“Kuondoa hatari” ni hila ya Marekani ya kutenganisha China katika mambo ya uchumi na biashara

“Kuondoa hatari” ni hila ya Marekani ya kutenganisha China katika mambo ya uchumi na biashara

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111439134933.jpg
Hivi karibuni, “kuondoa hatari” kumechukua nafasi ya “kutenganisha” kama neno jipya linalotumiwa zaidi na wanasiasa wa Marekani kuhusu China. Mkutano wa kilele wa Kundi la Nchi 7 (G7) uliofanyika mwezi uliopita ulitoa taarifa ikisema kuwa, nchi hizo 7 zinazoongozwa na Marekani zitajitahidi kuondoa hatari za kiuchumi zinazotokana na China. Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken hivi majuzi kwa mara nyingine alitetea “kuondoa hatari”, akisema kwamba Marekani na nchi za Ulaya hazitaki mivutano, au vita baridi ya “kupingana na China”, bali zinalenga “kuondoa hatari”.

Kuna hadithi moja ya Kichina, ambayo inasema zimwi mlawatu ana sura ya kutisha, ili kudanganya watu, hujipamba kama mrembo. Marekani inajitahidi kutengana na China katika mambo ya kiuchumi na kibiashara. Baada ya kupingwa kwa kauli moja na jumuiya ya kimataifa, ilibadilisha sura yake na kusema inataka kuondoa tu hatari zinazosababishwa na China. Kitendo hicho ni sawa na hadithi ya zimwi mlawatu.

Katika miaka ya hivi karibuni, Marekani imezidi kuwa na “wasiwasi” kuhusu China, na imefanya mambo mengi ili kuzuia maendeleo ya China. Katika sekta ya uchumi na biashara, Marekani imewekea China vikwazo vingi, na zaidi ya hayo, imezichochea nchi nyingine haswa zile zilizoendelea, kuchukua hatua kama hiyo dhidi ya China. Hata hivyo, China ni nchi ya pili kwa uchumi duniani, nchi kubwa zaidi ya kiviwanda, na mshirika mkuu wa biashara wa zaidi ya nchi 140 duniani. Kuvunja uhusiano wa kiuchumi na kibiashara na China kwa kweli kutadhuru sana maslahi ya nchi hizo. Ripoti iliyotolewa na taasisi moja ya utafiti ya Ulaya inakadiria kwamba, ikiwa Ujerumani itatengana na China kiuchumi na kibiashara, pato lake la ndani la kila mwaka litashuka kwa asilimia 2. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema wazi kwamba Umoja wa Ulaya na China zinapaswa kufanya juhudi kwa pamoja ili kutoingia kwenye mtego wa kutengana. Hata nchini Marekani, watu wengi, haswa wale wa sekta za uchumi na biashara, wanapinga msimamo wa serikali yao dhidi ya China. Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tesla ya Marekani Elon Musk, amesema maslahi ya Marekani na China yamefungamana, kama mapacha walioungana.

Baada ya kushindwa kushawishi pande nyingine kutengana na China moja kwa moja katika mambo ya uchumi na biashara, serikali ya Marekani imetafuta njia nyingine mbadala. Baada ya kutangaza “kuondoa hatari” dhidi ya China kwa mara ya kwanza kwenye mkutano wa kilele wa G7, hivi karibuni Marekani iliitisha mkutano wa mawaziri wa nchi za bahari ya Hindi na Pasifiki, na mkutano wa biashara kati ya Marekani na Umoja wa Ulaya, ili kutetea “kuondoa hatari” dhidi ya China. Marekani inadai China imeleta hatari nyingi kwa uchumi wa nchi zilizoendelea, ili kuvutia nchi nyingine kupingana na China katika mambo ya uchumi na biashara.

