Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,363
Hodi Hodi Jamvini, Malenga na wasomaji,
Tafadhali tambueni, tumeupata mtaji,
Tunakuja uwanjani, jengo tunalihitaji,
Kura zenu ni muhimu, ili kuwa wapangaji.
Timu imekamilika, kila idara yatosha,
Slaa tumemsimika, kamwe hatotuangusha
Sera amezitamka, Mtanzania kuneemesha,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Kazunguka mikoani, sera kuelezea,
Watoto madarasani, vyuoni na chekechea
Kulipia asilani, shule bure kupatia
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Wafanyakazi kakumbuka, kilio chao cha kale
Mishahara kufutuka, kuwafanya watoto wale
Chochote wakikumbuka, mifukoni ziko hela
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Timu haijatimia,jengoni kumsindikiza
Baregu anafuatia, uzushi kuudamaza,
Mabere afuatilia, sheria kuwaeleza
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Zitto pia Ndesamburo, wote wanaunguruma,.
Halima pia Mbogoro, kidete wamesimama,
CCM wana Kihoro, wamuonapo Lema,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Nimtaje naye Mbowe, Mbilinyi jimbo la Mbeya,
Na anatamba Shamwee, kule Vijijini Mbeya,
Waonekanapo mayowe, Nisemacho si umbea,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Swali sasa ni lako, wewe unisomaye,
Ulanga na Makambako, Hassani, Pili, Simbeye,
Muhimu ni kura yako, wa CHADEMA umpendaye,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Kura peke haitoshi, Kuzilinda ni lazima,
Bukoba Lindi na Moshi, kura kuzitazama,
Itamaliza ubishi, itasimama CHADEMA,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Kwa wingi tujitokeze, Pasi kudai ujira,
Watoto wajane wazee, kuzilinda zetu kura,
Mtatufanya tuweze, kupata kilicho bora,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Tafadhali tambueni, tumeupata mtaji,
Tunakuja uwanjani, jengo tunalihitaji,
Kura zenu ni muhimu, ili kuwa wapangaji.
Timu imekamilika, kila idara yatosha,
Slaa tumemsimika, kamwe hatotuangusha
Sera amezitamka, Mtanzania kuneemesha,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Kazunguka mikoani, sera kuelezea,
Watoto madarasani, vyuoni na chekechea
Kulipia asilani, shule bure kupatia
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Wafanyakazi kakumbuka, kilio chao cha kale
Mishahara kufutuka, kuwafanya watoto wale
Chochote wakikumbuka, mifukoni ziko hela
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Timu haijatimia,jengoni kumsindikiza
Baregu anafuatia, uzushi kuudamaza,
Mabere afuatilia, sheria kuwaeleza
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji
Zitto pia Ndesamburo, wote wanaunguruma,.
Halima pia Mbogoro, kidete wamesimama,
CCM wana Kihoro, wamuonapo Lema,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Nimtaje naye Mbowe, Mbilinyi jimbo la Mbeya,
Na anatamba Shamwee, kule Vijijini Mbeya,
Waonekanapo mayowe, Nisemacho si umbea,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Swali sasa ni lako, wewe unisomaye,
Ulanga na Makambako, Hassani, Pili, Simbeye,
Muhimu ni kura yako, wa CHADEMA umpendaye,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Kura peke haitoshi, Kuzilinda ni lazima,
Bukoba Lindi na Moshi, kura kuzitazama,
Itamaliza ubishi, itasimama CHADEMA,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.
Kwa wingi tujitokeze, Pasi kudai ujira,
Watoto wajane wazee, kuzilinda zetu kura,
Mtatufanya tuweze, kupata kilicho bora,
Kura zenu ni Muhimu, ili kuwa wapangaji.