Kupanda kwa thamani ya Tsh. dhidi ya Us. dola kunaashiria nini? (kutoka 1800---1584 within a month)

Kupanda kwa thamani ya Tsh. dhidi ya Us. dola kunaashiria nini? (kutoka 1800---1584 within a month)

ngwendu

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2010
Posts
1,964
Reaction score
175
Nakumbuka shilingi ya tanzania ilishuka nakufikia thamani ya 1800 kwa dola moja ya Us na sasa imepanda na imefikia 1584 leo. hii inaashiria nini? kipindi ikishuka thamani kila siku zilikuwa zinakuja threads mpya kuripoti hilo lakini mbona sasa wale maripota wetu hatuwaoni? tunawashauri pia wendelee kuripori kama walivyokuwa wakifanya hapo awali.
Na mwishi kabisa ambalo ndo lengo la thread hii, ni kuwa inaashiria nini? wataalamu wa uchumi hebu tusaidieni sisi wauza machungwa huku mtaani.
 
Nakumbuka shilingi ya tanzania ilishuka nakufikia thamani ya 1800 kwa dola moja ya Us na sasa imepanda na imefikia 1584 leo. hii inaashiria nini? kipindi ikishuka thamani kila siku zilikuwa zinakuja threads mpya kuripoti hilo lakini mbona sasa wale maripota wetu hatuwaoni? tunawashauri pia wendelee kuripori kama walivyokuwa wakifanya hapo awali.
Na mwishi kabisa ambali ndo lengo la thread hii, ni kuwa inaashiria nini? wataalamu wa uchumi hebu tusaidieni sisi wauza machungwa huku mtaani.

Mkuu Hiki ni kipindi cha mapunziko, biashara nyingi zinafunga hadi January, so no much use of foreign currency this month. kwa sababu hiyo lazima foreign currecies zitapungua thamani kwa sasa lakini haimaanishi Tsh imepanda thamani. Kuthibitisha hilo angalia bei ya vitu soko la ndani je na vyenyewe vimeshuka bei au la? hapo ndo utajua kama shilingi bado inaporomoka au inainuka.

Kitu kingine subiri ikifika januari 15 na kuendelea wakati biashara nyingi zinafunguliwa tena, utaona kama Dola itabaki hapo pa 15xx au la.

conclusion: Shilingi haijapanda thamani hata kidogo, with comparison na Local market, Dola haijashuka thamani ila kwa mwezi huu wa mapumziko watumiaji wa Dola hawapo.

Kama una Tsh zisizokuwa na kazi huu ni wakati wako mazuri wa kuwekeza kwenye Dola, Mwezi wa pili mwakani utakuwa na faida sana ukiziuza.
 
Ukienda madukani kununua vitu kama computer wenyewe huuza kwa dola,dola 1 ni sawa na Tsh 1640 kwa hiyo mambo baado yako palepale huo unafuu haupo
 
Kinachotokea ni kwamba Serikali kupitia BoT ime-release fresh dollars sokoni, kawaida BoT huwauzia bank na bank huwauzia individuals na makampuni, lakini kinachofanyika sasa BoT in awauzia individuals like Bureau de change kwa rate ya chini mno, mwisho wa siku bank nao wanalazimika kushusha rate (function of supply nad demand). Lakini hiki kinachofanyika si measurement nzuri ya ku-control exchange rate kwani mara nyingi haidumu, kwani BoT ina maximum foreign reserve haiwezi kuuza USD kila siku, at the same time kati ya wale wanouziwa kwa bei rahishi kuna wengine wanazifadhi wakisubiri BoT itakopoacha kurelease more USD wao wauze kwa bei ya juu. Serikali inatakiwa imaimarishe uuzaji nje bidhaa , yaani tuwe na more export than import, hii ni njia nzuri ya ku-control exchange rate.
 
