Kupata matibabu bila PF 3 baada kujeruhiwa na kutaka kufungua mashtaka Polisi

Rato

Member
Joined
Jul 10, 2012
Posts
92
Reaction score
7
Nilivamiwa na kibaka akanijeruhiwa na kuninyang'anya simu.Baada ya hapo nilikwenda hospital bila PF 3 na kupata matibabu na kurudi nyumbani bila kwenda Polisi.Wakati kidonda kinaanza kupona nikakutana na mtuhumiwa wangu.Baada ya kumzidi nguvu nikamfikisha kituo cha Polisi lkn wamekataa kumpokea kwa madai kwamba sikuwa na PF 3 na pia wataamini vipi kwamba yeye ndi
ye aliyenivamia? Msaada wa kisheria nifanyeje?
 
Hapo huna chako,na ukienda vibaya unaweza kujikuta ktk matatizo,kwanini hukwenda polisi na kupata rb? Kwani ndio utaratibu wa kisheria.Mi nakushauri kama uliamua kuzembea kwenda polisi achana nalo tu.
 
Hili swala limekaa kikiritimba mno, linatakiwa lifutwe, kwanza uhai matibabau, mengine baadae, maana lazima taarifa zako zitachukuliwa tu, hasa kwenye madhara kama ya risasi, mapanga, ajali n.k.
Bado tunaishi kama tuko miaka ya sabini, kwani vigogo au wenye vyeo huwa wanaulizwa pia PF3?
Kazi tunayo...Tuko nyuma mno, watu wanapoteza maisha bila ya sababu kwa kusubiria PF3 au kwenda polisi kwanza..
Ila wakubwa watatusikia?!
 
Nilishaibiwa ila sikwenda police. Nikakutana na aliyeniibia. Nilimfanya mbaya akarudisha nusu ya alivyoiba na yeye ndio akaenda polisi kunishtaki kwa kumpa kichapo kitakatifu. Sikutaka kupoteza muda wangu bure.
 
Hapo mkuu ulienda tofauti na hakuna ushahidi wowote. Huyo jamaa ungemkaba tu atoe chako hukohuko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…