Godlisten Masawe
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 738
- 283
Huyo ni wife beater na hata acha na ipo siku atakuumiza uwe kilema au hata mauti yakukute. Kaa mbali sana nae, mwanaume anayepiga mke wake mbele ya watoto au ndugu huyo sio mwanaume.
Pole sana Serenity, mlilie mungu wako kamwe hatokuangusha trust me, bali mm ni mwanaume lakn nachukia sana tabia ya baadhi ya sisi wanaume kupiga wanawake, kama mapenzi mtu uyawezi si mwache kwa amani, mtu kakuzalia watoto, anakupikia, anakufulia nguo bado unamgeuza panch bag.!! mwanamke ni kama yai bhana, anaitaj kubembelezwa, kukumbatiwa na kutunzwa kwa kila namna. My mumy alishawai nieleza nitakapokuja oa nisije kupiga mke wangu hata siku moja.
Kila mara huwa nawaambia dada zangu mapenzi yawe kitu cha mwisho. Yaani, elimu, uchumi halafu mapenzi, ukiwa na elimu na uchumi bora huwezi kamwe kunyanyasika ktk mahusiano. Kama hisia za ngono zinajaa mwilini unatafuta msela anazipunguza kama tunavyofanya sisi wanaume wakati tukiwa tunasubiri mambo yawe safi. Maisha ni mahesabu.
Tukushauri nini dada?
Umefanya uamuzi wa busaara wa kuondoka, mali na pesa zinatafutwa lakini maisha hayatafutwi.....
Nenda kaanze upya maisha yako, mwanaume ambaye ni abusive huwa haachi, mbaya zaidi mkweo nae mkorofi, hutopata amani kwenye hiyo ndoa/nyumba.
Huyo mwanaume hafai, hafai usirudi nyumba, mwanaume anapiga, anakudharau na kukutukana wa nini? Heri uwe single....
Mungu amemuumba binbadamu na moyo wa kusamehe, in time utasahau na utafungua moyo wako....in time utapenda tena, kwa sasa songa mbele na wanao na maisha yako........
Umenikumbusha utoto wangu .. Samahani sintoweza
Kuchangia zaidi.. Very sensitive topic .
hahaaaa,umniacha hoi bin taaban
Jambo Wanajamii. Ninaandika kwa masikitiko makubwa na majonzi, na stori yangu ni ya manyanyasiko makubwa.
Nimekuwa kwenye relationship huu mwaka wa 5 na huu mwaka wa pili nimekaa na huyu mwanamume as wife. Tuna watoto 2. Jamani nimepitia matatizo meeeeeeeeeengi na nimekuwa navumilia tu. Na mimi ndo nimekuwa nahangaika na kibarua changu kusupport familia. Amenipiga mara mbili vibaya tu, na hata mtoto wangu mkubwa akishuhudia.
Mara ya pili akamwita mama yake ambaye alinisimanga na kunitolea maneno machafu na hata kunivua kanga mbele za wadogo zangu,mwanangu na mkwelima wake. Mwisho walinifukuza na watoto usiku. Hata ninapoandika hapa sina sehemu ya kukaa naomba kujiegesha tu kwa ndugu. Baada ya siku moja akanifuata kuomba msamaha, mimi roho bado nzito. Siku 2 hazijapita akanitumia matusi ambayo si heshima kuandika hapa jamvini na hata kunionesha jinsi anavyobadilisha wanawake na kwamba nisipige jungu atamchukua mwanamke mwingine.
Jamani sina amani na nimekuja kuwachukia saaaaaaaaaaaana wanaume. Nimeondoka na wanangu na sitaki hata wamjue baba yao maana kanifanyia unyama. Wadau naombeni ushauri. Mdogo ana miezi 5 na wamenifukuza usiku.
Natanguliza shukrani.
Unazingatia?
ofcoz yes
Hongera sana, natamani wanawake wote wawe kama wewe. Nisambazie elimu hii kwa wasichana hasa wa shule za msingi na sekondari.