Kupunguza miaka ya uchakavu wa magari kutoka miaka 10-8

chipalila1

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
259
Reaction score
32
Kwa wenye taarifa kuhusu hili watujuze, vipi TRA wamesha anza kutumia sheria hii kama ilivyopendekezwa na waziri wa fedha? Mwenye kujua naomba anijuze.
 
tayari mkuu,tumeshaonja machungu yake
ingia kwenye web ya tra angalia calculator ya magari new version 19 ni balaaaaa
 
tangu tarehe 1 july ndo mwaka wa fedha unaanza.... tayari wananchi wenzio tushalia, kigari changu kimenasia apo, kodi karibia mara mbili ya kununulia gari japan. Kuna gari nimeagiza mpya kiwandani ni dola 28,000 lakini TRA wameandika dola 42,000 na pointi...ni shida!!
 

pole sana mkuu, hii nchi inavyo endeshwa ni hatari.
 
hawa jamaa wa TRA ni watu wa ajabu sana na wameshindwa kumpa unafuu mwananchi wa kawaida tu anayetaka kujikwamua na adha za usafiri,sijui source ya RSP wanaitoa wapi wakati saa nyingine hata bei ya kiwandani ni chini ya wanaokulazimisha wewe kulipia,utakuta gari CIF hadi dar ni $1200(Shs.2,120,000/=) utashangaa ukijumlisha na gharama za kulitoa bandari utaambiwa Mil 6.6,hivii hapo Serikali kuipitia TRA ina nia kweli ya kuwainua au kuwakandamiza wananchi weke??
 

mifumo ya hii serikal ni kandamizi, watendaj wa tra wanajiona miungu watu, wanafanya wanavyojisikia.
 
Serikali ingekuwa na akili kodi za magari wangezipunguza ili yanunuliwe mengi, af wakakusanya kodi za kutosha kwenye mafuta.
 
du wengne kama mambo ndvyo yalvyo tutazehekea kweny daladala
 
Serikali inatoza kodi kubwa kuliko hata wanaoyatengeneza, ukitaka kufaidi hii nchi uwe mwanasiasa au fisadi
 
Tatizo ata ukinunua lililo ndani ya miaka nane ushuru ni mkubwa sana,tulitoa Harrier ya mwaka 2007 ushuru pekee ulikuwa 14Ml maana ktk hesabu za Tra wanaweka C.I.F ya juu sana kwa magari yaliyo ndani ya miaka 8.Hii ni habari mbaya si kwetu tu bali ata kwa wauzaji Japan /Dubai,maana wauzaji wanapata faida nzuri kama wakiuza gari za zamani (zaidi ya miaka kumi) kuliko hizi za ndani ya miaka 8.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…