Kitendo cha Marekani kimeamsha umakini wa jumuiya ya kimataifa. Naibu Waziri Mkuu wa Singapore Wong Xun Choi amesema, kauli ya “kuondoa hatari” dhidi ya China badala ya “kutengana na China” pia itasababisha kugawanyika kwa uchumi wa dunia, hali ambayo italeta changamoto kubwa kwa biashara na uwekezaji duniani.

Uundaji na maendeleo ya minyororo ya kimataifa ya uzalishaji na ugavi ni matokeo ya soko. “Kutengana” au kinachodaiwa kuwa “kuondoa hatari” dhidi ya China, sio tu kwamba kutazidhuru nchi zinazohusika, lakini pia kutaleta hatari kubwa kwa utulivu wa minyororo ya kimataifa ya uzalishaji na ugavi, na pia kusababisha uharibifu wa kudumu kwa uchumi wa dunia. Nchi zinazohusika zinapaswa kugundua hila ya “kujipamba kwa zimwi mlawatu”, na kurudi kwenye biashara huria na uchumi unaofungua mlango.
 
Ukisoma maandiko ya mtu anaeish kweny umaskin utagundua kuwa hata akili zake zipo ivo ivo yaan hawa waswahili wasiotaka hata kupost chochote kuhusu bandar yao basi wanahisi na duniani huko kupo hivyo, China kaharibu soko la mabeberu duniani kote kwa kuduplicate brands zao na kuleta copy za bei nyepesi kiufup Ulaya sio wajinga kumsikiliza tu USA bila ushahidi pia wao Ulaya wamepoteza vingi kwasababu ya China so hao hawajanishinikizwa wazungu sio wajinga kama wewe, kutwa unazungumzia mambo ya nje ila hapa kwetu kunafuka moshi hata kuposti picha ya bandari huez halaf upo bize kuunga unga story kuhusu West,

Binafsi naamin ukifika muda mtagundua ubaya wa hiyo east block nmpitia documentary nyingi huo upande wa east block mchafu sana kwasasa kuna biashara ya utumwa inafanywa na huo upande na hatari sna inasikitisha kuona hii mijitu meusi haitak kufuatilia na kutwa wanashabikia huo upande wa east, nmeona watu wengi wa east block wanawambia upande wa dunia utakuta haki ni huo wa west, ebu anzeni hata na hii ya MAID IN HELL.

PIA BLOOD ON SEAS (ingawaje hii nahis ilofungiwa mitandaoni inatisha) pia ipo RACISM FOR SALE (Huyo mchina anaongea kabisa kwamba sis weusi hatuna akili na hatupaswi kupewa haki zetu na ni wavivu sana kiubunifu) Ebu waafrika fanyeni research kabla hamjashabiki jambo.

CHINA NI HATARI KWA DUNIA, MAANA AKITUA KWAO ANAUA MFUMO MZIMA WA VIWANDA KWA KULETA BIDHAA FAKE ZA BEI NYEPES, WENZETU KENYA ANGALAU WANAJARIBU KUCHUKUA HATUA ILA HATA BONGOLALA BADO SANA.
 
Ukisoma maandiko ya mtu anaeish kweny umaskin utagundua kuwa hata akili zake zipo ivo ivo yaan hawa waswahili wasiotaka hata kupost chochote kuhusu...
Sio ajabu wewe ni mama wa watoto wawili kabisa alafu unaandika upuuzi!

Hao wamagharibi wamekusaidia nini nje ya kukubana usiendelee huku wakikulazimisha ufuate maadili yao ya ufirauni?
 
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema wazi kwamba Umoja wa Ulaya na China zinapaswa kufanya juhudi kwa pamoja ili kutoingia kwenye mtego wa kutengana.
Macron ni miongoni mwa viongozi wa Ulaya wanaojielewa sana he is so smart.
 
China anachojaribu kufanya ni kufurukuta tu lakini uhalisia ulivyo hata pro Russia na pro china sometimes Huwa wanaukiri
Screenshot_20230512-182546.jpg


Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom