Kupunguza wafanyakazi kwa kutoa notice of termination ya siku 30 lakini hakukuwepo na consultation wala notice for intention of retrenchment

Shukran kwa elimu hii, naomba kuuliza sheria inasemaje muda wa kupeleka shauri CMA, maana tangia nipewe notice of termination ni siku 20 sasa zimepita, zimebaki siku 9 ambazo naendelea kufanya kazi kama notice inavyosema kwahyo muda wa kwenda CMA unakuwa mgumu.
Je nikisubiria mpaka siku ya mwisho ya notice kuisha nitakosa haki yangu. Ni upi muda wa kureport CMA kisheria?
 
1. Kabla ya Kuondoka kazini rasmi(Tarehe ya mwisho ya kufanya kazi) Siku 30 toka tarehe ambayo ulipewa taarifa ya retrenchment- kama utaenda kuchange validity of the reason for the retrenchment (hivyo kesi itaenda CMA kwa ajili ya Usuluhishi(Mediation)
2. baada ya Kuachishwa kazi unaweza kufungua kesi ya Unfair termination(CMA) ndani ya Siku 60 toka tarehe ya kuachishwa kazi.
Kwa upande wangu,ningekushauri kwa sasa ukachallenge kupitia option namba 1 kwani mwajiri atazuiliwa kuendelea na rentrechment processes huku issue zingine zikiendelea kupatiwa ufumbuzi.
 
Kwenye kuchallange retrenchment process, sawa vip ikiwa sinaiman tena ya kuendelea na kazi kwa mfano mwajiri anaonesha nia ya kutonihitaji kazin ikiwa ni kunidai vitu vyote alivyonipa na ikiwemo zawadi imebidi nizirudishie na huwa hataki maongezi na mimi.

Kama nitazuia process ya retrenchment si inamana nahitajika kuendelea? Si naweza undiwa zengwe nikiwa kwenye eneo la kazi?.
 
Pole sana, naomba kukuuliza ;
1. unataka nini?
kuendelea na kazi,kulipwa stahiki zako au kitu gani hasa unachohitaji?maana naona bado hujawa specific kujua unataka nini?maana huwezi jua hatua za kufuata kama bado hujafahamu unachotaka.

ila narudia tena tafuta WAKILI/MWANASHERIA WALIOBOBEA KATIKA MASUALA YAKAZI ili upate msaada na mwongozo kamili.Maana kutype kwa muda mrefu kidogo changamoto.
 

Hatua na timing ya unfair termination ndo lengo langu,
Maana siwezi lazimishia nisifutwe kazi wakat wao washanikataa, ndomana wakanipa notice na sababu zao et taasisi inapitia changamoto ya kifedha wakati huo hatukaa, sikuitwa wala kuzungumzia hizo changamoto wanazo sema zaidi tu ya kupewa notice ya Siku 30.
 
basi hakuna tatizo,cha muhimu subiri hadi siku ya mwisho ifike na ukishapatiwa barua ya kuachishwa kazi basi taratibu zingine zote zitaanza.
pia kama inawezekana tafuta ushahidi wa yafuatayo uwe nao pembeni tu(japo katika mashauri au kesi za mambo ya kazi ni jukumu la mwajiri kutoa ushahidi kuwa termination was fair) jitahidi kuhakikisha kuwa unapata vifuatavyo kabla hujatoka hapo;
1. piga picha ya tangazo lilitolewa la kupunguza wafanyakazi,ambayo itaonyesha tarehe na mwezi ambao lilitolewa.
2.naimani uko na barua yako ya kukuruhusu uende likizo(anayoonyesha tarehe ya kutolewa barua,tarehe ya kuanza na kumaliza likizo pamoja na tarehe ya kurudi kazini.)
3.Notice ya rentrenchemnt
4. muhtasari wa majadiliano ya kupunguza wafanyakazi
pia andaa kabisa document zifuatazo;
5. Mkataba wako wa ajira
6.nakala zako utakazopewa za kupunguzwa kazini pamoja na cheti cha utumishi.
hizo nyaraka zote ukiweza kuwa nazo ni vyema kwani itamsaidia Wakili/Mwanasheria wako kuwa na wigo mpana ya namna ya kuliendea suala lako.

Mwisho kabisa,jipe muda wa kurelax na cool down kabla ya kufanya maamuzi yoyote,Wish you all the best na imani utakuwa umepata mwanga kiasi.
 
Oh Asante be blessed 🙏
 
Hivi kama una mkataba let's say wa mwaka mmoja na imepita zaidi ya miaka mitatu ujawai kusaini mkataba ila stahiki zote unapata je ikitokea umepewa termination letter kisheria hii imekaaje
 
Hivi kama una mkataba let's say wa mwaka mmoja na imepita zaidi ya miaka mitatu ujawai kusaini mkataba ila stahiki zote unapata je ikitokea umepewa termination letter kisheria hii imekaaje
Kama mwanzo ulipewa mkataba wa mwaka moja ukiisha bila kusaign mwingine na ukaendelea kufanya kazi maana yake huo mkataba umejirenew automatic, nisawa nakusema mkataba wako mpaka sasa umejirenew ni mara ya pili. niwajibu wako kujua ulianza kazi lini, unakoma lini na upige hesabu Stahiki zako.
 
Hivi kama una mkataba let's say wa mwaka mmoja na imepita zaidi ya miaka mitatu ujawai kusaini mkataba ila stahiki zote unapata je ikitokea umepewa termination letter kisheria hii imekaaje
alichoshauri jeremiamnzava yuko sahihi kabisa,ila sasa hapo tayari mkataba umeshabadilika na kuwa wakudumu,Sababu hufahamu au hauna expiration period.Muhimu endelea kupiga kazi na cautions katiak kila kitu unachofanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…