Haya ndio aliyoaandika Mheshimiwa Zitto Kabwe kwenye FACEBOOK PAGE yake:
Siri? Wazi?
Wabunge wamegawanyika, wananchi wamegawanyika. Wachambuzi kama Mimi Mwanakijiji na wengine wanashauri kura ya wazi. Mgawanyiko pia umekaa kivyama ambapo wengi wa wabunge wa CCM wanataka iwe wazi na wengi wa wabunge wa upinzani wanataka iwe siri. Wajumbe wa BMK (Bunge Maalum la Katiba) kama Maria Sarungi-Tsehai na wanataka kura ya Siri. Siri au Wazi imekuwa habari kubwa na imesheheni vyombo vya habari. Mwafaka umekosekana.
Kwa nini Siri?
Kura ya siri humlinda mpiga kura asijulikane chaguo lake na hivyo kama kuna madhara ya chaguo lake huepukwa. Hii ni pamoja na kuadhibiwa kwa kunyimwa fursa fulani fulani au hata kuondolewa kwenye chama cha siasa alichomo. Wanaotaka kura ya siri wanataka ulinzi dhidi ya madhara hayo na pia kuwapa uhuru zaidi wabunge kuamua bila ya woga. Chaguzi zote kuu duniani kote hufanyika kwa kura ya siri.
Kwanini Wazi?
Kwenye mabunge takribani yote duniani kura huwa wazi. Lengo ni kuweka wazi misimamo ya vyama/makundi kwani mabunge hupata wabunge kutoka kwenye vyama/makundi. Hivyo inakuwa ni vema wawakilishi hao wajulikane kwa makundi yao kama wamepiga kura kwa matakwa ya makundi na sio matakwa binafsi.
Kura ya Wazi pia huweka rekodi ya mbunge/mwakilishi binafsi na hivyo kujua misimamo yake kutokana na rekodi yake ya kura. Kwa mfano mgombea Urais nchini Marekani anajulikana sera zake kwa kuangalia historia yake ya kura kama alikuwa Seneta au Mwakilishi (Congressman/woman).
Wabunge wafanyaje?
Siku ya Jumatatu wabunge wataamua kama wapige kura ya siri au ya wazi kwa kupiga kura ya siri. Nasikia kampeni zinaendelea Dodoma kuhusu uamuzi huo. Siasa zetu tunazifanya ni 'zero-sum game' kwamba anayepata anapata vyote na anayekosa anakosa vyote. Haipaswi kuwa hivyo hata kidogo.
Tufanye hivi;
- Kwa kuwa vifungu vya Katiba ni masuala (issues) basi ni vema kifungu kwa kifungu kura ziwe za wazi ili wawakilishi wa makundi wenye maslahi na masuala yao wajue misimamo ya kila mjumbe na rekodi ziwe wazi. Kama mtu anaunga mkono ndoa ya mashoga ajulikane, anayeunga mkono haki ya kupata elimu bila vikwazo ajulikane nk.
- Upitishaji wa Katiba nzima ufanywe kwa kura Siri ili kutunza uhuru wa Mjumbe kuamua kuhusu katiba kama ilivyo kwa wananchi watakapopiga kura kwenye 'referendum' kwa siri.
Ni vema vyama vya siasa vitambue kuwa Katiba inayotakiwa ni ya wananchi na sio katiba ya vyama. Hivyo kuweka misimamo ya kivyama kunaondoa kabisa dhana nzima ya kuandika Katiba na kupata mwafaka. Ni vema kwa chama kama CCM kuacha kabisa kutumia wingi wake kuburuza mchakato wa Katiba. Bila mwafaka Katiba haiwezi kupatikana.
It must not be a Zero-Sum Game.......
Absalom Kibanda Mwananchi Communications Ltd Ismail Jussa January Y. Makamba David Kafulila William J. Malecela John MnyikaDennis Msacky Bunge la Katiba
Maelezo ni sahihi kabisa.
Weka kwenye muktadha wa sasa ndani ya bunge hili.
CCM ilifanya hila kuweka wajumbe wengi kwa migongo ya aina ya vikundi vyoteili sera zake zipite , lakini bado hao hawaaminiki na CCM japo wanawahonga na kuwaahidi zawadi mbali mbali, hivyo ni muhimu ihakikishe hawafanyi kosa.
Wajumbe hawa walioteuliwa kama hongo wametishwa sana na watawapendeza ccm kwenye kura ya wazi lakini ikiwa ya siri ni piga ua na ni mwisho wa CCM. Na CCM inajua hilo, hivyo lazima wapiganie kura ya wazi.
Mpaka sasa CCM ndio chama kilichopoteza kwa asilimia kubwa sana kwenye rasimu ya Warioba ndio maana walileta rasimu nyingine haramu mbadala na kumtukana mzee Warioba saa zote.
Ni CCM pekee isiyowaamini wajumbe wake, na ndio yenye uwezo wa kuadhibu na kuwazawadia wajumbe kadiri ya utendaji wao.
Hivyo, kura ya wazi ni ya muhimu sana kwa CCM kuliko ya siri kwa CDM
CCM iliyopo sasa ni ya MAFISADI na wenye uchu wa madaraka, CCM ya nyerere imepokwa, ndio maana ya sasa siyo shirikishi ni ya wateule.
Ikumbukwe CCM ndio ilo vunja muungano, msingi ni mkapa na kikwete ka sakafia kwa katiba ya znz. sasa leo wana haha, wameona wakitoka asilimia 90 ni makuruta wa segerea
ZZK ni kipenzi cha CCM Mafisadi, hivyo atawatetea kwa namna yoyote ile hasa penye mwanya wa hoja. Zaidi na yeye ni mnufaika wa huo ufisadi