Pre GE2025 Kura za Maoni CCM: Mambo muhimu Mbunge wa Moshi Mjini anayohitajika kuyafanya na kuyamaliza kabla ya October 2025.

Pre GE2025 Kura za Maoni CCM: Mambo muhimu Mbunge wa Moshi Mjini anayohitajika kuyafanya na kuyamaliza kabla ya October 2025.

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mpendwa Mbunge wa Moshi Mjini,

Natumai uko salama na unaendelea vizuri.

Kama mwananchi wa Moshi, na mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM, Moshi Mjini, naandika barua hii kukujulisha kuhusu vipaumbele muhimu vya maendeleo ya mji wetu, ambayo ni muhimu kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Ni muhimu kutambua kwamba ikiwa unataka kuchaguliwa tena, unapaswa kuchukua hatua za haraka na madhubuti katika utekelezaji wa mipango hii kabla ya uchaguzi mkuu October 2025.

Vipaumbele vya Moshi Manispaa unavyohitaka kuvifanyia kazi haraka na ambavyo wapigakura walikutuma Bungeni

1. Ujenzi wa Barabara za Njia Nne:
Ujenzi wa barabara za njia nne kutoka Mijohoroni kupitia YMCA kuelekea Arusha hadi Maili Sita ni muhimu ili kupunguza msongamano wa magari na kuboresha usafiri.

Barabara hii itasaidia kuunganisha maeneo mbalimbali na kurahisisha usafiri wa abiria na mizigo.

2. Ujenzi wa Barabara ya Njia Mbili kutoka YMCA hadi KCMC Hospital:
Barabara hii ni muhimu kwa ajili ya huduma za afya, kwani itarahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wakazi wa Moshi. KCMC ni hospitali kuu, na barabara hii itahakikisha kuwa wagonjwa wanapata huduma haraka zaidi.

3. Ujenzi wa Stand Kubwa ya Mabasi Nganga Mfumuni:
Ujenzi wa stand hii utasaidia katika kupanga na kusimamia usafiri wa umma, kupunguza msongamano na kuboresha hali ya usafiri wa abiria. Stand hii itakuwa na uwezo wa kuhudumia mabasi mengi na itatoa huduma bora kwa wakazi wa Moshi.

4. Ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa King Jorge, Memoria:
Uwanja huu utatoa nafasi kwa vijana kushiriki katika michezo na shughuli za kijamii. Ni muhimu kuunga mkono vipaji vya vijana na kuimarisha afya zao kupitia michezo.

5. Kuvunja Majengo ya Zamani ya Hospitali ya Mawenzi:
Hospitali ya Mawenzi inahitaji ukarabati wa kina. Kuvunja majengo ya zamani na kujenga majengo mapya ya kisasa kutasaidia kuboresha huduma za afya na kutoa mazingira bora kwa wagonjwa na wafanyakazi wa afya.

6. Uwekaji wa Taa za Barabarani:
Uwekaji wa taa za barabarani nje na ndani ya mji utaboresha usalama wa barabara, hasa usiku. Taa hizi zitasaidia kupunguza ajali na kuongeza usalama kwa watembea kwa miguu na waendesha baiskeli.

7. Kuupanua Mji wa Moshi na Kuufanya Jiji:
Kuupanua mji wa Moshi na kuufanya jiji kutasaidia kuleta maendeleo zaidi. Hii itahusisha mipango ya ujenzi wa miundombinu, huduma za kijamii, na kuboresha mazingira ya biashara.

8. Kulipa / Kutimiza ahadi ulizo Ahidi taasisi mbali mbali,vikundi,watu binafsi kwa haraka iwezekanavyo.

Hitimisho

Moshi ni mji wenye uwezo mkubwa wa kuendelea na kuleta maendeleo kwa jamii yetu.

Hata hivyo, ili kufikia malengo haya, ni muhimu kwa wewe kama mbunge kutekeleza mipango hii kwa haraka na kwa ufanisi vinginevyo,usigombee Tena ubunge.

Wananchi wa Moshi wanatarajia kuona hatua chanya zinazochukuliwa na wewe kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Tunaamini kwamba kama utaweza kutekeleza vipaumbele hivi, utajijengea msingi imara wa kuweza kuchaguliwa tena katika uchaguzi ujao.

Tafadhali chukua hatua hizi kwa umakini, na hakika tutakuunga mkono katika juhudi zako.

Asante kwa muda wako, na tunatarajia kuona mabadiliko chanya katika mji wetu wa Moshi.

Wako kwa dhati,

Wajumbe Wapiga kura za maoni ( Mkutano Mkuu wa CCM 2025, Moshi Mjini -Tanzania


CC: KATIBU WA CCM MOSHI MJINI.
Acha kupotosha watu mbunge kafanya kazi kubwa sana kuliko wapinzani waliokaa kwa miaka 20 usijidai mwanaccm kumbe mpinzani kibaraka wa Ibraline acha kupotosha mbunge amefanya makubwa sana nipongezi kubwa sana kwake na hata mpaka sasa nenda pale mawenzi usikie aibu majengo yalivyojengwa na njoo mbuyuni pameungua kajitahidi pamejengwa hapa kuwa katika ahadi.. njoo magari ya ZIMAMOTO au haya yote sio kazi alitakiwa atoe pesa MFUKONI na huyo mbunge anayetoa fedha MFUKONI kwake ni yupi au kazi ni zipi afanye ilimseme kafanya??

Stand ngangamfumuni tayari kashaipigania na sasa wakandarasi wanarejea kuanza kazi na UWANJA WA ndege nao utaanza kujengwa hivi punde pesa ishawekwa na serikali kuu je ajenge nini turidhike???
 
Cha kushangaza zaidi na kusikitisha,mbunge anakuja na Gari la fire kutoka Dodoma kulikabithi manispaa.

2. Ambulance ya hospital ya mawenzi kutoka Dodoma,kuikabithi

3. Ukarabati wa uwanja wa majengona uwanja wa ndege.

4. Kujebga kwa kiwango cha lami Barabara ya kwenda nyumbani kwake.

Hivi vyote sio vipaumbele vya wapiga kura wa Moshi na wapiga kura wake.

- Nani alimtuma kuvileta ??


Iwao hataharakisha na kutejelezs majukumu aliyotumwa na wananchi na wanachama wa CCM, October 2025, lazima akachunge mbuzi Rombo.
Ajabu sana kwani wewe unatumia aina gani ya akili kichwani kwako??

Unakiri kuleta gari je ulitaka alete nini maendeleo ni aina Tofauti ya miradi na utatuzi WA kero aina mbalimbali sasa wewe ulitaka alete gari ya kutembelea??

Unakiri ukarabati wa Uwanja wa mpira na uwanja wa ndege je ulitaka ajenge mpya au hayo sio maendeleo??

Kajenga barabara ya kwenda kwake kwanini unapotosha jamii kiasi hiki kwanini usiseme kweli hujaona boss wako ibraline amejenga kale kasheli kake kwenye open space??

Endelea kutumwa kupotosha ila Moshi inakwenda na PRISCUS TARIMO BINGWAA
 
Back
Top Bottom