Kunahitajika Chombo Huru cha kulichunguza Jeshi la Polisi, operesheni ya kukamata wanaotuhumiwa kuhusika na biashara ya ukahaba yaibua mengi

Kunahitajika Chombo Huru cha kulichunguza Jeshi la Polisi, operesheni ya kukamata wanaotuhumiwa kuhusika na biashara ya ukahaba yaibua mengi

passion_amo1

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2023
Posts
1,828
Reaction score
3,922
Wakuu Heshima mbele.

Tangu kutokee sekeseke la kukamatwa kwa wanaodaiwa ni “madada poa” nimeona kuna haja kubwa sana kuwe na chombo huru cha kuchunguza mienendo ya jeshi la Polisi na Polisi kwa ujumla.

Video inayoonyesha wanaodaiwa ni madada poa wakiwa wanalalamika unyanyasi waliopotia. Wamefika kituoni wakapelekwa garage nafikiri tuliowahi kulala polisi tunaelewa garage ni sehemu ya namna gani.

Wamefika huko wanaambiwa anzeni kuvua nguo zenu, tanueni mapaja na mambo mengine mengi ya kutweza na kudharirisha utu wa mwanamke ambao kimsingi ni dada na mama zetu.

wengine wanadai walikuwa wakiomba msaada wa taulo za kike lakini walikuwa wakijibiwa kwamba tafuta njia ya kujisitiri unayoyajua. Na mwingine alikuwa akiambiwa nikufungulie Mlango uje chooni ili tumalizane.

Kiukweli aliyetoa hii Amri anapaswa kuwajibishwa kwa udharirishaji alioufanya.Polisi hawa hawa ambao mishahara yao tunaifahamu na maisha yao mtaani tunayafahamu ndio wamekuwa wakifanya vitendo ambavyo si sahihi katika jamii.

Kwanini pasiundwe chombo huru cha kushugulikia tuhuma hizi zinazofanywa na Polisi? Hii inachafua jeshi zima la Polisi, Kwanini watuhumiwa wananyimwa dhamana wakati ni haki yao?

Sijui ndugu yangu Abdul S Naumanga mnasubiri nini kushugulika na kesi kama hizi?

Yaani binti anamuona mama mtu mzima Makamu ya mama yake anavuliwa nguo na kuambiwa atanue mapaja?! Kweli Polisi limefikia hatua hii?

TUENDELEE KUAMKA NA KUPINGA UONEVU UNAONDELEA KWA KUENDELEA KUDAI KATIBA MPYA ITAKAYOTULINDA WOTE.


=====

Pia soma:
Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili
 
Shida aliyefanyiwa hivyo ni Mwanamke right? Mnajua pia hata Wanaume wanapitia changamoto? Kupanua mapaja nayo inawauma?..

Juzi nilienda kumtoa mtu Stakshar moja hivi..

Kuna watu walikuw wametok kutembezewa (Kiminyo) kuna mwendo unaitwa kutembea kama Penguin.. hicho kiminyo wangetembezew hao Dada poa nafkir mpk Marekani wangeingilia kati.

Mjitahidi kuangalia pande zote mbili na sio kisa jnsia fulani.
 
Shida aliyefanyiwa hivyo ni Mwanamke right?
Gentlemen,

Shida ni mkuu wa wilaya Hassan bombproof aliyeamua kutumia ubabe kwenda kukamata watu ndani ya vyumba vyao wakiwa faragha na kudai kwamba hao ni madada poa wanaojiuza.

Mnajua pia hata Wanaume wanapitia changamoto?
Ninaelewa sana mkuu. Tofauti ndogo tuliyonayo na watoto wakike wao huongea tofauti na mtoto wa kiume.
Mjitahidi kuangalia pande zote mbili na sio kisa jnsia fulani.
Gentle

Upo sahihi kabisa
 
Sijui ndugu yangu @Abdul S Naumanga mnasubiri nini kushugulika na kesi kama hizi?
Ndugu yangu kwanza suala la kesi si Adv.Madeleka ana deal nalo brother, lakini Binafsi pia nakubaliana nawe kabisa kuhusu umuhimu wa kuwa na chombo huru cha kuchunguza mienendo ya jeshi la Polisi na Polisi kwa ujumla. Vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji kama vile ulivyoelezea vinapaswa kushughulikiwa kwa uwazi na kwa kina.

Chombo hicho kitasaidia kupunguza hisia hasi juu ya jeshi hilo na kuhakikisha kuwa maafisa wanaohusika wanawajibishwa kwa vitendo vyao. Pia, kingeongeza ufanisi na umakini katika utendaji wa jeshi la polisi nchini.

Kwahiyo mzee, ni muhimu kuendelea kuhamasisha na kupinga vitendo vya unyanyasaji na kudumisha haki na usawa katika jamii yetu. Asante kwa kuleta suala hili jamvini na kutoa wito wa hatua zaidi🤝.​
 
Shida aliyefanyiwa hivyo ni Mwanamke right? Mnajua pia hata Wanaume wanapitia changamoto? Kupanua mapaja nayo inawauma?..

Juzi nilienda kumtoa mtu Stakshar moja hivi..

Kuna watu walikuw wametok kutembezewa (Kiminyo) kuna mwendo unaitwa kutembea kama Penguin.. hicho kiminyo wangetembezew hao Dada poa nafkir mpk Marekani wangeingilia kati.

Mjitahidi kuangalia pande zote mbili na sio kisa jnsia fulani.
Nadhani hoja kuu ni kuundwa kwa chombo huru cha kuchunguza mienendo ya jeshi la Polisi na Polisi na hakitokuwa kwaajili ya wanawake tu NO bali pande zote mbili (ME & KE), suala la madada poa limekuja ku trigger call for action tu.​
 
CHOMBO HURU kwa maana ipi??

Kitapewa mamlaka yepi kuhusu hukumu dhidi ya polisi itakayokutwa na hatia???,isijekuwa ni kupiga makelele tu baada ya kubaini makosa.

KItatumia mhimili upi kama nguzo ya kusimama,kikiwa kinatekeleza majukumu yake,mahakama,bunge,serikali kuu??

Kitaundwa na watanzania aina gani??wahanga wa manyanyaso,wanaharakati,mtanzania yeyote tu atakayejisikia,au tutakodisha FBI??

Ipi itakuwa taasisi ya kuhakiki,taarifa za taasisi hiyo kwamba ni za kweli,hazina upendeleo,njama,ama maslahi yoyote kinyume na kutafuta haki na weledi kwa jeshi la polisi??
 
Nchi zisizoendelea ni shida tupu, ndomaana watu wengi hupenda kuishi nchi kama Marekani na Canada maana wanajali sana haki za Binadamu.
 
Back
Top Bottom