DOKEZO Kupata huduma kwenye Ofisi za Uhamiaji kunahusiana nini na mavazi mtu aliyovaa?

DOKEZO Kupata huduma kwenye Ofisi za Uhamiaji kunahusiana nini na mavazi mtu aliyovaa?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Don Gorgon

Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
35
Reaction score
68
Mara nyingi nimeona akina dada wakikataliwa kuhudumiwa katika ofisi za uhamiaji kwakuwa aidha wamevaa nguo zinazoelezwa maafisa kuwa ni fupi au za kubana. Nani anaweka vigezo hivi? Mbona neno uchi tumelikuza hadi kufikia maeneo ambayo hayapaswi kuwa uchi? Kwahiyo Maafisaa wakiona miguu ya akina dada wanashindwa kufanya kazi au ufanisi unapungua?

Huwa likija suala la mavazi Watanzania wengi tunakimbilia kuongelea maadili kana kwamba sisi sote tuna maadili.

Siku moja nimefika ofisi fulani ya Uhamiaji nikakuta walinzi getini wanawarudisha akina dada wawili waliovyaa suruali, tena ambazo hata hazina mbano wa namna ya kuleta “mfadhaiko” kwa afisa wa kiume, kama hiyo ndiyo hoja. Hivi huwa wanawarudisha hata wageni wenye rangi tofauti na nyeusi wanapoenda kushughulikia permits zao au nyaraka nyingine?

Well, huenda nimekengeuka kimaadili kutokuona na kutokuona shida ya mavazi hayo.
 
Nenda siku HOSPITAL LUGALO uone ukivaaJEZI au TRACKSUIT unapelekwa uwanjani ukacheze mpila na kufanya mazoezi ya VIUNGO na wanajeshi.
HESHIMU maadili yako ya KITANZANIA acha kuigaiga UZUNGU.
 
Ni ushamba tu huo ila unaondoka muda unavyozidi kwenda, kwa watu wanaofanya kazi kwenye ofisi zinazojielewa hakuna hizo restrictions za kipumbavu hata kwa staff, mavazi na performance ni vitu ambavyo havitangamani hasa kwa dunia ya leo
 
Nenda siku HOSPITAL LUGALO uone ukivaaJEZI au TRACKSUIT unapelekwa uwanjani ukacheze mpila na kifanya mazoezi ya VIUNGO
HESHIMU maadili yako ya KITANZANIA acha kuigaiga UZUNGU
Ngoja tuige waarabu najua nitakubalika ...nikienda na kanzu na barakashea mambo swafiii
 
Upuuzi tupu,
Sijui kwann,
Et ukivaa jersey hauingii ofisini kwao 😂😂😂 jamaa wanajiona kina nani sijui,
Nenda na jezi ya Arsenal, ukirudishwa njoo unipe feedback
 
Ulimbukeni tu. Ipo nguo ambayo unaweza sema imekiuka maadili, lakini mfano wa Jeans kwa mwanamke imekiuka maadili gani? Au 3 quarter pants kwa mwanaume ina athari gani kimaadili?
 
Mama Samia atoe amri kabisa ofisi zote watu wanaoenda na wafanyakazi wavae stara kama ndugu zetu waislamu.
 
Nenda siku HOSPITAL LUGALO uone ukivaaJEZI au TRACKSUIT unapelekwa uwanjani ukacheze mpila na kifanya mazoezi ya VIUNGO
HESHIMU maadili yako ya KITANZANIA acha kuigaiga UZUNGU
Tukirudi kwenye Uafrika patakalika? Lakini je, tukiachana na "uzungu" tuna nini cha kwetu? Tukiwaachia nguo na kila tunachovaa leo si ndiyo matiti na korodani zitakuwa upenuni mapema asubuhi? Wacha hoja zi kihisia.

Kwahiyo, hivyo vitendo vya wana-Lugalo navyo unaona ni jambo la kujivunia kama taifa? 😀
 
Back
Top Bottom