Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu wengi ni wavivu tu mimi natia gambe na mazoezi kama kawaida tu.😁😁😁Hana madeni huyu itakuwa. Hawezi kupungua
🤣🤣🤣🤣 Hatari hiyo fasta tuuHii uhakika kabisa akipiga mlo mmoja wiki moja tu, nguo zinapwelepweta
Haya mazoezi si ndo yale ya yule msauzi ya kukuza nyash "squat" sijui mnaitaHana madeni huyu itakuwa. Hawezi kupungua
Kilo 10 mpaka 15 kwa mwezi ni kujitafutia matatizo ndugu. Nakushauri:Habari wakuu naomba ushauli wa kupunguza uzito kwa haraka zaidi naona ninapoelekea sio kuzuri, je nitumie dawa gani maana kwa kufanya mazoezi nitakuwa muongo sina muda huo kabisa
Umri: 25
Uzito wa Sasa: 100 kg
Lengo: Kupunguza kilo 10-15 kwa mwezi mmoja.
Sina unene kupita kiasi, lakini nina mwili mkubwa na kitambi kidogo.
Ninaweza kukimbia na kufanya kila kitu kwa ufasaha kabisa lakini nina minyama nyama kwenye kifua imeshuka ndo kinachonikela zaidi
Nina nia ya kupunguza uzito kwa njia yoyote isio na madhara. Naomba ushauri wenu kuhusu dawa gani nzuri naweza kutumia ikafanikisha lengo langu
Asante
Sasa ntakula nini jamaniNiliona watu wanafanya mazoezi asubuhi halafu hao wanaenda restaurant kula mapochopocho, nikacheka sana maana mule kulikuwa na vibonge na havipungui...cha kwanza kabisa cha kuzingatia unakula Nini?. Badilisha kwanza namna unavyokula, unaweza punguza kilo nyingi Kwa namna nzuri ya kula tu.
Utumbo keshauzoesha hawezi tena kukaa bila kula.Kuna brother angu in town namuita DON, nae amekua akihangaika Sana na madawa ya kupunguza uzito.
Kaenda Hadi Thailand, gym Sana Ila wapi, hana dalili yoyote ya kupungua.
Siku nmempitia kwake tuwai bandarini alfajiri Sana, kaamka na kumwamsha mkewe ampashie kiporo na chai, jamaa kapiga. aisee nikamshangaa sn alfajiri yote na viporo, jamaa akadai ndo kazoea hivo.
Tuko kwny foleni, nikaagiza maji baridi, Jamaa nae kanunua coca-cola ya baridi, kaipiga yote.
Tumefika bandari, mishe zikawa nyingi, Saa 3 asbh akadai njaa inauma sn, tukapate supu, nkamkatalia mpk tumalize mishe mishe Kwanza, saa 5 sio mbali.
Jamaa UZALENDO ukamshinda, kaagiza vitumbua 5 na juice ya bharesa. Kapiga vyote wkt Mi Bado Hata chupa Moja ya maji Lita 1.5 nilonunua kwny foleni sijaimaliza.
Saa 5:30 tushamaliza mishe mishe, saa 6 tuko k'koo OFSIN kwangu, jamaa anaulizia wale wadada wa delivery ya lunch Huwa wanapitisha msosi saa ngapi🤔
Ushauri wangu; usitumie njia za mkato za kupunguza unene kwani zitakuletea matatizo. bali zingatia ratiba ya mlo kwa kufunga au kupunguza kiwango Cha chakula unachokula;Habari wakuu naomba ushauli wa kupunguza uzito kwa haraka zaidi naona ninapoelekea sio kuzuri, je nitumie dawa gani maana kwa kufanya mazoezi nitakuwa muongo sina muda huo kabisa
Umri: 25
Uzito wa Sasa: 100 kg
Lengo: Kupunguza kilo 10-15 kwa mwezi mmoja.
Sina unene kupita kiasi, lakini nina mwili mkubwa na kitambi kidogo.
Ninaweza kukimbia na kufanya kila kitu kwa ufasaha kabisa lakini nina minyama nyama kwenye kifua imeshuka ndo kinachonikela zaidi
Nina nia ya kupunguza uzito kwa njia yoyote isio na madhara. Naomba ushauri wenu kuhusu dawa gani nzuri naweza kutumia ikafanikisha lengo langu
Asante
Bwana kibonge pole sana mwili unakera mno kwa taarifa zako ni kwamba wewe huli sana wala kufakamia fakamia mamisosi, iko hivi watu wengi wanakimbilia kuchangia pasipo kuangalia sababu moja , kwa maelezo yako wewe una mwili wa asiliNikweli sina muda
Unachosema ndiyo sahihiBwana kibonge pole sana mwili unakera mno kwa taarifa zako ni kwamba wewe huli sana wala kufakamia fakamia mamisosi, iko hivi watu wengi wanakimbilia kuchangia pasipo kuangalia sababu moja , kwa maelezo yako wewe una mwili wa asili
Mwili wa asili ni mbaya sana utafanya mazoezi ,utafanya diet ila ukitulia wiki tu huooo ndambi hilooo , kwanza unatakiwa uangalie je una asili ya mwili kama una asili ya mwili piga mazoezi kutia wepesi uwe kibonge mwepesi ila kupungua sahau kabisaa