Kupotea kwa Jabiri Timbula wa mwongozo-Tabora

Kupotea kwa Jabiri Timbula wa mwongozo-Tabora

moto ya mbongo

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2009
Posts
484
Reaction score
337
Naomba kuomba msaada wenu wanajamvi wa JF kuna kijana ametoweka wiki 2 sasa anaitwa JABIRI TIMBULA. Alikuwa ameajiriwa kama VEO kijiji cha Mwongozo Tarafa ya Ulyankulu Wilaya ya Kaliua mkoa wa Tabora. Pamoja na kuajiriwa alikuwa mwanafunzi wa shahada ya kwanza wa chuo kikuu huria (OUT) tawi la Tabora akisoma Bachelor of Arts in Sociology, kabla ya hapo alimaliza kidato cha IV shule ya sekondari Sikonge mwaka 2015 kisha akasomea cheti na astashahada ya Sociology ya chuo cha TEKU cha Tabora. Baada ya kuwa hapatikani katika simu zake hizi 0786 445757, 0767 445757 na 0626 055099 nduguze waliamua kwenda kijiji cha mwongozo kuulizia. Huko waliambiwa kuwa alikuwa ameaga kuwa anaenda Tabora mjini kuendelea na masomo yake hivyo aliondoka kijijini. Wadau tunaomba mtusaidie angalau tujue yupo wapi.
Jabiri Timbula lost.jpg
 
Hatua za muhimu zote zimefuatwa na nduguze. Ila habari zisizothibitishwa zinasema kijana huyu amechunwa ngozi yake na hivyo amepoteza uhai wake!. Inauma sana kwa kweli tunasubiria uchunguzi zaidi kama kuna ukweli kwenye hili. Inatisha sana mtu kutoweka kwa siku nyingi kiasi hiki.
 
Kama nitakuwa nimekosea mnisamehe. Hapa Tanzania hakuna makabila maovu na makatili kama wasukuma na wanyamwezi.

Huwa sitaki hata kushare nao chochote they are too evil.

Ila siyo wote .....na wewe msukuma au mnyamwezi unayesoma post hii haumo😂😂😂
 
Hatua za muhimu zote zimefuatw na nduguze. Ila habari zisizothibitishwa zinasema kijana huyu amechunwa ngozi yake na hivyo amepoteza uhai wake!. Inauma sana kwa kweli tunasubiria uchunguzi zaidi kama kuna ukweli kwenye hili. Inatisha sana mtu kutoweka kwa siku nyingi kiasi hiki.


Anzeni na huyo aliyezungumzia ya kuchunwa ngozi
 
Kama alikuwa na tabia ya kumkosoa jiwe, halafu akasikika na wapambe wa jiwe, basi atakuwa kachuuliwa na wasiojulikana.

Na kama hilo limefanyika hamtakaa mumpate tena. Kuna akina Ben Sa8, Azory, na wengine wengi.
 
Kama alikuwa na tabia ya kumkosoa jiwe, halafu akasikika na wapambe wa jiwe, basi atakuwa kachuuliwa na wasiojulikana.

Na kama hilo limefanyika hamtakaa mumpate tena. Kuna akina Ben Sa8, Azory, na wengine wengi.
Hiyo siyo sababu ndugu kijana alikuwa mpole na tena mwajiriwa wa serikali hakuwahi kufanya hayo masuala. Kuna sababu zingine tu inabidi POLISI wafanye uchunguzi na upelelezi zaidi ili tufahamu ni nini kimempata.
 
Kama nitakuwa nimekosea mnisamehe. Hapa Tanzania hakuna makabila maovu na makatili kama wasukuma na wanyamwezi.

Huwa sitaki hata kushare nao chochote they are too evil.

Ila siyo wote .....na wewe msukuma au mnyamwezi unayesoma post hii haumo[emoji23][emoji23][emoji23]
Mbona unajitetea sana mkuu? Unaweza ukakuta huyo unaemtoa hayumo,anaesoma huu uzi huyo ndio balaaa. We wape tu makavu watajijua wenyewe na tabia zao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom