Kupiga Mzinga enzi unasoma

Kupiga Mzinga enzi unasoma

rikiboy

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
21,952
Reaction score
43,265
Aisee kuwa BABA wa familia yataka moyo Sana maana kuna muda Unakuta mwanao anaomba hela unajua kabisaa hapa napigwa Kibomu aisee hasa mwanao akiwa mwanafunzi.... Mimi nlipokuwa mwanafunzi nimekula Sana hela za vitabu na kuna kipindi nikampiga mzee mzinga wa hela ya miwani aisee utoto kazi afu hela yenyewe nlienda kutumia na manzi...

Tuambie enzi unasoma ulidanganya nini upate helaa...!!??? Kwa wazee ulidanganywa nini na ulijua kuwa umedanganywa still ukatoa hela???
 
mshua alikuwa akija na benzi jeusi, lakini nyuma ya shilingi nilikuwa naachiwa mia 500 na panadoli...hakukuwa na njia nyingine zaidi ya kuuza magodoro ya wazembe ama kubadilishana na sahani ya wali kwa mama gumbo
 
nilikua naomba pesa sehem tatu
1.home
2.kwa sister
3.kwa bro
na kote nilikua napata
na wala hawakua wakiwasiliana kuhusu hilo suala ko sija wahi shitukiwa
 
nilikua naomba pesa sehem tatu
1.home
2.kwa sister
3.kwa bro
na kote nilikua napata
na wala hawakua wakiwasiliana kuhusu hilo suala ko sija wahi shitukiwa
Haa ha ha...uliwawezaa!! sema ungezidishaa wangeshtukiaa
 
mshua alikuwa akija na benzi jeusi, lakini nyuma ya shilingi nilikuwa naachiwa mia 500 na panadoli...hakukuwa na njia nyingine zaidi ya kuuza magodoro ya wazembe ama kubadilishana na sahani ya wali kwa mama gumbo
Kwani mlikuwa hamruhusiwi kukaa na hela??
 
Kati ya vitu sijawahi kufanya ni kudanganya kwenye kuomba pesa nyumbani. Kwanza sikuwa muombaji wa pesa, nikipewa hiyo hiyo naridhika mpaka labda itokee inahitajika pesa na ni hitaji la msingi ndio naomba.
 
Haa ha ha...uliwawezaa!! sema ungezidishaa wangeshtukiaa
Huu ndo mchezo wa mdogo angu, anatuma kwa baba, mama, dada yake na mimi message ile ile. Mwanzo hatukujua, Mungu si athumani siku tuko kikao cha familia zikaingia message muda mmoja kusoma kila mmoja anasema ngoja nimtumie fulani pesa, tukaonyeshana. Kwakua ni binti tukamtumia visije vidume vikahudumia. Now ashamaliza chuo ana kazi kaolewa akija kunitembelea nikimwambia anaishia kucheka tu
 
Kati ya vitu sijawahi kufanya ni kudanganya kwenye kuomba pesa nyumbani. Kwanza sikuwa muombaji wa pesa, nikipewa hiyo hiyo naridhika mpaka labda itokee inahitajika pesa na ni hitaji la msingi ndio naomba.
Aisee ulikuwa mwema Sana...Sema sababu ulikuwa wakikee piaa...sisi videmu kutaka makuu akati uwezoo duni so lazima upigee mazinga
 
Huu ndo mchezo wa mdogo angu, anatuma kwa baba, mama, dada yake na mimi message ile ile. Mwanzo hatukujua, Mungu si athumani siku tuko kikao cha familia zikaingia message muda mmoja kusoma kila mmoja anasema ngoja nimtumie fulani pesa, tukaonyeshana. Kwakua ni binti tukamtumia visije vidume vikahudumia. Now ashamaliza chuo ana kazi kaolewa akija kunitembelea nikimwambia anaishia kucheka tu
Haa ha ha Hugo alikuwa mafiaa...!! kwa wakati mmoja
 
me nmesoma mtandaoni nilikuwa napiga vizinga vya salio la data.
 
Nilijenga nyumba kwa kumpiga mzee mzinga ..

Imagine ilikua mizinga ya aina gani ??

Sina cha kuongeza
 
Nlipiga mzinga kwa mshua, ya kuhusu mchango wa mazishi mwalimu mkuu amefariki. Akanipa

Siku tatu mshua akapishana nae mtaani na kumwambia kua mwanangu juzi aliniomba mchango wa mazishi eti umefariki dunia.

Nlipata tabu sana nyumbani na shule week nzima, kama vile waliambizana adhabu nlizokua napata.
 
Back
Top Bottom