Kuondoka kwa Hayati Magufuli kumewavua nguo wapinzani

Kuondoka kwa Hayati Magufuli kumewavua nguo wapinzani

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Nimetafakari nikakumbuka story ya jamaa waliokuwa wanamkimbiza mwizi ila hawamjui (hawana target). Kufika sehemu wakaanza kuulizana mwizi yuko wapi kila mtu hata mimi sijui.

Kuondoka kwa JPM kumewavua nguo wapinzani.

1: Imethibitika huwa wanapinga watu na sio mfumo uliopo dhidi ya mfumo mbadala wanaouamini.

2: Sasa hivi kama wamepigwa butwaa wanashindwa wanzie wapi. Wampinge mama au washambulie Marehemu. Wapowapo tu bila dira.

3: Hawana dai moja lenye consistency ambalo hata kama chama tawala kibadilishe mtawala wao wapigekelele yenye kiwango hichohicho. Ni kama watu wanaofukuza upepo, unakoelekea nak wanakimbizia huko.

4: Sasa hivi ndio ilikuwa fursa ya kutushawishi wananchi maana mambo mengi yako neutral. Ila naona kama wanaviziavizia kutafuta viudhaifu wapate pa kuanzia kufanya mihadhara.

5: Wanaichukia CCM wakati wanamsifia Rais wa CCM. Haijulikani wakati uliopita walikuwa wanampinga rais au taasisi nzima iliyokuwa inatawala maana wanayemsifu ndiye mshauri pia wa yaliyopita.

Wapinzani mmeacha ombwe kubwa sana, akitokea mtu mwenye akili na rasilimali fedha na ushawishi anaweza kuanzisha chama bora msimu huu kinachoweza kufuta Chadema, CUF, ACT n.k maana wameshindwa kujua kuna mapinduzi makubwa sana ya kimtazamo wa kisiasa hadi kwa mtanzania asiyejua kitu sasa kuliko miaka 6 iliyopita. CCM wanajitahidi kuwa agile wakinyumbuka kila kukicha wakati wenzao wako rigid wakiishi kwa kitegemea tuhuma na tetesi na sio mipango.

Yangu ni hayo tu.
 
Mama jana kasema jukumu la ulinzi wa afya yako linaanza na wewe. Kwa hiyo wahi hospital ukwapimwe afya ya akili
Tangu lini Nyumbu wakamtakia mema rais Samia hadi wampangie cha kufanya?

Hangaikeni na mzee wa MIGA mtetezi wa mashoga.
 
Ndugu ya ngu matunduizi mtu asiye weza kushukuru kwa wema kidogo hata kwa wema mwingi hataweza,kuwa mwazi hayo kweli una Manisha unayosema,au chemsha bongo kwa jukwaa.
 
Ni mpinzani gani amekufa kwa corona?
 
Hivi lini tutamaliza arubaini tuachane na mambo ya marehemu
 
walisema hawamtambui JPM na uongozi wake ila hao hao wanamtambua Mama Samia maajabu. hawautambui uchaguzi wala bhnge ila wanamtambua kiongozi mkuu mashikolo

JPM kawaacha wakiwa hawaelewi waanze kushambulia wapi
 
Tangu lini Nyumbu wakamtakia mema rais Samia hadi wampangie cha kufanya?
Hangaikeni na mzee wa MIGA mtetezi wa mashoga.
Mzee wa MIGA alibobea kutukana. Sasa hivi hana pa kukanyagia.
 
walisema hawamtambui JPM na uongozi wake ila hao hao wanamtambua Mama Samia maajabu. hawautambui uchaguzi wala bhnge ila wanamtambua kiongozi mkuu mashikolo

JPM kawaacha wakiwa hawaelewi waanze kushambulia wapi
Uchonganishi Mama kakataa keanu hamumwelewi.
 
Back
Top Bottom