Kupambana na watu wasiojulikana: Ukija kukamatwa na polisi bila uniform na hajaambatana na kiongozi wa eneo husika piga firimbi, kusanya nzi

Kupambana na watu wasiojulikana: Ukija kukamatwa na polisi bila uniform na hajaambatana na kiongozi wa eneo husika piga firimbi, kusanya nzi

Mimi nilikamatwa wiki jana kwenye kituo kidogo cha polisi. Wakasema wanasubiri afande wao mwenye V mbili, nikasubiri mpaka jioni nikaona hawaji. Nikaomba kwenda haja nikatoroka. Kesi yenyewe ya kuhisiwa tu
 
Siku za karibuni kumekuwa na mambo mabaya ya kutisha, mambo ya kishetani kabisa, watu kutekwa na wengine kupotezwa moja kwa moja.

Utekaji huo mara nyingi umehusishwa na Polisi au watu wa usalama wa Taifa. Na wananchi wengi wameamini hivyo kutokana na mazingira ya matukio. Baadhi ya watekaji walipoenda kuwateka watu walijitambulisha kuwa wao ni polisi, na kwamba walikuwa wanawachukua kuwapeleka vituo vya polisi, lakini watu hao waliotekwa hawakuonekana kwenye kituo chochote cha polisi.

Polisi kwa upande wao wamekataa katakata kuwa wao hawahusiki na utekaji watu.

Kwa hiyo ina maana watu wamekuwa wakitekwa na maharamia kwa kutumia jina la polisi, na polisi hawawajui watekaji. Kwa mazingira hayo, polisi hawawezi kutuhakikishia usalama wananchi, kwa vile hawawezi kuwepo kila mahali, hivyo yatubidi wananchi tushiriki kwenye ulinzi wetu na wa wananchi wenzetu. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tunashirkiana kikamilifu na polisi kwenye ulinzi wa Taifa letu dhidi ya haya maharamia.

Kama kuna mtu yeyote anatakiwa kukamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma zozote zile, taratibu za kumkamata mtuhumiwa wa uhalifu zipo wazi. Miongoni mwa taratibu hizo, ni pamoja na:

1) Polisi atafika ofisi ya Serikali ya mtaa au kijiji kuujulisha uongozi wa kijiji au mtaa kuwa kuna mtuhumiwa anayeishi eneo hilo wamekuja kumkamata. Na uongozi wa mtaa au kijiji utaambatana na polisi kwenda nyumbani kwa mtuhumiwa.

2) Polisi watajitambulisha kwa mtuhumiwa, na wataeleza kuwa wamekuja kumkamata kwa tuhuma ambazo watazitaja.

3) Kama kutakuwa na upekuzi, mtuhumiwa atakuwa huru kumwita mtu yeyote kuwa shuhuda wa upekuzi.

4) Mtuhumiwa akiwa mikononi mwa polisi ana haki ya kuwasiliana na ndugu zake au wakili wake na kumjulisha kuwa amekamatwa, anapelekwa kituo cha Polisi.

Hivyo basi:

1) wananchi tuwe macho na tuwe makini, usikubali kuondoka na watu ambao wamejitambulisha tu kuwa ni polisi, huku hawajafuata taratibu hizo zote wala hawajakupa kitambulisho chochote cha kuthibitisha kuwa hao waliojiita ni polisi, kweli ni Polisi.

2. Wananchi ambao tupo karibu, ikitokea watu tusiowajua wanamchukua mwananchi mwenzetu kwa nguvu, kwa kusema tu wao ni polisi, huku hakuna uhakika wowote, na wala hawajafuata taratibu ambazo polisi hutumulia kumkamata mtuhumiwa, moja kwa moja tujue kuwa hao watu ndio maharamia yenyewe yenye lengo la kumpoteza mwananchi mwenzetu. Hivyo ni muhimu kuchukua hatua za haraka ili kumwokoa mwenzetu. Kwa kuwa haya majitu ni maharamia yanayowamaliza watanzania na kulipaka matope jeshi la polisi, kwa umoja wetu tuyaangamize yote hapo hapo, yenyewe binafsi, na kila kitu yalichokuja nacho, iwe ni gari au kitu chochote yanayotumia kwenye ubaramia wao. Hapa ndipo pa kuonesha ile hasira inayoitwa, "Wananchi wenye hasira kali" Tukifanya hivyo tutakuwa tumelisaidia jeshi la polisi, tumeokoa maisha ya mwenzetu, tumelinda maisha ya wengine ambao walikuwa njiani kutekwa, na pia tutakuwa tumeisaidia Serikali, maana hatimaye tutajua hayo maharamia yanatoka wapi, yanatumwa na nani, na yanafanya hayo kwa lengo gani.

