Kupigwa, kudhalilishwa na Kunyanyasika kwenye Mahusiano

Kupigwa, kudhalilishwa na Kunyanyasika kwenye Mahusiano

Pole sana Serenity, mlilie mungu wako kamwe hatokuangusha trust me, bali mm ni mwanaume lakn nachukia sana tabia ya baadhi ya sisi wanaume kupiga wanawake, kama mapenzi mtu uyawezi si mwache kwa amani, mtu kakuzalia watoto, anakupikia, anakufulia nguo bado unamgeuza panch bag.!! mwanamke ni kama yai bhana, anaitaj kubembelezwa, kukumbatiwa na kutunzwa kwa kila namna. My mumy alishawai nieleza nitakapokuja oa nisije kupiga mke wangu hata siku moja.
 
Last edited by a moderator:
Huyo ni wife beater na hata acha na ipo siku atakuumiza uwe kilema au hata mauti yakukute. Kaa mbali sana nae, mwanaume anayepiga mke wake mbele ya watoto au ndugu huyo sio mwanaume.

sasa umeongea hapa vema
 
Pole sana Serenity, mlilie mungu wako kamwe hatokuangusha trust me, bali mm ni mwanaume lakn nachukia sana tabia ya baadhi ya sisi wanaume kupiga wanawake, kama mapenzi mtu uyawezi si mwache kwa amani, mtu kakuzalia watoto, anakupikia, anakufulia nguo bado unamgeuza panch bag.!! mwanamke ni kama yai bhana, anaitaj kubembelezwa, kukumbatiwa na kutunzwa kwa kila namna. My mumy alishawai nieleza nitakapokuja oa nisije kupiga mke wangu hata siku moja.


kumbe wa mama wenye maadili bado wapo kwani mh ngoja ninyamazie hapo
 
pole dia wako hawa majini wa kupiga na kungoa nywele wake zao hata wakati mwingine kuwamwaga damu na wakaona nisawa kwo tu kumbe wanajipalia mkaa kwa huyo aliyewapa pumzi
 
The more naskia these stories the more i drift away psychologically from marriage(God help me)..Ngoja nizisake tu hela.

Dad poleMungu akusaidie sana.For now bora watoto wawe mbali na baba yao(my thought) trust me hakuna kitu kibaya kama mtot kuona jinsi mamake anateswa na babaake..inajenga enemity kubwa na ya kudumu.
Kama ni kuzaa kwa uchungu (as per God's words) tayari..be the Man of the family and step up your game!chacharika.
 
Kila mara huwa nawaambia dada zangu mapenzi yawe kitu cha mwisho. Yaani, elimu, uchumi halafu mapenzi, ukiwa na elimu na uchumi bora huwezi kamwe kunyanyasika ktk mahusiano. Kama hisia za ngono zinajaa mwilini unatafuta msela anazipunguza kama tunavyofanya sisi wanaume wakati tukiwa tunasubiri mambo yawe safi. Maisha ni mahesabu.

hahaaaa,umniacha hoi bin taaban
 
Hongera kwa kuchukua uamuzi wa busara.
Jipange na utashangaa utakavyokuwa happy hadi kujiuliza kwanini ulivumilia kiasi hicho.

Chonde chonde wanaume; hakuna kosa lolote ambalo linahalalisha kuumpiga mkeo. Ni udhaifu mkubwa kushindwa kujadiliana na kureason na mkeo, na kuishia kuprove uanaume wako kwa kumpiga defenceless woman. Mbona hamuwapigi ma coleague wenzenu wanapowakosea, kama kweli ni wanaume?

Mwanaume anapiga mkewe ni DHAIFU tu na hana moral authority ya kumuita kiongozi fulani Dhaifu!
 
Tukushauri nini dada?
Umefanya uamuzi wa busaara wa kuondoka, mali na pesa zinatafutwa lakini maisha hayatafutwi.....

Nenda kaanze upya maisha yako, mwanaume ambaye ni abusive huwa haachi, mbaya zaidi mkweo nae mkorofi, hutopata amani kwenye hiyo ndoa/nyumba.

Huyo mwanaume hafai, hafai usirudi nyumba, mwanaume anapiga, anakudharau na kukutukana wa nini? Heri uwe single....

Mungu amemuumba binbadamu na moyo wa kusamehe, in time utasahau na utafungua moyo wako....in time utapenda tena, kwa sasa songa mbele na wanao na maisha yako........

ushauri mzuri sana. that man wont change. madam hajakukata mikono unaweza songa mbele mama. kikubwa ni kuwa tayari tu kiakili kwamba sasa unapambana kivyako. mi naamini kabisa kuwa hakuna lisilolowezekana ni muda tu.
 
Umenikumbusha utoto wangu .. Samahani sintoweza
Kuchangia zaidi.. Very sensitive topic .

pole sana AD. unajua ktk familia za kiafrika ni engi tumeshuhudia either wazazi au ndugu zetu kuwa abused physically. i remember thoooose days my brother in law alikuwa anampiga sana sister angu halafu dada ndo mchakarikaji. tulimshauri sana aondoke but she culdnt. aaah all in all it hurts a lot.
 
Jambo Wanajamii. Ninaandika kwa masikitiko makubwa na majonzi, na stori yangu ni ya manyanyasiko makubwa.

Nimekuwa kwenye relationship huu mwaka wa 5 na huu mwaka wa pili nimekaa na huyu mwanamume as wife. Tuna watoto 2. Jamani nimepitia matatizo meeeeeeeeeengi na nimekuwa navumilia tu. Na mimi ndo nimekuwa nahangaika na kibarua changu kusupport familia. Amenipiga mara mbili vibaya tu, na hata mtoto wangu mkubwa akishuhudia.

Mara ya pili akamwita mama yake ambaye alinisimanga na kunitolea maneno machafu na hata kunivua kanga mbele za wadogo zangu,mwanangu na mkwelima wake. Mwisho walinifukuza na watoto usiku. Hata ninapoandika hapa sina sehemu ya kukaa naomba kujiegesha tu kwa ndugu. Baada ya siku moja akanifuata kuomba msamaha, mimi roho bado nzito. Siku 2 hazijapita akanitumia matusi ambayo si heshima kuandika hapa jamvini na hata kunionesha jinsi anavyobadilisha wanawake na kwamba nisipige jungu atamchukua mwanamke mwingine.

Jamani sina amani na nimekuja kuwachukia saaaaaaaaaaaana wanaume. Nimeondoka na wanangu na sitaki hata wamjue baba yao maana kanifanyia unyama. Wadau naombeni ushauri. Mdogo ana miezi 5 na wamenifukuza usiku.

Natanguliza shukrani.

Unangoja mpaka akuuwe ndio ujue kuwa ulihitaji kuondoka toka kwenye hiyo ndoa/uhusiano mapemaaa!? Watu wanauawa wanatiwa vilema kwenye magomvi ya mahusiano...utakuwa mmoja wa hizo takwimu ukirudi kwenye hiyo nyumba!
 
Hongera sana, natamani wanawake wote wawe kama wewe. Nisambazie elimu hii kwa wasichana hasa wa shule za msingi na sekondari.

asante mkuu. namshukuru Mungu maana amenijalia nimekua mtu ninayeheshimu misimamo yangu. aissee mm ni balozi mzuri sana wa hilo maana nimeshuhudia ndugu zangu wengi sana wakiwa abused na wanaume wao. inaumiza sana,

my mom ni balozi wa hili. imekuwa ni wimbo wake but si unajua tena sometimes mabinti ndo wanakuwa hawataki kutoka japo wanakuwa mistreated,
 
Back
Top Bottom