Kunywa madafu kwa wingi ni hatari kwa uhai wako

Kunywa madafu kwa wingi ni hatari kwa uhai wako

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Habari ndugu zangu. Nimekuja kuwatisha tena. Maji ya nazi/madafu yana madini ya potasium kwa wingi sana. Matunda kama machungwa na ndizi yana potasium kwa wingi lakini hayagusi hata kidogo kwa madafu.

Sasa basi. Potasium kazi yake kubwa ndani ya mwili ni kujihusisha na masuala ya umeme. Mishipa ya fahamu, kureguralte midundo ya moyo nk nk. Madini ya potasiumu yakizidi mwilini(Hyperkalemia) husababisha moyo kupiga bila mpangilio mzuri(arrythmia) jambo hili ni hatari na linaweza sababisha kifo.

Tabu hii huwapata hasa wale wenye matatizo ya figo, maana figo inashindwa kuondoa potasium kwa kasi kama inavyoingia.

Pia sijajua namna pombe ya mnazi inatengenezwa, kama inatumia maji ya dafu basi hatari ya hyperkalemia kwa wanywa mnazi ni kubwa sana. Maana pombe mtu anaweza piga lita kadhaa. Chukua tahadhari.

=====

Taarifa hii imefanyikwa kazi kwenye Jukwaa la Jamii Check. Soma: Madafu ni hatari kwa watu wenye ugonjwa wa Figo
 
Hii ni concept.... inafaa kufanyiwa tafiti.

Kuna maswali mengi yanahitaji majibu

1. Je dafu moja lina potassium kiasi gani?

2. Je mwili wa binadamu unahitaji potassium kiasi gani?

3. Baada ya muda gani kiwango kipya cha potassium kiwe kinaingia mwilini?
 
Habari ndugu zangu. Nimekuja kuwatisha tena. Maji ya nazi/madafu yana madini ya potasium kwa wingi sana. Matunda kama machungwa na ndizi yana potasium kwa wingi lakini hayagusi hata kidogo kwa madafu...

Mwili una kazi ya kuregulate hizo minerals,ndio kazi za figo,labda kama mwili una shida ya figo ndio utoe hiyo warning.
 
Back
Top Bottom