Kuomba Msamaha ndani ya mahusiano!!


.... Nigeieni basi na mimi hii bahati? maana mie weza nuna hadi jua likashuka na msamaha usiombwe hata kama kakosa yeye....... yaani nimechoka kabisa
 
.... Nigeieni basi na mimi hii bahati? maana mie weza nuna hadi jua likashuka na msamaha usiombwe hata kama kakosa yeye....... yaani nimechoka kabisa


pole sista.... hivi bado hujatatua yale mambo?? wanaume wa aina hiyo wanaudhi sana.. sijui huwa ndiko kuonyehsa ushujaa ama hawataki kuonekana kuwa na weakness... jamni kuomba msamaha isnt a sign of weakness but of respect, love and thats what real gentlemen do! mmm pole aisee sasa umemuaje dadangu? I feel your pain as a sista!
 

......... dada na visa kila kiukicha vinaibuika- nadhani ni yale ya akufukuzaye hakwambii toka.
 

Mkuu Mbu, nakuunga mkono kabisa yote unayoyasema lakini wengine ni Bullies ukiamua kumignore hapo ndiyo ataongeza jingine sasa kwamba unamdharau kwa kutomsikiliza anayoyasema na kuongeza ugomvi na kuwa mkubwa zaidi na yeye kudhani kwamba unamdharau kwa sababu kuna mtu anayekuvimbisha kichwa anakufundisha kiburi etc, kumbe wala hakuna mtu kama huyo bali umechoshwa na kelele zisizo na kichwa wala miguu ambazo hutokea karibu kila siku iendayo kwa mungu.

Kuomba msamaha kwa maoni yangu si kitu cha ajabu lakini inabidi iwe ni 2 way traffic wanaume nao wawe tayari kusema 'samahani' pale wanapogundua kwamba wamekosea na si mwanamke tu ndiyo awe muomba msamaha kila anapokosea vinginevyo itafikia wakati na yeye ataamua kuomba msamaha sasa basi, hata anapojua fika kwamba amekosea.

Wanaume wengine wanajisikia sana kiasi ambcho kutamka neno 'samahani' ni kujishusha hadhi yao kama wanaume hivyo hata wanapojua fika kwamba wamekosea hawawezi kulitamka neno hilo. Hili ni kosa kubwa kama mnataka kujenga uhusiano wa kuheshimiana kati yenu maana hakuna binadamu ambaye yuko perfect na asiyefanya makosa na pia makosa madogo madogo tunaweza kabisa kuyamezea badala ya kutaka kuanzisha kasheshe kila unapoona kosa hata kama halina athari yoyote katika uhusiano wenu.
 
Last edited:


Ndugu yangu...
nakupongeza sana kwa kutokuwa biased.Hujapendelea wanaume wenzio kama ambavyo ingeweza kufanywa na mwanaume mwingine kulinda ego.
Ni watu kama wewe mtakaobadilisha hali ya unyanyasaji katika mahusiano.Im sure kama kuna bullies humu wanasoma mchango kama huu basi wataona haya na kufikiria kubadilika.Ungegombea ubunge nakuhakikishia ningekupigia kampeni na ungepata kura za wanawake wote kiulainiiiiii.
 
WoS na BAK mnaleta uBeijing. Mwanamme akosehi bwana na hakuna sababu ya kuomba msamaha.
 
WoS na BAK mnaleta uBeijing. Mwanamme akosehi bwana na hakuna sababu ya kuomba msamaha.
We Za10!
Unataka kusema nini sasa? yaani mtu aseme kile ambacho hakipo au siyo ukweli anaoamini just because atakutana na backlash kama hivi?
Usidanganye wenzio.Tena mtu kama wewe utakuta mwepesiii kuomba msamaha.Halafu hapa unawadanganya wenzio wakomae tu!!
 

WoS:

Mi mgumu sana LOL. Kuombaomba msamaha ni dalili za udhaifu. Mwanamme lazima uwe na Ego hata kama umechemsha.
 

