Kupanga kulivyonikutanisha na huyu mdada

Kupanga kulivyonikutanisha na huyu mdada

Kaluluma

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2019
Posts
468
Reaction score
619
Wasalaam wakuu,

Leo naomba nishee kisa changu kipindi nikiwa chuo,nilipoingia chuo mwaka wa kwanza nilienda kukaa hostel sasa maisha ya hostel sikuyafurahia,nilikaa semester moja pekee,wakati wa likizo nikawahi kwenda chuo ili nisisumbuke kupata chumba cha kupanga,niliamua kutafuta chumba mwenyewe bila dalali, sasa wakati nazunguka nikakutana na mdada mmoja mwanachuo aliyekuwa anasoma chuo jirani na chuo nilichokuwepo, alikuwa ni pisi flani hivi nzuri,nikawa nimevutiwa nae, kwa hyo nikaomba mawasiliano nikaendelea na mishe zangu, baadae nikamtafuta tukawa na kaukaribu flani ka kirafiki baadae nikatupia swaga mambo yakatiki,sasa kimbembe demu akawa hataki kuja ghetto, ukimuita visingizio kibao, nikaona isiwe tabu, nikapiga kimya.

HUKU NILIKOPANGA SASA
Alihamia dada mmoja anafanya kazi bucha la nyama,kama kawaida mzee nikatest uwezo mambo yakanyooka,ikawa ni mwendo wa kubadili vyumba tu,leo kwake kesho kwangu,baada ya kama miezi miwili yule mdada wa chuo akanitafuta kwenye simu anauliza kwanini simjuliihali kama zamani,nikamwambia tu masomo yamebana.

Siku moja nimekutana nae maeneo ya chuo chao akanirukia akanikumbatia,halafu kawatambulisha marafiki zake eti mi ndo shemela wao.

Akanivuta kando akanambia anataka akapaone getto kwangu,weeeh,nikawaza demu wa buchani akimkuta je? Wakati ananiamini kinyama.nikampiga fix tu kwamba nitampigia jioni ili twende akapaone.

Jioni nikapiga kimya kanitafuta,nikamwambia nimebanwa kidogo. Ikapita kama wiki,wikiendi moja nipo gengeni nanunua mazaga,akanifuma,kaniganda kwamba hata iweje lazima twende nae home, nikaona sio kesi ngoja niende nae tumefika home, nikawa naandaa msosi,mara nasikia "kaluluma hizi nguo za nani?"maana aliona nguo za kike mle ghetto,nikamwambia tu ni za mchumba wangu.

Akasema "kumbe ndo maana ulikuwa hutaki nije huku? "mi nikamwambia " sasa kama ulikuwa hutaki kuja huku ulitegemea mi ningefanyaje?" akanambia sawa ila ujue mi bado nakupenda nikamjibu "mi mwenyewe nakupenda kama rafiki" akajichekeshachekesha pale,msosi ulipoiva wakati tunakula mara kanilisha,mwisho wake tumejikuta tunadendeka,wakati bado mambo hayajafika mbali simu yangu ikaita,kucheki ni yule demu wa buchani anasema yuko njiani anakuja kula,weeeh nilijichomoa kutoka mikononi mwa yule demu nikamwambia ajiweke fresh maana mchumba wangu anakuja.

Baada ya muda akafika yule dem mwingine nikamtambulisha kwa huyu mdada wa chuo kama girlfriend halafu yule mwingine nikamwambia ni rafiki yangu japo alionesha mashaka kidogo tukaungana kwenye msosi baadae nikamsindikiza akaondoka,jioni yake huyu girlfriend wangu alinihoji sana akawa anasema ana mashaka kama huyo alikuwa ni rafiki yangu,nikaongea naye tukayamaliza.

Sasa ikawa nikikutana nae analalamika kwanini sikumvumilia wakati alikuwa ananipima,mi nikamwambia labda haikupangwa niwe na yeye,bora tuendelee kuwa marafiki tu,nashukuru alinielewa na kwa upendo wa huyu dada wa bucha mpaka nikawa siendi likizo yaani ikifika likizo mimi ni wa kubaki maghetoni tu mpaka bi mkubwa akawa ananiuliza mbona umetususa baba,namwambia tu kuna vitu naweka sawa na mpaka sasa ninavyoandika huyo dada wa bucha ni official Mrs. Kaluluma
 
kwanza nikupe hongera Bwana kaluluma kwa kufanya kweli. Pili nikupongeze kwa kumpa funzo huyo bidada wa chuo na nyodo zake., unajua wananwake wengine wanajua tunawatafuta kwa mtafuno tu. Kumbe ndiko maisha yanakoanzia. Mama Mrs Kaluluma hajambo lakini.
 
Kkwamza nikupe hongera Bwan kaluluma kwa kufanya kweli. Pili nikupongeze kwa kumpa funzo huo bidada wa chuo na nyodo zake., unajua wananwake wengine wanajua tunawatafuta kwa mtafuno tu. Kumbe ndiko maisha yanakoanzia. Mama Mrs Kaluluma hajambo lakini.
yupo ni mzima wa afya kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom