Kupiga & kugombeza watoto kwasababu ya uwezo shuleni ni ujinga

Kupiga & kugombeza watoto kwasababu ya uwezo shuleni ni ujinga

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
A. KUPIGA & KUGOMBEZA WATOTO KWASABABU YA UWEZO SHULENI NI UJINGA

1639223015532.png


Unakuta mtoto kila siku anaenda shuleni, anahudhuria kila kipindi, anafanya home work, n.k. ya nini kumchapa au kumgombeza huyu pale anaposhika namba za kawaida au chini darasani. nimesema namba kwasababu ndicho kigezo ambacho wazazi / walezi wengi hukiangalia, yani hata kama mtoto kafaulu vizuri mitihani lakini wao wanaangalia kashika mafasi ya ngapi.

Wengine huenda hatua za ziada kusomesha watoto wao shule za gharama huku wakiamini pengine ndio suluhisho kwa asilimia 100, matokeo yake mtoto akienda huko na kuwa na uwezo ambao bado shaujafikia mategemeo ya wazazi wake, wanamgombeza kwamba wamejibana sana ili asome huko, mtoto anapewa kipigo kwa makosa ambayo sio yake mithiri farasi aliepelekwa shule ya mamilioni ili awe na uwezo wa kuogelea kama wa samaki.

Ipo hivi wazazi wenzangu, hata sisi binadamu tunatofautiana uwezo,mtoto anaweza kuwa kajaliwa uwezo mkubwa shuleni kiasi kwamba hata akisoma shule hizi za kata zenye changamoto kubwa, unakuta anafaulu vizuri kabisa,

lakini kuna watoto wengine uwezo wao wamejaliwa zaidi sehemu nyingine , hivyo uwezo wa darasani unaweza kuwa mdogo , hawa kuwasaidia inabidi ufanya haya:

  • kuwasaidia wasome shule zenye walimu wa kutosha.
  • kuwalipia tuition, kama hela ipo mletee kabisa mwalimu nyumbani ili kama hajaelewa aelekezwe upya bila kuogopa wenzake.
  • 1639222738941.png
  • usiwapeleke boarding - huko boarding ni kazi sana kujua ana yopitia, pia tuition hakuna.
  • kuwapa moyo,
  • kufatilia mahudhurio yao, homework, n.k

hapo lengo liwe aweze kupata hata ufaulu wa kawaida wa kumfanya asonge mbele, kama ni form 4 basi apate walau division 3

B. KUPUUZA "PLAN B" NI UJINGA ULIOTUKUKA!!

Haijalishi mtoto ana uwezo kiasi gani huko shuleni, kwenye haya maisha haya ya sasa apa bongo huwezi kuweka mategemeo yako yote kwenye njia moja tu ya mafanikio, Nadhani sote ni mashahidi wa jinsi utitiri wa wasomi unavyozidi kujaa mitaani kadri miaka inavyoenda, kwa siku hizi kumaliza degree hapa nchini ni kama kumalza darasa la saba, degree zipo nyingi sana huku mitaani. (Mwenye uhakika wa elimu yake kumpa ajira ni mzanzibari tu, asilimia 21 za ajira za huku kwetu ni zao na pia huko kwao, ni wao tu wenye sifa za kuajiria na serikali yao)

ni wakati wa kusimama na miguu miwli, zile enzi za kusimama kwa mguu moja kusoma ili uajiriwe zilishapita, unahitaji "plan b" ili "plan a" ikifeli bado uwe umesimama na sio kulalamika tu umesoma sana

Kwa watoto wenye vipaji au uwezo flani tangu wadogo, hawa watoto ni mithiri ya chui mwenye mbio na uwezo mkubwa wa kuwinda lakini unapompima kwa kigezo cha uwezo wake wa elimu ya darasani mithiri ya uwezo wa kuogelea, hapo utakua umeufungia uwezo wake wa chui. Kama mtoto unaona wazi kabisa ana kipaji au uwezo flani wewe muendeleze huko, huenda ni kitu alichobarikiwa na ni baraka waliyopewa wachache kufanya vitu vigumu kwa wepesi, wengine inabidi wasomee, kufundishwa na kutia bidii sana lakinii yeye kazaliwa na hiyo baraka, kama anatimiza jukumu lako la yeye kusoma kadri ya uwezo wake basi na yeye apewe nafasi kuendeleza alichojaliwa endapo kina manufaa maana si kila kipaji kina manufaa. unakuta mtoto anapenda sana upishi, ufundi, ushonaji, mpira, kuhubiri / kusoma koran, n.k huyo jua tu ya kwamba hio baraka yake ni zawadi na si ya kupuuzwa, ni baraka inayoweza kuwa plan b.

Kwa watoto wengine, akimaliza form 4 nashauri umpeleke veta mwaka mzima kisha ndio aenelee na shule, huko veta nadhani kozi ni miezi miwili lakini hi huwa ni elimu ya darasani kwa kiasi kikubwa, miei inayobaki inabidi aingie kazini kupata ujuzi zaidi kujua changamoto, kuzoea mazingira, n.k. hapa itamsaidia sana hata akiwa likizo akianza shule au chuo basi atakuwa hashindi mitaani kusubiri likizo iishe, atakuwa bize kujitaftia ridhiki yake, na hii ni mpaka hata akihitimu chuo, yani hatakuwa amekaa tuu yupo yupo anasubiria kuitwa kwenye ajira, hapa atakuwa anafanya mambo yake na neema ikimjia anaweza kusahau kabisa hizo ajira .
 
Mzazi mmoja alifika ofisini kwangu, na kusema hivi: "Hili toto langu jinga sana, alielewi kitu shuleni!, Nimelileta hapa, ili ulifundishe lielewe." Baada ya kimya kirefu nikamwambia huyo mzazi. "Ujinga, hauna mwisho kwa mwanadamu, kila siku tunajifunza, ili kuufuta ujinga. Huyo mwanao, anakipaji ambacho kinachomzuia kufanya unayoyawaza wewe, kwa kuwa na yeye anayo usiyoyawaza." Hakuongeza neno lingine.
 
Mzazi mmoja alifika ofisini kwangu, na kusema hivi: "Hili toto langu jinga sana, alielewi kitu shuleni!, Nimelileta hapa, ili ulifundishe lielewe." Baada ya kimya kirefu nikamwambia huyo mzazi. "Ujinga, hauna mwisho kwa mwanadamu, kila siku tunajifunza, ili kuufuta ujinga. Huyo mwanao, anakipaji ambacho kinachomzuia kufanya unayoyawaza wewe, kwa kuwa na yeye anayo usiyoyawaza." Hakuongeza neno lingine.
Elimu inahitajika sana kwa wazazi kujua haya mambo, wazazi wengi wanajua uwezo pekee ni darasani na kwamba fimbo na kugombeza kunaongeza uwezo
 
Elimu inahitajika sana kwa wazazi kujua haya mambo, wazazi wengi wanajua uwezo pekee ni darasani na kwamba fimbo na kugombeza kunaongeza uwezo
Tatizo kubwa ni wazazi kuwatumia watoto wao kama ngao ya kuficha madhaifu yao, kijamii. Wanatambiana sana, juu uwezo wa watoto wao wa darasani. Na mtoto mazingira ya shule yasipo mwezesha vizuri kuyafikia matarajio ya mzazi wake, basi ataishia kusimangwa kila uchao, kwa kumlinganisha na watoto wengine wenye ufaulu wa juu sana, hata kama alama zao za darasani, wanazipata kwa kuibia.
 
Binafsi nilikua mtoro kuanzia la kwanza mpaka la tatu. Nikawa mwanafunzi mzuri kuanzia la nne. Kuanzia form two mpaka six nikawa mwanafunzi miyeyusho.

All the while nazungukia shule za kata.

Kutokana na hilo I am never harsh towards my kids regarding their intelligence mfano huyu wa miaka minne anaweza kuhesabu, kuandika na kusoma ila siyo kuandika neno lenye herufi nyingi au kusoma neno refu. Mama yao anakasirika anasema mtoto atakua mjinga so one day nikamuuliza "Ulivyokua na miaka minne ulikua unaweza kuandika?"
 
Utakuta wewe ni mzazi tena uliyelelewa na hapahapa ujiji

USSR
 
Mtoto ambae hafanyi kama wazazi wanavyotarajia huko shuleni mzazi ndo aoneshe njia kumuelewesha kwa upendo na upole namna gani afanye ili awe unavyotaka.

Kuna mdogo wangu alokuwa anafanya vizuri sana kuna mtihani walipofanya akawa kama mtu wa 7 hivi wakati yeye wa kwanza wa pili,bi mkubwa akawaka.

Mimi nikamuambia kawaida hiyo,hayo ndio maisha kuna wakati wenzio watakupita na kuna wakati utawapita.
 
31D25101-AE21-4B43-B89A-3AE25D3B9E0D.jpeg

Kwa style hii mtaumiza sana watoto! 😂😂😂😂
 
Tatizo kubwa ni wazazi kuwatumia watoto wao kama ngao ya kuficha madhaifu yao, kijamii. Wanatambiana sana, juu uwezo wa watoto wao wa darasani. Na mtoto mazingira ya shule yasipo mwezesha vizuri kuyafikia matarajio ya mzazi wake, basi ataishia kusimangwa kila uchao, kwa kumlinganisha na watoto wengine wenye ufaulu wa juu sana, hata kama alama zao za darasani, wanazipata kwa kuibia.

Umemaliza kila kitu mzee[emoji119]

Nenda Serena Hotel au Regency fanya utakavyo gharama juu yangu
 
Je, ni kweli kwamba maombi ya upako yanaweza kubadili ubongo wa mtoto? Ili kama alikuwa anakuwa wa mwisho basi awe wa kwanza?

Kuna shuhuda kwenye Huduma kwamba watoto wamebadilika kwa maombi.
Mtoto kama ni kilaza atabakia hivyo tu
 
A. KUPIGA & KUGOMBEZA WATOTO KWASABABU YA UWEZO SHULENI NI UJINGA

View attachment 2040558


Unakuta mtoto kila siku anaenda shuleni, anahudhuria kila kipindi, anafanya home work, n.k. ya nini kumchapa au kumgombeza huyu pale anaposhika namba za kawaida au chini darasani. nimesema namba kwasababu ndicho kigezo ambacho wazazi / walezi wengi hukiangalia, yani hata kama mtoto kafaulu vizuri mitihani lakini wao wanaangalia kashika mafasi ya ngapi.

Wengine huenda hatua za ziada kusomesha watoto wao shule za gharama huku wakiamini pengine ndio suluhisho kwa asilimia 100, matokeo yake mtoto akienda huko na kuwa na uwezo ambao bado shaujafikia mategemeo ya wazazi wake, wanamgombeza kwamba wamejibana sana ili asome huko, mtoto anapewa kipigo kwa makosa ambayo sio yake mithiri farasi aliepelekwa shule ya mamilioni ili awe na uwezo wa kuogelea kama wa samaki.

Ipo hivi wazazi wenzangu, hata sisi binadamu tunatofautiana uwezo,mtoto anaweza kuwa kajaliwa uwezo mkubwa shuleni kiasi kwamba hata akisoma shule hizi za kata zenye changamoto kubwa, unakuta anafaulu vizuri kabisa,

lakini kuna watoto wengine uwezo wao wamejaliwa zaidi sehemu nyingine , hivyo uwezo wa darasani unaweza kuwa mdogo , hawa kuwasaidia inabidi ufanya haya:

