Kupunja vipimo (kwenye mizani), biashara inadumaa

Kupunja vipimo (kwenye mizani), biashara inadumaa

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Leo nimeguswa niandike kidogo kuhusu vipimo

Kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wanapunja watu kwa maksudi kabisa wakiwemo masikini kupitia vipimo mbali mbali kwa;
  • Kuharibu mizani au yale mawe ya kupimia
  • Kubonyeza ndoo au galoni za kupimia mazao
  • Kuharibu vipimo vya vimiminika nk
Hilo la mizani nimelishuhudia sana. Kuna baadhi ya wafanya biashara huwa na mawe feki ya kupimia na yale mazuri. Inamaana anajua anachokifanya na akiona wale wakaguzi hutoa yale mazuri wakiondoka hurudisha yale feki.
Wengine hufanya hivyo kwa vipimo mbalimbali vya nafaka, mafuta ya maji nk

Niseme tu kuwa, hakuna mfanyabiashara atatajirika kwa kupunja vipimo na kama wewe ni mmoja wapo; jua tu kuwa, unafanya kosa kubwa sana na kwa mujibu wa maandiko, hutakaa ufanikiwe. Unaweza kushangaa unauza miaka nenda rudi biashara haikui kumbe tatizo ni laana ya kupunja kwenye mizani. Lakini hata kwa elimu ya kawaida ya masoko inakubaliana kuwa, hutakaa utajirike kwani unafukuza wateja

Kama una amini kuwa ipo siku ya mwisho (siku ya hukumu) jua tu kuwa, kupunja kwenye mizani ni sawa na kujipalilia mkaa.

Chukua hatua ya kujirekebisha ukuze biashara yako lakini pia uwe na wakati mzuri siku ya mwisho.
 
Duniani kumejaa rafu nyingi sana wanyonge ni ngumu kusurvive.

Kuharibu vipimo sio ujanja ni ushamba
 
Mzani wa kuuza na wakununua lazima inakua tofauti na wanakupiga fasta kabla hujafungua macho na biashara ndio imeisha

Wakati wa kuuza kitu chako cha kg 100 mzani wao utasoma 80kg ili wakupige hiyo 20kg na wakati wa wewe kununua ni vice_versa
 
Uislamu umelieleza hili jambo siku nyingi sana

Nikipokua chuo Rafiki yangu ni mkristo alinambia kwamba alivokua mdogo akitumwa gengeni na mama ake anaambiwa aende kwa wauzaji Waislamu kwani hawapunguzi vipimo na mambo mengine

Karibuni kwenye Uislamu mujifunze maisha
View attachment 2700881
 
Leo nimeguswa niandike kidogo kuhusu vipimo

Kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wanapunja watu kwa maksudi kabisa wakiwemo masikini kupitia vipimo mbali mbali kwa;
  • Kuharibu mizani au yale mawe ya kupimia
  • Kubonyeza ndoo au galoni za kupimia mazao
  • Kuharibu vipimo vya vimiminika nk
Hilo la mizani nimelishuhudia sana. Kuna baadhi ya wafanya biashara huwa na mawe feki ya kupimia na yale mazuri.

Inamaana anajua anachokifanya na akiona wale wakaguzi hutoa yale mazuri wakiondoka hurudisha yale feki.

Wengine hufanya hivyo kwa vipimo mbalimbali vya nafaka, mafuta ya maji nk

Niseme tu kuwa, hakuna mfanyabiashara atatajirika kwa kupunja vipimo na kama wewe ni mmoja wapo; jua tu kuwa, unafanya kosa kubwa sana na kwa mujibu wa maandiko, hutakaa ufanikiwe. Unaweza kushangaa unauza miaka nenda rudi biashara haikui kumbe tatizo ni laana ya kupunja kwenye mizani. Lakini hata kwa elimu ya kawaida ya masoko inakubakiana kuwa, hutakaa utajirike kwani unafukuza wateja

Kama una amini kuwa ipo siku ya mwisho (siku ya hukumu) jua tu kuwa, kupunja kwenye mizani ni sawa na kujipalilia mkaa.

Chukua hatua ya kujirekebisha ukuze biashara yako lakini pia uwe na wakati mzuri siku ya mwisho.
Waambie wakasome na wajitahidi kuilewa Suratul Mutaffifin, sura ya 83 katika Quraan. Aya zake za mwanzo ni hizi hapa chini.

1. Ole wao hao wapunjao!
2. Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
3. Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
4. Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
5. Katika Siku iliyo kuu,
 
Uislamu umelieleza hili jambo siku nyingi sana

Nikipokua chuo Rafiki yangu ni mkristo alinambia kwamba alivokua mdogo akitumwa gengeni na mama ake anaambiwa aende kwa wauzaji Waislamu kwani hawapunguzi vipimo na mambo mengine

Karibuni kwenye Uislamu mujifunze maisha
View attachment 2700881
Suratul Mutaffifin, Sura ya 83
 
Wauza nyama Mungu anawaona hasa wale wa minadani
 
Uislamu umelieleza hili jambo siku nyingi sana

Nikipokua chuo Rafiki yangu ni mkristo alinambia kwamba alivokua mdogo akitumwa gengeni na mama ake anaambiwa aende kwa wauzaji Waislamu kwani hawapunguzi vipimo na mambo mengine

Karibuni kwenye Uislamu mujifunze maisha
View attachment 2700881
Wewe ni mpuuzi sana zaidi ya kukalia mboo hakuna la maana unaloweza kabisa
 
Waambie wakasome na wajitahidi kuilewa Suratul Mutaffifin, sura ya 83 katika Quraan. Aya zake za mwanzo ni hizi hapa chini.

1. Ole wao hao wapunjao!
2. Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
3. Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
4. Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
5. Katika Siku iliyo kuu,
Tumia akili mjinga wewe mbona hata hiyo biblia imekataza pia? MbOna munaingiza udini kwenye jukwaa hili?
 
Tumia akili mjinga wewe mbona hata hiyo biblia imekataza pia? MbOna munaingiza udini kwenye jukwaa hili?
Mjinga wewe na pumbavu sana. Kama biblia inakataza umenyimwa kuleta aya? Mkuu Ndugu wewe.
 
Uislamu umelieleza hili jambo siku nyingi sana

Nikipokua chuo Rafiki yangu ni mkristo alinambia kwamba alivokua mdogo akitumwa gengeni na mama ake anaambiwa aende kwa wauzaji Waislamu kwani hawapunguzi vipimo na mambo mengine

Karibuni kwenye Uislamu mujifunze maisha
View attachment 2700881
nanunua mahindi ya bisi (popcorn) kwa wapemba mwaka wa 6 sasa zamani hali ilikuwa tofauti lakini saiv ukinunua 2kg karibia robo inapungua hawa wapemba ni wakristo? Huu mchezo wanafanya wafanyabiashara wote
 
nanunua mahindi ya bisi (popcorn) kwa wapemba mwaka wa 6 sasa zamani hali ilikuwa tofauti lakini saiv ukinunua 2kg karibia robo inapungua hawa wapemba ni wakristo? Huu mchezo wanafanya wafanyabiashara wote
kuwa muislam au kuwa mpemba sio tiketi ya kufanya mabaya.ni dhambi yeyote atakayefanya
 
Back
Top Bottom