Kuna wengine hatujui tulipokosea

bila shaka mmeamka salama. lisa nimeamka sasa uchovu wa safari umepungua fuatana na mimi
Ep 6

Tumefika sehemu kwenye nyumba Fulani hivi dirishani nasikia bamkubwa anaita Beti! Beti… (si jina halisi) fungua uje umchukue mdogo wako akapumzike alafu utakuja nae asubuhi nyumbani. Huyu Beti ni dada yangu mtoto wa babamkubwa pale amepanga huwa anaenda kushinda kwao usiku anaenda kwake kulala.

Dada akanichukua akanipa maji nikaoga na kulala. Kumepambazuka asubuhi tumeamka tumeoga tunaenda kwa bamkubwa. Tumefika natambulishwa kwa wenyeji wangu yaani Watoto wengine wa bamkubwa na mke wake. Mke wake toka nipo mdogo huwa nasikia habari zake kuwa ni mjeuri sana na mkorofi. Baba yangu mkubwa ana Watoto wanne na kuna ndugu wa mamkubwa Watoto watatu jumla saba namimi nimekuwa wa nane. Yaani sio Watoto wadogo mabinti na vijana tupo pale.

Imeandaliwa chai tumekunywa pale. Mgeni nimepewa soda stori za hapa na pale na wenyeji wangu. Mazingira ya pale ni uswahilini sana babamkubwa ana nyumba mbili kubwa na ndogo za kawaida sana. Kubwa ina vyumba vingi kuna wapangaji wengi. Pia nyumba ndogo ni inaonekana ya zamani. Nyumba zote mbili hazina umeme wala solar. Kwenye nyumba kubwa kuna sebule ambayo wanatumia familia ya bamkubwa. Ila vyumba vyote vilivyobaki vina wapangaji.

Muda wa chakula cha mchana umefika. Umesongwa bonge la ugali hapo kwa bakubwa ni familia kubwa na mboga inawekwa kwenye bakuli moja imewekwa katikati juu ya ugali watu wanaizunguka sahani na kuanza kula. Lisa mbona sijazoea mambo haya jamani kwa dada nilipotoka ilikuwa self service na kwa babu japo ni kijijini hatujawahi kushare mboga bakuli moja. Hata hamu ya kula sina majamaa wanakula kama wapo vitani mpaka mama mkubwa alinionea huruma na kusema nitakuwa nakula nae. yeye ana chakula chake special hali na watoto wala chakula kama chao ndo ikawa pona yangu. nawaza baba arudi tu anipele kwake.

Naongea na baba kwenye simu ananiahidi ndani ya siku chache ataakuwa amerudi na atnipeleka kwake hivo niwe mvumilivu kidogo. Namimi nanvyompenda baba yangu nitaachaje kuvumilia sasa.

Muda umeenda jioni imeingia naona mamkubwa anawambia ndugu zangu wakawatandikie kuku. Nashangaa mapya haya sasa kuku wanatandikiwa vipi? Ngoja nione naona wanazunguka nyuma ya nyumba wanachukua viroba vimechakaa vimejaa kinyesi cha kuku. Kumbe vilikuwa vimeanikwa vinapelekwa ndani kwenye nyumba ndogo vinatandazwa chini kama kapeti na giza linavyozidi kuingia kuku wanarudi mmoja moja wanaingia ndani. Wana kuku kibao si chini ya kuku 50.

Usiku umeingia tupo nyumba kubwa sebuleni tumekula. Dada beti anapewa maagizo akamtandikie mgeni. Dada anaingia nyumba ndogo kule kulipotandikiwa kuku ana andaa mazingira baadae ananifuata lisa twende ukapumzike mdogo wangu. Nanyanyuka namfuata dada tunaingia ndani nyumba ndogo kuna kachumba kadogo kuna kitanda. Vyombo kibao mandoo kibao mkaa kila yaani makolokolo kibao naonyeshwa kitanda nikalale. Dada ameondo nimepanda kitandani kulala. Huku nimeanza kupakumbuka kanda ya ziwa. Kitanda kile kina wadudu kibao sijawahi kuwaona wala kuwasikia popote. Ukimuua ananuka. Nikipitiwa usingizi kidogo nageuka kitoweo wa wadudu hawa ambao sijui ni wadudu gani wamenikaribisha mjini Morogoro.