Mkuu Hiki ni kipindi cha mapunziko, biashara nyingi zinafunga hadi January, so no much use of foreign currency this month. kwa sababu hiyo lazima foreign currecies zitapungua thamani kwa sasa lakini haimaanishi Tsh imepanda thamani. Kuthibitisha hilo angalia bei ya vitu soko la ndani je na vyenyewe vimeshuka bei au la? hapo ndo utajua kama shilingi bado inaporomoka au inainuka.

Kitu kingine subiri ikifika januari 15 na kuendelea wakati biashara nyingi zinafunguliwa tena, utaona kama Dola itabaki hapo pa 15xx au la.

conclusion: Shilingi haijapanda thamani hata kidogo, with comparison na Local market, Dola haijashuka thamani ila kwa mwezi huu wa mapumziko watumiaji wa Dola hawapo.

Kama una Tsh zisizokuwa na kazi huu ni wakati wako mazuri wa kuwekeza kwenye Dola, Mwezi wa pili mwakani utakuwa na faida sana ukiziuza.
Thanks, ila nasubiri hiyo tarehe 15 january uliyosema. ila kitu kingine ambacho ungenisaidia, mbona watu hawarepoti kama kipindi sh ikishuka? au sisi tunaombeana mabaya tu? mbona naona kama jambo la aibu kwetu waTZ? au mnaonaje?
 
Wanasema ukiona mgonjwa mahututi kapata nafuu kaa chonjo...! tafakari
 
Kimsingi kupanda thamani dhidi ya $ kuna mambo mengi yanaweza yakajitokeza. Hiyo ni njia mojawapo ya kupunguza mfumuko wa bei(Inflation). Je mfumuko wa bei umepungua kutoka kipindi hicho unachozungumzia cha miezi mitatu?. Kama bado basi njia waliotumia kupunguza mfumuko wa bei sio mbadala na mathara yake yataendelea kuzoofisha uchumi wa nchi zaidi ya hapo mwanzo. Kwa kipindi kirefu (in a long run) kijacho Uwezekano ni mkubwa wawekezaji wa ndani wakashindwa kuendesha shughuli zao-hii ni kutokana na gharama za uzalishaji kuongezeka -Riba( Interest rate ) kuwa juu. Pia kushuka kwa mauzo ya bidhaa nje ya nchi (decrease in exports).Pia ukumbuke na ufunguke macho kuwa Tsh haijapanda thamani kutokana na uzalishaji ama exports .Mfano Ksh imepanda thamani dhidi ya $ kutokana na kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa zao nje ya nchi hususani mazao ya kilimo.Kwa hiyo nchini Kenya hali ya uchumi inazidi kuimarika tofauti na nchini Tanzania ambako kuna ongezeko la thamani ya Tsh dhidi ya $ lakini uchumi unazidi kuzorota.
 
Nakumbuka shilingi ya tanzania ilishuka nakufikia thamani ya 1800 kwa dola moja ya Us na sasa imepanda na imefikia 1584 leo. hii inaashiria nini? kipindi ikishuka thamani kila siku zilikuwa zinakuja threads mpya kuripoti hilo lakini mbona sasa wale maripota wetu hatuwaoni? tunawashauri pia wendelee kuripori kama walivyokuwa wakifanya hapo awali.
Na mwishi kabisa ambalo ndo lengo la thread hii, ni kuwa inaashiria nini? wataalamu wa uchumi hebu tusaidieni sisi wauza machungwa huku mtaani.