NB: Viongozi wa dini kwa kuwa mnakutana na wananchi wengi kwa pamoja na kwa kila wiki, ni muda sahihi sasa wa kuwapa waumini wenu tahadhari ya hii hatari ya utekaji, na kuwaongoza waumini wenu namna ya kusaidiana pale inapotokea mwenzao anaonekana yupo hatarini kutekwa.

HATUA YA AWALI:
Kila mwananchi atembee na filimbi. Ukiwa kwenye hatari ya kutekwa au ukaona mwenzako anafanyiwa vitendo vinavyoashiria ni utekaji, puliza filimbi mara moja, na wote tuliosikia filimbi, twende kwenye tukio kumwokoa mwenzetu na kila aina ya silaha itakayosaidia kumwokoa mwenzetu..

Huu ni wakati wa kujitetea na kushiriki katika ulinzi wetu binafsi kuliko kuwaachia polisi pekee yao.
Umeeleza vizuri sana ! 🙌🙏
 
Dawa nyingine ni kujizindika kishirikina (Wacha Mungu mnisamehe). Yaani kwamba aliyekuja kukufanyia baya anaparalaizi anashindwa kufanya kilichomleta, au wanateka kiumbe kingine ambacho siyo wewe, au wanakuteka na kukutesa ila kila aliyeshiriki anakufa kwa mateso makali sana baada ya hapo. Mnafikiri Kurjuan haipo?
Juju lipo Mzee !
Ni Ubaya Ubwela kwa kwenda mbele !
 
Arusha huko sijui tengeru, kuna watu wameshamvuliwa...na raia
Walidhani ni watekaji watoto
Wamechezea mapanga,kipondo
Walipaki gari raia walikuwa hawawaelewi....kumbe ni watu familia walikuwa na mambo yao tu...
Juzi tu nimetoka kumcmnt humu kuwa sahv raia wataanza kujjlinda wajuavyo wao na lazima action watakazo chukua zitakuwa na mabalaa tu
Tutazidi kuona na kusikia visa

Ova
 
Arusha huko sijui tengeru, kuna watu wameshamvuliwa...na raia
Walidhani ni watekaji watoto
Wamechezea mapanga,kipondo
Walipaki gari raia walikuwa hawawaelewi....kumbe ni watu familia walikuwa na mambo yao tu...
Juzi tu nimetoka kumcmnt humu kuwa sahv raia wataanza kujjlinda wajuavyo wao na lazima action watakazo chukua zitakuwa na mabalaa tu
Tutazidi kuona na kusikia visa

Ova
Hatari sana !
Mambo yakifikia out of control itabidi walioyaanzisha wajitokeze hadharani na kutubu !!
Mabalaa katika Nchi yanaanzaga hivi hivi kama utani !

Tuombe Mungu tusifike huko 🙏🙏
 
Muhimu sana kujilinda wakati huu, usikae kizembe.

Usipokee hovyo hovyo namba usizo zijua.

Ukiona jumbe zisizo eleweka wataarifu ndugu na jamaa wa karibu.

Usiwaamini sana watu wa pembeni wengine ndio wachoma ramani yako.

Nawakumbusha tena usikubali kamwe mpumbavu mmoja ama wawili kukuteka kwenye karandiga yao kama mzoga pambana uwezavyo.

Wao si ndio wahuni basi nasi twende nao kihuni hivyo hivyo.
 
Hatari sana !
Mambo yakifikia out of control itabidi walioyaanzisha wajitokeze hadharani na kutubu !!
Mabalaa katika Nchi yanaanzaga hivi hivi kama utani !