Kwa mara ya kwanza na mimi najua kuwa kweli usiku ni mzito hewa chafu ya kuku wadudu wananisurubu. Ukipitiwa na usingizi kuku akivurugwa unaweza msikia mara kakaupanda mguuni mara mkononi mpaka kichwani kuku hawa hawana adabu kabisa na wageni.

Naamka asubuhi vipele mwili wote umevimba nimeanza kuwa na vipele naamka, wenyeji nao wameamka wananiambia pole tunaona Ngozi yako haipatani kabisa na kunguni ona walivyokutoa vipele. Ndo nikagundua kumbe hawa ndo kunguni.

Siku zimesogea baba hatokei zaidi ya kunipiga kalenda ndo nagundua kuwa kumbe haya ndo yatakuwa makazi yangu hapa mjini Morogoro. Kuwa nitatafutiwa shule ila nitakuwa natokea pale kwenda shule. Nagundua pia kuwa kweli baba hana mke, wala nyumba anaishi Tanga kwa sasa na mke wake walishaachana na mke wake ameshaolewa na mwanaume mwingine na ana mtoto mdogo wa huyo mwanaume wake mpya. Baba amezaa nae mtoto mmoja tu.

Na stori fupi kuwa huyo mama yetu mdogo alieachana na baba ndo chanzo mgogoro kati ya baba na mama mpaka kufika hatua ya baba na mama kuachana. Mamadogo alikuwa akifanya kazi bar.baba akienda bar anaweza kulala huko huko. Mama aliposhindwa akamua kuondoka zake Dar kwa ndugu zake. Ila sasa hata huyo mwanamke ameshindwa kuishi na baba. Msjijali huyu mama angu wa kufikia tutakuja kumuona vizuri huko mbele.
 
Tam lakini fupi
 
Ep 7

Siku zinaenda Lisa sina nuru tena kama nilivyotoka kanda ya ziwa nimefubaa nimechoka sina amani wala furaha Maisha ya pale kwa baba mkubwa ni magumu kiasi chake hawalali njaa lakini ni uswahilini sana. Inabidi nizoee japo kibaya hakizoeleki. Ngozi yangu imeharibika sana sababu ya kunguni alama kibao mpaka sasa baadhi ya alama ya vipele vya kunguni ninazo.

Siku zinavyozidi kwenda Ngozi yangu inazidi kuharibika sizoeleki na kunguni nina vipele kibao yaani ilifika hatua hata kunguni akinitambaa tu alipopita naota vipele nimejaa usaha mwili mzima. Dada ananionea huruma na kuamua nitakuwa naenda kulala kwake. Nimepata unafuu kidogo nalala kwa dada. Kama unavyojua binadamu tumeumbiwa kuchoka dada yangu kaanza kunichoka kila nikienda nae kwake ananikasirikia bila sababu anafokafoka tu. Usiku mmoja usiku sana nimelala usingizi na nasikia dada ananiita kwa ukali “Lisa lisa unajigeuzaje kama linguruwe utanvunjia kitanda changu.” Hii kauli iliniuma sana nikakumbuka kanda ya ziwa kwa dada mwingine nilikuwa na chumba changu nalala bila kumsumbua mtu. Kwa babu kijijini pia nilikuwa nachumba changu leo hii nafananishwa na nguruwe. Nililia sana.

Kesho yake naamua kumpigia mama simu na kumweleza matatizo nayoyapitaia. Ananijibu utajijua mwenyewe pambana na shida zako. Tulikwambia usubiri ukakataa ukamchagua tena baba yako kwa mara ya pili wacha wakuue na usinitafute tena. Mweleze baba yako shida zako si ndo kipenzi chako wewe. Akanikatia simu. Nililia sana. Usiku umefika ananiambia twende tukalale nikamkatalia nikasema nitalala huku sababu kesho nataka niwahi kuamka ili niende kanisani kesho yake ilikuwa ni jumapili. Ndo ukawa mwisho wa mimi kwenda kulala kwa dada nikaona ni heri nilale na kuku na kunguni wangu kuliko binadamu wa kunisimanga. Mama yake aliniuliza kwanini sitaki kwenda kulala tena kwa dada nikamwambia hakuna kitu.