  • kuwasaidia wasome shule zenye walimu wa kutosha.
  • kuwalipia tuition, kama hela ipo mletee kabisa mwalimu nyumbani ili kama hajaelewa aelekezwe upya bila kuogopa wenzake.
  • View attachment 2040552
  • usiwapeleke boarding - huko boarding ni kazi sana kujua ana yopitia, pia tuition hakuna.
  • kuwapa moyo,
  • kufatilia mahudhurio yao, homework, n.k

hapo lengo liwe aweze kupata hata ufaulu wa kawaida wa kumfanya asonge mbele, kama ni form 4 basi apate walau division 3

B. KUPUUZA "PLAN B" NI UJINGA ULIOTUKUKA!!

Haijalishi mtoto ana uwezo kiasi gani huko shuleni, kwenye haya maisha haya ya sasa apa bongo huwezi kuweka mategemeo yako yote kwenye njia moja tu ya mafanikio, Nadhani sote ni mashahidi wa jinsi utitiri wa wasomi unavyozidi kujaa mitaani kadri miaka inavyoenda, kwa siku hizi kumaliza degree hapa nchini ni kama kumalza darasa la saba, degree zipo nyingi sana huku mitaani. (Mwenye uhakika wa elimu yake kumpa ajira ni mzanzibari tu, asilimia 21 za ajira za huku kwetu ni zao na pia huko kwao, ni wao tu wenye sifa za kuajiria na serikali yao)

ni wakati wa kusimama na miguu miwli, zile enzi za kusimama kwa mguu moja kusoma ili uajiriwe zilishapita, unahitaji "plan b" ili "plan a" ikifeli bado uwe umesimama na sio kulalamika tu umesoma sana

Kwa watoto wenye vipaji au uwezo flani tangu wadogo, hawa watoto ni mithiri ya chui mwenye mbio na uwezo mkubwa wa kuwinda lakini unapompima kwa kigezo cha uwezo wake wa elimu ya darasani mithiri ya uwezo wa kuogelea, hapo utakua umeufungia uwezo wake wa chui. Kama mtoto unaona wazi kabisa ana kipaji au uwezo flani wewe muendeleze huko, huenda ni kitu alichobarikiwa na ni baraka waliyopewa wachache kufanya vitu vigumu kwa wepesi, wengine inabidi wasomee, kufundishwa na kutia bidii sana lakinii yeye kazaliwa na hiyo baraka, kama anatimiza jukumu lako la yeye kusoma kadri ya uwezo wake basi na yeye apewe nafasi kuendeleza alichojaliwa endapo kina manufaa maana si kila kipaji kina manufaa. unakuta mtoto anapenda sana upishi, ufundi, ushonaji, mpira, kuhubiri / kusoma koran, n.k huyo jua tu ya kwamba hio baraka yake ni zawadi na si ya kupuuzwa, ni baraka inayoweza kuwa plan b.

Kwa watoto wengine, akimaliza form 4 nashauri umpeleke veta mwaka mzima kisha ndio aenelee na shule, huko veta nadhani kozi ni miezi miwili lakini hi huwa ni elimu ya darasani kwa kiasi kikubwa, miei inayobaki inabidi aingie kazini kupata ujuzi zaidi kujua changamoto, kuzoea mazingira, n.k. hapa itamsaidia sana hata akiwa likizo akianza shule au chuo basi atakuwa hashindi mitaani kusubiri likizo iishe, atakuwa bize kujitaftia ridhiki yake, na hii ni mpaka hata akihitimu chuo, yani hatakuwa amekaa tuu yupo yupo anasubiria kuitwa kwenye ajira, hapa atakuwa anafanya mambo yake na neema ikimjia anaweza kusahau kabisa hizo ajira .
Mm hua naangalia wastani
 
Nikiri wazi Mimi ni Miongoni mwa wazazi wanaoadhibu watoto kwa kufanya vibaya masomoni.
But Jana ndio itakuwa Mwisho wa kufanya ujinga huu niliokuwa ninaufanya..
Asante sana mtoa mada,umenifunza vyema.
#MMM
 
Back
Top Bottom