Tuombe Mungu tusifike huko 🙏🙏
Sahvi ni kukaa kwa tahadhari
Ukienda sehemu huna mgeni kaa
Mguu sawa maana lolote linaweza tokea
Ukienda sehemu kwa wale wenye magari wanapaki tu bila kueleweka nao wakae mguu sawa
Lolote linaweza tokea,
Nlikuwa nawasikiliza hawa jamaa waliyokuwa arusha wanasema sjui walipaki gari,mara wakawaona watoto wakawa wanawaita wanawapa pipi balaa ndiyo likaanzia hapo,

Ova
 
Wakuu kwema,

Watu wasiyojulikana siyo maneno mageni kwetu, na mambo haya yameanza kitambo kuanzia enzi za Kikwete na Ulimboka (kusoma tukio hilo zaidi hasa kwa Gen Z soma hapa - Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sanaaliyetekwa na watu wasiyojulikana na kukukwa ametupwa kwenye msitu akiwa ameteswa sana na kung'olewa meno.


Kadri awamu zilivyobadilika na ndivyo matukio haya yamezidi kuongezeka, na sasa wamekuja na mbinu mpya.

Wanakuja watu wanaojitambulisha kama polisi na kutaka kukukamata, lakini wanakuwa wamevalia kiraia yaani hawana gwanda za polisi, watakuonesha kitambulisho (lakini hivi hata vya mchongo vinapatikana), wakiwa pia na gari binafsi, nyingi ambazo zimekuwa zikihusika ni Noa nyeupe au nyeusi, au zile Cruza, lakini pia jamaa huibuka wenyewe wenyewe tu bila kiongozi wa husika.

Kuelewa zaidi haki yako pale polisi anapokuja kukukamata soma: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

Mfano wanakuja mtaani kwako lakini mjumbe wa eneo husika hana taarifa, au anafika sokoni lakini hawaambatani na uongozi wa soko.

Polisi wakishutumiwa kuhusika na matukio haya wanakana, kwamba waliofanya matukio hayo siyo polisi, wanauliza uongozi wa eneo hilo ulikuwepo? Walikuwa na uniform? Walitoa vitambulisho? Walikuja na gari ya polisi?

Ukiangalia ni kweli sababu hawaendi na utambulisho wowote kuwa wale ni polisi, ni tobo (loophole) tunalotakiwa kuliziba, huku polisi wakitoa matamko polisi akija kwa namna hiyo (bila utambulisho official) basi mtuhumiwa anatakiwa kukataa kukamatwa!

Pia soma: Sativa225 (Edgar Mwakabela) kijana maarufu kwa kukosoa serikali X apatikana, baada ya kutekwa na watu wasiojulikana

Hapa kwenye kukataa kukamatwa ndio kunaleta ka ugumu, maana tuambiane ukweli kuwadindishia wajeda labda na wewe mwenyewe uwe na msuli, vinginevyo unapigwa makofi mawili, unashikwa kwenye pindo ya suruali huyo ndio umeenda hivyo.

TUFANYAJE SASA KUKABILIANA NA HAWA JAMAA WANAOITWA WATU WASIYOJULIKANA?

Bila wananchi kushirikiana hatuwezi kushinda hili, inabidi tuwe na umoja kama tunavyoshadadia mambo ya kijinga.

Kwenye maandamano yanayoendelea Kenya ili mwandamaji aepuke kukamatwa ovyo walikuwa wanatembea na firimbi, akiona ameshindwa anaichomoa fastaa anaipuliza wenzake wanajaa kuhoji kuna nini, tuitumie njia njia hii.

~ Ukiona watu wanaojitambulisha kama polisi hawajavaa uniform zao, wana gari private na wakati mwingine hakuna plate number, na wala hawajaambatana na uongozi wa mtaa/eneo husika wanang'ang'ana kukuchukua usiende kizembe, puliza firimbi yako, puliza kwa nguvu zako zote kushutua watu wajae.

- Huna filimbi siyo kesi, piga kelele, yaani PIGA KELELE kwa nguvu zako zote mpaka watu wajae, hapa na wewe usiwe mzembe, sema hawa wanadai ni polisi lakini hawana uthibitisho kuwa wao ni polisi.