Ha ha ha ha ahsante sana jirani kwa maneno yako mazuri. Ni kweli kwenye haya mambo inabidi usiwe biased hata kidogo vinginevyo jambo dogo linaweza kuwa kubwa kabisa na kujenga chuki ndani ya nyumba. Kama unampenda mkeo/mumeo na unajua umetenda kosa ukiomba samahani hutapungukiwa na chochote na mwenzio atakuthamini sana kwa kumuona unamuheshimu.

Kuhusu kugombea Ubunge ha ha ha ha jirani hunitakii mema unataka mafisadi waanze kunitumia jumbe zenye vitisho na si ajabu kupanga mikakati ya kunikolimba au kunibalali!? Juzi tu wamemkosakosa Mwakyembe? Dr. Slaa wameshamtisha vya kutosha na kumuwekea vidaka sauti ndani ya chumba chake na hadi hii leo wahusika hawajulikani na kuzomea Wabunge wa CCM wanamzomea bungeni kwa kutetea maslahi ya Watanzania.

Ningekuwa nafikiria kugombea jirani, wewe ungekuwa kampeni Meneja wangu najua kabisa ningepita kwa kazi nzuri ambayo ungeifanya ha ha ha ha lakini hili la kuishi roho juu juu kutokana na vitisho vya mafisadi linaogopesha, tutapambana nao tu pembeni hata kama hatuna nyadhifa za waheshimiwa mpaka tuikomboe nchi yetu toka mikononi mwa mafisadi tumeanza kupata mafanikio madogo ambayo yanatia moyo sana jirani.
 
WoS na BAK mnaleta uBeijing. Mwanamme akosehi bwana na hakuna sababu ya kuomba msamaha.

Mwanaume hakosei kwa sababu tuko perfect! Wenye makosa siku zote ni wanawake! Halafu mke akiamua kuondoka ndiyo mtu anaanza kusikitika, Ooohhh! I made a big mistake I am still in love with my wife.

Nilichoandika nimeandika kutokana na uzoefu niliokuwa nao katika kusuluhisha ndoa ambazo zimenihusu kabisa ana kwa ana na wahusika au hata kupitia njia ya simu kwa masafa marefu, na hakina ubeijing wowote.

Wote walikubali bado wanapendana na kila mmoja anamtuhumu mwenzake kafanya makosa katika ndoa ambayo yamesababisha migongano ndani ya nyumba.

Na neno sahamahi ndilo mara nyingi lilinisaidia katika kurudisha amani katika nyumba za wana ndoa hao kwa kuwaambia kila mmoja kamkosea mwenzie sasa muombane samahani na hayo makosa mjitahidi msiyarudie ili kujenga upendo na amani ndani ya nyumba zenu.

Ndoa mbili kati ya hizo nilizoshiriki kutafuta amani kwa kweli nilikuwa sina matumaini kabisa kutokana na makosa ya wahusika lakini hadi hii leo bado wanadunda pamoja kama mke na mume kwa sababu ya kukubali makosa yao na kuwa tayari kulitamka neno samahani.

Wewe unayeamini kwamba Wanaume huwa hatukosei kwa sababu Mungu katuumba perfect endelea na imani yako hiyo.
 
Last edited:
Mwanaume hakosei kwa sababu tuko perfect! Wenye makosa siku zote ni wanawake! Halafu mke akiamua kuondoka ndiyo mtu anaanza kusikitika, Ooohhh! I made a big mistake I am still in love with my wife...

...ha ha haa... eti ' i made a big mistake!' 😀

unajua bro BaK, nishasikia binti anaambiwa kwenye send offs au kwenye tafrija za harusi huko aendako amtii mumewe, ...huko aendako mumewe ndio kichwa cha nyumba,... mwisho wana ndoa hao huaswa kuzingatia maneno matatu; samahani, nimekosa, nisamehe!

Wanaume wengi huyatumia maneno hayo matatu pale anapofumaniwa tu, kinyume na hapo hata umshikie panga hatamki ng'ooo...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…