya mwisho kuamua nani agombee ni kile kinachoongozwa na mwenyekiti taifa tena hata awe na kura sifuri kwa vile tu atakua na sifa njema machoni pa mwenyekiti basi atatoboa kama walivyopita ndugu zetu wabunge baadhi wanaodemka bungeni mule.

Jambo la pili linalowatia kichaa ndugu waabudu ni uchaguzi wa ndani ya chama mwakani ambao kwakweli kutokana na msiba mzito wa mwenyekiti aliyepita uliokuja ghafla kabla hata upangaji wa safu mpya 2022 na mabadiliko ya taratibu za uchaguzi ndani ya chama zinazompa leo hii mwenyekiti mamlaka makubwa ya kuamua nani awe wapi praise wengi wamevurugwa kwelikweli.

Kiujumla kutokana na ujuaji mwingi na kutokufikiri kwa upana majority ya waabudu walichonga majeneza yao wenyewe na kufunga maturubai ya misiba yao kwa kutokufikiri kuwa katiba haimuhusu mtu mmoja bali jamii nzima ni jambo la kumshukuru MUNGU kuwa katiba ya nchi haikubadilishwa laiti kama ingekua imebadilika na yakatokea ya kutokea sijui leo hii wangekua na hali gani.

NB: TUKUMBUKE KABLA YA MTU KULIKUA NA MTU NA BAADA YA MTU KUNA MTU
 
CCM wanatakiwa wajifunze kwa hili la Mwendazake, na waache kiburi cha kukwamisha upatikanaji wa katiba mpya isiyopendelea chama chochote cha siasa.

Kwani wakiendelea na kiburi chao wakae wakijua upinzani wanaweza kuingia madarakani kwa katiba hii afu wao wakajikuta ni wapinzani na hapo ndipo watajua ni kwanini samaki Hulia pasipo kutoa sauti.

Chini ya jua hakuna lisilowezekana hivyo ukipata nafasi itumie kutengeneza mazingira ya wewe kuishi siku ukiwa huna hiyo nafasi
 
IMG_20210607_084510.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
word
Ccm wanatakiwa wajifunze kwa hili la Mwendazake, na waache kiburi cha kukwamisha upatikanaji wa katiba mpya isiyopendelea chama chochote cha siasa.
Kwani wakiendelea na kiburi chao wakae wakijua upinzani wanaweza kuingia madarakani kwa katiba hii afu wao wakajikuta ni wapinzani na hapo ndipo watajua ni kwanini samaki Hulia pasipo kutoa sauti.

Chini ya jua hakuna lisilowezekana hivyo ukipata nafasi itumie kutengeneza mazingira ya wewe kuishi siku ukiwa huna hiyo nafasi
 
Mlishawai kujiuliza siku Mbowe akiondoka ghafla kwenda kwa aliemuumba hali itakuwaje Chadema?

Hivi hamuoni kuwa karibu 90% ya akili za wanachadema zinaongozwa na watu 3 yani Kigogo,Mbowe na Lissu ?

Leo JPM amekufa lakini hujaona vurugu yeyote kuanzia Nchi mpk Chama chake leo wana Mwenyekiti Mmama hakuna vurugu wala nini je ingetokea Chadema unadhani ingekuwa hvyo?

Mngeweza kumuachia Chama mwanamke? Baada ya Mbowe kufa ghafla? ikiwa hakuna hata anayejua baada ya Mbowe nani anafata lakini CCM inajulikana kuwa Rais wa nchi ndo mwenyekiti so kikatiba Samia ndo angekuwa Rais automatically anakuwa mwenyekiti .

Leo unasema kusifu na kuabudu hiyo ni Tabia ya watanzania kujifedheesha kwa ajili ya vyeo na fedha leo waimba mapambio wapo kuanzia ngazi ya Familia mpk Taifa

Hv unajua 99% ya Chanachagadema tawi la mitandaoni wanamsifu na kumuabudu Mbowe?
 
Unaposema unadhani maana yake ni kwamba huna uhakika na unachokiuliza.kama ambavyo hamkudhani Jpm ataperish kabla ya muda na akaperish mambo yako kama yalivyo sasa ndivyo ambavyo pia ikitokea mbowe kaded mambo ya chadema yataenda jinsi yatakavyokua.

Mtoa mada kaongelea mambo ambayo yalikuepo na kayashuhudia wewe unaongelea mambo ambayo ata hujui kama yatatokea.sasa kihere here cha nini kuizungumzia kesho ambayo bado haijafika.mengine uliyoandika ni umbea tu.
 
Mkuu sasa Mbowe atamwachiaje chama mwanamke wakati msaidizi Wake ni mwanaume?

Mama kawa hapo alipo kwasababu alikuwa msaidizi wa mwendazake ila mwendazake angekuwa na msaidizi wa kiume basi huyo msaidizi wake ndiye angerithi mikoba.

Team Rungwe.

Nalog
 
Viongozi waliokuwa wanakula maisha awamu ya tano, sasa wanaishi kwa hofu dhidi ya mashitaka yanayoweza kufunguliwa juu yao

Hapo awali Paul Makonda ndiye alikuwa anaongoza kuishi kwa hofu ya kutiwa nguvuni, hongera kwake maana Hamduni ameweka wazi kila kitu kinaenda vizuri.

1. Bashiru Ally
Wakuu huyu jamaa awamu hii inamkondedha kwa mawazo mno! kwa upigaji alioufanya ndani ya mwezi mmoja alipopewa ukatibu mkuu kiongozi hakika hawezi lala

Kila kitu kiko wazi ni suala la muda tu atatiwa nguvuni na shughuli yake itaishia hapo

2. Hamis Kigwangala mzee wa nje ya box
Huyu nae anamsongo wa mawazo hatari. Wengi wanafikiri anastress za kunyimwa uwaziri, huyu anaifikiria PCCB na kuwekwa ndani bila ya dhamana akisubiri hukumu
 
Back
Top Bottom