Siku za kwenda shule bado kuna shangazi yangu anaishi marekani amerudi ana nyumba Morogoro maeneo ya forest kwa wenyeji wa Morogoro watanielewa. Akaja kunichukua niende kwake kumsalimia nimeenda ninamkuta shangazi yangu kaja na Watoto wake mapacha wa kike na wakiume hao ni wakubwa kwangu natambulishwa kwao. Sasa shangazi ana bonge la jumba nyumba imezungukwa na miti tu ukitoka nje unasikia sauti za ndege tu majirani wapo mbali kidogo.

Shangazi ananionea huruma Ngozi ilivyoharibika anasema ngoja nitaongea na mdogo wangu (baba) uje ukae hapa na ndugu zako. Kule hapakufahi kabisha. Nafurahi kusikia hivyo nakubaliana na shangazi yangu lakini kabla hujaongea na baba inabidi nirudi kwa bamkubwa kwanza alafu mkisha elewana ndo na mimi nije kuishi hapa.

Shangazi amenipeleka hospitali nimepewa dawa Ngozi yangu ssasa inaanza kurudi katika hali ya kawaida.

Kaka angu binamu pacha ananitaka kimapenzi.

Kaka angu ameanza kubadilika hataki nimwamkie, hataki nimwite kaka ananiambia anataka kunioa. Nikawa najua anatania sababu alikuwa mtu wa masiala sana hivyo simtilii maanani.

Shangazi ameenda kwenye mizunguko yake nimebaki na ndugu zangu mapacha mara dada nae anaondoka sijui anaenda wapi. Kaka anamtuma dada wa kazi sijui amemtuma nini tumebaki peke yetu. Kaka ananiita chumbani kwake nimpelekee maji sikuwa na wasiwasi sababu hata shangazi akiwepo ni kawaida sisi kuingia chumbani kwa kaka.

Kaka nampa maji anayaweka mezani mimi nimegeuka naukaribia mlango mara mtu ananivuta na anafunga mlango kwa ndani ana mwili mkubwa kumbuka. Ananiambia ama nikubali kwa ridhaa yangu ama anibake na anambia hata upige kelele hakuna wa kukusaidia make tumebaki peke yetu. Lisa sijawahi kumjua mwanaume nafanyaje sasa. Naanza kulia kaka amevua shati amebaki na pensi sasa ikawa vuta nikuvute humu ndani namwambia mimi ni mdogo wako ananijibu kuwa mimi ni binamu. Mungu yupo kengele inagongwa tena kwa fujo kaka anajisonya huku maneno yanamtoka lazima nikuoe utake usitake. Kengele inaendelea kwa fujo namwomba Mungu anayegonga kengele asiache kaka anatoka ananiambia hatujamalizana na mimi nachomoka ndani nduki naelekea getini kumbe aliyegonga kengele ni dada pacha wake kuna kitu kasahau. Namfata dada naomba tuondoke wote siwezi kukaa na kaka ananitishia ngedele dada nakuomba tuondoke wote. Pale kwenye nyumba yao kuna ngedere wanarukaruka hivyo nikapata sababu ya kumwambia dada.

Dada ananisubiri tunaondoka wote wanamshukuru Mungu kuniponya dada ananidadisi sana lakini naogopa kumwambia. Shangazi anarudi nageuka mkia wa shangazi kila akitaka kwenda sehemu naanza kujiliza ili niondoke nae. Shangazi anasema unadeka sana wewe ndo tatizo la Watoto kulelewa na babu na bibi baba amekudekeza sana wewe. Narudi kwa bamkubwa namwambia shangazi baba akikuba tu nitakuja kukaa na kina kaka.

Nampigia baba simu na kumwambia kuwa sitaki kukaa kwa shangazi naomba usikubali baba ananiuliza tatizo namwambia ngedere. Sitaki hata kuwaoana nawaogopa sana bora nikae tu bamkubwa sitaki kabisa kuwaona ngedere mara kwa mara.

Narudi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…