- Tutumie simu zetu vizuri, wakati jamaa aliyeshikwa anapayuka na kelele zake, wengine rekodini kila kitu, tupate sura zao, pamoja na usafiri waliokuja nao. Namba halisi ya gari huwa inaandikwa kwenye kioo cha gari pale mbele upande wa dereva kama sijakosea, maana kuna uwezekano mkubwa plate iliyotumika ni fake chukueni video na ya namba hizo. Wengine mko vizuri kwenye utaalamu wa mitandao ya kijamii, badala ya kurekodi kwenye simu yako ingia kwenye mtandao wowote wa kijamii na urushe tukio hilo live, amini nakwambia ni dk 0 tu litakuwa limeshasambaa nchi nzima na hao jamaa hawatochomoka.

- Wakati hayo yanaendelea wahojini watu hao ni kina nani na wanatoka wapi, kwa kiasi kikubwa ili kuua soo wataingia kwenye gari na kusepa ili wasitambulike zaidi, ikiwa watatoa silaha, ni muhimu kujilinda, wakifanikiwa kuondoka na jamaa walau tutakuwa na utambulisho wao wote kuanzia sura mpaka namba kamili za usajili.

Kufanya hivi itakuwa rahisi kuwatambua watu hawa wanaotekeleza matukio hayo, na tukiwabaini ni polisi, Jeshi la Polisi litatueleza vizuri kwanini wanashiriki kwenye mauaji ya raia.

Kama nilichokiweka kina manufaa sambaza ujumbe kwa ndugu na jamaa tushirikiane kukomesha watu hawa wasiyojulikana.
Maelezo na ushauri mzuri sana!!

Kule Dodoma wameanza kutupiga na kutuchomea kwenye nyumba
 
Sahvi ni kukaa kwa tahadhari
Ukienda sehemu huna mgeni kaa
Mguu sawa maana lolote linaweza tokea
Ukienda sehemu kwa wale wenye magari wanapaki tu bila kueleweka nao wakae mguu sawa
Lolote linaweza tokea,
Nlikuwa nawasikiliza hawa jamaa waliyokuwa arusha wanasema sjui walipaki gari,mara wakawaona watoto wakawa wanawaita wanawapa pipi balaa ndiyo likaanzia hapo,

Ova
Hatari sana !
 
Tangu utawala wa Magufuli watanzania wengi wamekuwa wakilalamika kutekwa kupotezwa na miili kuokotwa fukweni au porini kama ilivyotokea kwa Sativa na Dr. Ulimboka. Nimeamua kuwapa ushauri tu, kama hutaufuata basi tambua kuwa wakishakuteka hautarudi tena. Watakutupa kama mzoga wa mbwa.

Zingatia yafuatayo
1. Usimuamini askari yoyote. Ukiitwa kituoni kama sababu inaonekana ni kukusaidia chochote basi usiende hasa unapoitwa kwa kupigiwa simu.

2. Hakikisha number mpya usipokee hovyo hasa ikiwezekana block number zote ambazo hujazisevu kwenye simu yako. Hii itakusaidia maana hawatakupata kirahisi.

3. Wito wowote wa ghafla na rafiki yako bila mpangilio usiukubali.

4. Jilinde - Unajua kuwa police wanakutafuta basi jitahidi kujilinda.

Wanao tafutwa sana ni CHADEMA NA WAFUASI WAO na tambua kuwa CCM waliapa kuimaliza CHADEMA na polisi ni waajiriwa wa CCM na wao ni wanaccm kwahiyo ni juu yenu kudadavua.

JILINDENI MSIFE KIBOYA.

Pia soma=> Kupambana na watu wasiyojulikana: Ukija kukamatwa na polisi bila uniform na hajaambatana na kiongozi wa eneo husika piga firimbi, kusanya nzi
 
Tangu utawala wa Magufuli watanzania wengi wamekuwa wakilalamika kutekwa kupotezwa na miili kuokotwa fukweni au porini kama ilivyotokea kwa Sativa na Dr. Ulimboka. Nimeamua kuwapa ushauri tu, kama hutaufuata basi tambua kuwa wakishakuteka hautarudi tena. Watakutupa kama mzoga wa mbwa.

