Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 31,009
- 60,629
Kwenye maisha kuna kupata na kukosa pale tunapotaka, tunapohitaji, au tunapoomba kitu. Muhimu ni kukubaliana na hali halisi.
Linapokuja swala la mahusiano ni jambo la kawaida kijana/mwanaume kumtaka, kumpenda ama kumtamani msichana/mwanamke. Na nikawaida msichana kukubali ama kukataa ombi la mwanaume, kumpenda ama kutompenda.
Binafsi hua nashangazwa sana na wale wasiokua waelewa. Kwamba yeye mdada akimkatalia ombi lake basi anajenga chuki kabisa, wengine hufikia hata kutoa matusi na kashfa za kila aina kisa kaambiwa "HAPANA/HAIWEZEKANI". Wanashindwa kuelewa kwamba kama kila anaeomba angekua anapewa "NDIO" kisa tu kasema anampenda/mhitaji mdada basi wadada wengi wangekua na msururu wa wapenzi wanaowakubalia kwa huruma. Kwamba wanavyolazimisha wao wakubaliwe kwasababu wamependa ndivyo wanavyoweza wakafanya wengine watakaovutiwa na msichana yule yule, je atakubali mwenzake nae akubaliwe ili asiumie?
Mtu akikwambia "hapana haiwezekani" jitahidi kuheshimu maamuzi/matakwa yake. Usijenge chuki wala usianzishe ugomvi. Na ikibidi jaribu wewe kujiweka kwenye viatu vyake na ufikirie "je kama ningekua mimi ningemkubalia kila aliyenitaka/nipenda/nihitaji hata kama hanivutii ama nina mtu wangu mwingine?" Usiwe mbinafsi, kama ambavyo wewe unachagua wa kuwafuata kwa kutumia vigezo vyako binafsi ndivyo ambavyo na wao wana haki ya kuchagua wa kumkubalia kwa vigezo walivyojiwekea wenyewe.
Linapokuja swala la mahusiano ni jambo la kawaida kijana/mwanaume kumtaka, kumpenda ama kumtamani msichana/mwanamke. Na nikawaida msichana kukubali ama kukataa ombi la mwanaume, kumpenda ama kutompenda.
Binafsi hua nashangazwa sana na wale wasiokua waelewa. Kwamba yeye mdada akimkatalia ombi lake basi anajenga chuki kabisa, wengine hufikia hata kutoa matusi na kashfa za kila aina kisa kaambiwa "HAPANA/HAIWEZEKANI". Wanashindwa kuelewa kwamba kama kila anaeomba angekua anapewa "NDIO" kisa tu kasema anampenda/mhitaji mdada basi wadada wengi wangekua na msururu wa wapenzi wanaowakubalia kwa huruma. Kwamba wanavyolazimisha wao wakubaliwe kwasababu wamependa ndivyo wanavyoweza wakafanya wengine watakaovutiwa na msichana yule yule, je atakubali mwenzake nae akubaliwe ili asiumie?
Mtu akikwambia "hapana haiwezekani" jitahidi kuheshimu maamuzi/matakwa yake. Usijenge chuki wala usianzishe ugomvi. Na ikibidi jaribu wewe kujiweka kwenye viatu vyake na ufikirie "je kama ningekua mimi ningemkubalia kila aliyenitaka/nipenda/nihitaji hata kama hanivutii ama nina mtu wangu mwingine?" Usiwe mbinafsi, kama ambavyo wewe unachagua wa kuwafuata kwa kutumia vigezo vyako binafsi ndivyo ambavyo na wao wana haki ya kuchagua wa kumkubalia kwa vigezo walivyojiwekea wenyewe.