Si kweli kuwa shilingi inapanda. Ukweli ni kwamba Dolla inashuka thamani
 
Dah mkuu uko fiti hata kama sikuoni lakini maneno uliyoyaandika mtu anaweza akaakonvisika,thanks you open my mind
:eyebrows::eyebrows::A S embarassed::shock:
 
Kinachotokea ni kwamba Serikali kupitia BoT ime-release fresh dollars sokoni, kawaida BoT huwauzia bank na bank huwauzia individuals na makampuni, lakini kinachofanyika sasa BoT in awauzia individuals like Bureau de change kwa rate ya chini mno, mwisho wa siku bank nao wanalazimika kushusha rate (function of supply nad demand). Lakini hiki kinachofanyika si measurement nzuri ya ku-control exchange rate kwani mara nyingi haidumu, kwani BoT ina maximum foreign reserve haiwezi kuuza USD kila siku, at the same time kati ya wale wanouziwa kwa bei rahishi kuna wengine wanazifadhi wakisubiri BoT itakopoacha kurelease more USD wao wauze kwa bei ya juu. Serikali inatakiwa imaimarishe uuzaji nje bidhaa , yaani tuwe na more export than import, hii ni njia nzuri ya ku-control exchange rate.
Noted with thanx.
 
Si kweli kuwa shilingi inapanda. Ukweli ni kwamba Dolla inashuka thamani
mkuu lakini umeangalia thamani ya dola juu ya currency nyingine kwa miezi miwili iliyopita kama vile Euro na Pound? Better ungekuwa na data. internet siunayo hebu bofya ndo utoe data zako hizo.
 
Kinachotokea ni kwamba Serikali kupitia BoT ime-release fresh dollars sokoni, kawaida BoT huwauzia bank na bank huwauzia individuals na makampuni, lakini kinachofanyika sasa BoT in awauzia individuals like Bureau de change kwa rate ya chini mno, mwisho wa siku bank nao wanalazimika kushusha rate (function of supply nad demand). Lakini hiki kinachofanyika si measurement nzuri ya ku-control exchange rate kwani mara nyingi haidumu, kwani BoT ina maximum foreign reserve haiwezi kuuza USD kila siku, at the same time kati ya wale wanouziwa kwa bei rahishi kuna wengine wanazifadhi wakisubiri BoT itakopoacha kurelease more USD wao wauze kwa bei ya juu. Serikali inatakiwa imaimarishe uuzaji nje bidhaa , yaani tuwe na more export than import, hii ni njia nzuri ya ku-control exchange rate.

Ebi bishuba omu kipindi eki ila Endeleea yagamba amazima umu kipindi eki!
 
Mkuu Hiki ni kipindi cha mapunziko, biashara nyingi zinafunga hadi January, so no much use of foreign currency this month. kwa sababu hiyo lazima foreign currecies zitapungua thamani kwa sasa lakini haimaanishi Tsh imepanda thamani. Kuthibitisha hilo angalia bei ya vitu soko la ndani je na vyenyewe vimeshuka bei au la? hapo ndo utajua kama shilingi bado inaporomoka au inainuka.

Kitu kingine subiri ikifika januari 15 na kuendelea wakati biashara nyingi zinafunguliwa tena, utaona kama Dola itabaki hapo pa 15xx au la.

conclusion: Shilingi haijapanda thamani hata kidogo, with comparison na Local market, Dola haijashuka thamani ila kwa mwezi huu wa mapumziko watumiaji wa Dola hawapo.

Kama una Tsh zisizokuwa na kazi huu ni wakati wako mazuri wa kuwekeza kwenye Dola, Mwezi wa pili mwakani utakuwa na faida sana ukiziuza.

Aga mazima omukipindi eki! ninkusima muno!
 
Gwendu hakuna mwenye wajibu wa kumpasha mwenzie habari. Hii thread uloleta wewe inatosha pia.

kuhusu tshs yetu kama haikuwa na nguvu kipindi cha msimu wa mazao (pamba,korosho,kahawa n.k hiki unachokiona sasa ni sanaa zo benki kuu tu, tujipe muda.
 
Katika wote walotoa maelezo hapo Dero ndo yuko right.Nadhani kitaaluma Dero utakuwa mchumi.Sababu zilizotolewa za watu kwenda Xmass hazina mashiko.Tuache siasa kwenye mambo tusoyajua.Naomba kuwakilisha!!
 
Back
Top Bottom