Zingatia yafuatayo
1. Usimuamini askari yoyote. Ukiitwa kituoni kama sababu inaonekana ni kukusaidia chochote basi usiende hasa unapoitwa kwa kupigiwa simu.
2. Hakikisha number mpya usipokee hovyo hasa ikiwezekana block number zote ambazo hujazisevu kwenye simu yako. Hii itakusaidia maana hawatakupata kirahisi.
3. Wito wowote wa ghafla na rafiki yako bila mpangilio usiukubali
4. Jilinde - Unajua kuwa police wanakutafuta basi jitahidi kujilinda

Wanao tafutwa sana ni CHADEMA NA WAFUASI WAO na tambua kuwa CCM waliapa kuimaliza CHADEMA na polisi ni waajiriwa wa ccm na wao ni wanaccm kwahiyo ni juu yenu kudadavua.

JILINDENI MSIFE KIBOYA
dah!
kumbe siku zote mlikua hamjilindi?
miljisahau au Imani ilikua kwa Mungu,

lakini sasa mnaamini ushirikina tu na kudanganyana namna za kijadi kujilinda, right? that is very wrong...

umaskini wa fikra na imani potofu ni utumwa mzito sana wa kifukara..

sikilizeni niwasanue, kwanza Muamini Mungu,

lakini pia,
vyombo vya ulinzi na usalama, muhalifu uwe na mawasiliano ama hauna, umejilinda ama vinginevyo. ukiwa muhalifu utatafutwa popote ulipo, utatiwa nguvuni na kisu au silaha za kijadi ulizonazo, na utawajibika kwa uhalifu wako mujibu wa sheria bila mbambamba yoyote, msidanganyane 🐒

Malaika Mkuu Gabriel atuondolee unyonge na hofu zisizo na maana yoyote na atulinde na adui muovu sote, sasa na hata milele .
Amina
 
dah!
kumbe siku zote mlikua hamjilindi?
miljisahau au Imani ilikua kwa Mungu,

lakini sasa mnaamini ushirikina tu na kudanganyana namna za kijadi kujilinda, right? that is very wrong...

umaskini wa fikra na imani potofu ni utumwa mzito sana wa kifukara..

sikilizeni niwasanue, kwanza Muamini Mungu,

lakini pia,
vyombo vya ulinzi na usalama, muhalifu uwe na mawasiliano ama hauna, umejilinda ama vinginevyo. ukiwa muhalifu utatafutwa popote ulipo, utatiwa nguvuni na kisu au silaha za kijadi ulizonazo, na utawajibika kwa uhalifu wako mujibu wa sheria bila mbambamba yoyote, msidanganyane [emoji205]

Malaika Mkuu Gabriel atuondolee unyonge na hofu zisizo na maana yoyote na atulinde na adui muovu sote, sasa na hata milele .
Amina
Daaaah! Unajidanganya kuwa wewe huu ushauri haukuhusu eeeeeeh?
Unaifahamu ile hadithi ya "MTEGO WA PANYA"?
 
dah!
kumbe siku zote mlikua hamjilindi?
miljisahau au Imani ilikua kwa Mungu,

lakini sasa mnaamini ushirikina tu na kudanganyana namna za kijadi kujilinda, right? that is very wrong...

umaskini wa fikra na imani potofu ni utumwa mzito sana wa kifukara..

sikilizeni niwasanue, kwanza Muamini Mungu,

lakini pia,
vyombo vya ulinzi na usalama, muhalifu uwe na mawasiliano ama hauna, umejilinda ama vinginevyo. ukiwa muhalifu utatafutwa popote ulipo, utatiwa nguvuni na kisu au silaha za kijadi ulizonazo, na utawajibika kwa uhalifu wako mujibu wa sheria bila mbambamba yoyote, msidanganyane 🐒

Malaika Mkuu Gabriel atuondolee unyonge na hofu zisizo na maana yoyote na atulinde na adui muovu sote, sasa na hata milele .
Amina
Hii hoja unaichukulia poa? Watu wanapotea ni lazima tuwasanue, watapunguza kuilinda ccm na uovu wao
 
Back
Top Bottom