Kunyimwa vyeti udom

mansakankanmusa

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
4,162
Reaction score
796
serikali iliangalie suala hili kwa sura ya nje sio ya utawala wa chuo

sababu aliyotoa waziri kuhalalisha kunyima vyeti wanafunzi kwa sababu eti waligoma kusaini

sio sahihi. wawaite wawasikilize

source: BUNGE LA TZ
 
Mbona hueleweki, waligoma kusaini nini sasa?
 
Wanafunzi wa UDOM tangu wachangishane pesa za jk kuchukua fomu za kugombea urais,mimi siwathamini tena, ila kama walikataa kusaini fomu za mkopo kwa mujibu wa Dr. Kawambwa wanatarajia hiyo mikopo wangepata je na inashangaza chuo kiliendeleaje kuwaruhusu waendelee kusoma wakati mikopo haipo!kama kuna sababu zingine ambazo zimesababisha wasipewe vyeti waseme!
 
Mbona hueleweki, waligoma kusaini nini sasa?

Kwa mujibu wa Dr. Kawambwa wanafunzi waliokosa vyeti ni wale waliokataa kusaini fomu za mikopo hivo mikopo yao haikuja walipomaliza wanatakiwa walipe mikopo hiyo ndio wapewe vyeti! maana bila kusaini fomu za mikopo wangepewaje mikopo??
 
Kwa mujibu wa Dr. Kawambwa wanafunzi waliokosa vyeti ni wale waliokataa kusaini fomu za mikopo hivo mikopo yao haikuja walipomaliza wanatakiwa walipe mikopo hiyo ndio wapewe vyeti! maana bila kusaini fomu za mikopo wangepewaje mikopo??


hapo nimeelewa, nawapa pole sana ila ndio mfumo wa nchi yetu. Wasubiri tu 2015 walipe kisasi. Mi sidhani kama waligoma ila ni mfumo mbobu wa uongozi wa chuo na ukosefu wa utaratibu kwa ajili ya usainishaji.
 
hapo nimeelewa, nawapa pole sana ila ndio mfumo wa nchi yetu. Wasubiri tu 2015 walipe kisasi. Mi sidhani kama waligoma ila ni mfumo mbobu wa uongozi wa chuo na ukosefu wa utaratibu kwa ajili ya usainishaji.

Kawambwa kasema wamegoma wachache wengi wao wamepewa vyeti kwa kuwa walisaini fomu za mikopo na bodi ya miikopo ikapeleka mikopo chuoni hawa vichwa maji ndio waligoma matokeo yake hawana vyeti hadi sasa na wameambiwa pesa ambaye walitengewa ya mikopo imerudi hazina na imelipia wanafunzi wengine maana hawa walikataa kusaini ili wapewe!!
 
hapo nimeelewa, nawapa pole sana ila ndio mfumo wa nchi yetu. Wasubiri tu 2015 walipe kisasi. Mi sidhani kama waligoma ila ni mfumo mbobu wa uongozi wa chuo na ukosefu wa utaratibu kwa ajili ya usainishaji.

asilimia karibu ya 90 ya viongozi wa inchi hii hususan magamba wanaongea kitu wasichokifaham.
 
hapo nimeelewa, nawapa pole sana ila ndio mfumo wa nchi yetu. Wasubiri tu 2015 walipe kisasi. Mi sidhani kama waligoma ila ni mfumo mbobu wa uongozi wa chuo na ukosefu wa utaratibu kwa ajili ya usainishaji.

2015 katiba mpya. Uongozi mpya, lakini si magwanda, hilo sahau.
 
2015 katiba mpya. Uongozi mpya, lakini si magwanda, hilo sahau.


Kwani mimi nimetaja Magwanda na magamba hapo? mi nimesema wasubiri 2015 walipe kisasi, 2015 ina uhusiano gani na magwanda?
 
Ndio mfumo uliopo huo lakini una mushkeli. Wakati tupo mwaka wa pili chuoni ilitokea incident kama hiyo, watu hawakusaini pesa zao, chuo kikadai zimerudi bodi. Vijana wakaenda bodi sio kudai pesa zirudi chuo bali wakataka wapewe barua maalum zinaonyesha kuwa hawakulipiwa 2nd semester of 2nd year.

Hapo ndipo bomu lilipolipuka, kumbe zile pesa bado zilikwepo chuo, maofisa wa chuo na bodi kwa pamoja walikuwa wanasubiri jamaa wamalize waje kupiga ile pesa at the end jamaa waje kudaiwa kama walipewa. Haikupita muda, vitabu vikaletwa tena chuo na watu wakasaini kama kawaida, watu walisaini 2nd semester fee of the 2nd year wakati tuko last semester 3rd year.
 
Kwani mimi nimetaja Magwanda na magamba hapo? mi nimesema wasubiri 2015 walipe kisasi, 2015 ina uhusiano gani na magwanda?

Achana nae huyo akilala anaota magwanda. kwa ujumla yy muda wote anawaza magwanda 2.
 
Achana nae huyo akilala anaota magwanda. kwa ujumla yy muda wote anawaza magwanda 2.

Kwa sababu kazaliwa kipindi hiki jamaa yetu yupo madarakani tusimlaumu sana, lakini sisi tunayo kumbukumbu nzuri ya NCCR ya Mrema hivyo hatushangai sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…