Reciprocal
JF-Expert Member
- Jan 6, 2022
- 329
- 523
Kuna baadhi ya maeneo hospitali za umma hazipo na kama zipo zinatoa huduma za ngazi ya chini ( Mfano: Litembo(Mbinga), Peramiho( Songea vijijini).Ieleweke kuwa kuna mlipuko wa uanzishwaji wa Hospitali binafsi almaarufu Polyclinics na Specislized clinics hapa nchini ambazo kwa maoni yangu nyingi zimejibatiza majina tu.
Nyingi ya clinic hizi zinategemea malipo kutoka mfuko wa bima ya afya (NHIF) na kiukweli bila NHIF nyingi zitakufa.
Clinic hizi ndio vinara wa kuandika vipimo na dawa bila justification.
Kwa muktadha huu ni vyema Sera ya Afya ihuishwe na kuaccomodate maswala ya Bima ya Afya kwa wote,tukijaribu modal ya Kuwa na mifuko miwili yaani NHIF kwa wale watakaotumia huduma za umma na mfuko mwingine (wa kuratibu ) bima za afya za binafsi.
Inasikitisha kuona baadhi ya uncontrolled private sector wakitaka kuufilisi mfuko huu.
Aidha NHIF iache kukurupuka kila mara na kwa kumbukumbu zangu ni kuwa ilipaswa kuratibu mfumo wa / swala la bima ya afya kwa wote japo hadi sasa hakuna kinachoeleweka.
Pia Kuna suala la kupunguza mlundikano wa wagonjwa( Mfano: Bugando(Mwanza))
Pia suala la utendaji mzuri na wa haraka katika kuhudumia wagonjwa( hospitali za serikali baadhi ya wafanyakazi wanafanya kazi wanavyojisikia(hasa baada ya kuondoka Magufuli). Kwahiyo, hospitali za private ni muhimu Sana hasa katika kutoa huduma bora na za haraka(Hatahivyo, kuwepo na follow up na monitoring ya kile kinachofanyika).