mpimamstaafu
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 4,445
- 4,707
Kumekuwa na purukushani kubwa kipindi cha Usajili hasa kwa vilabu vyetu vikubwa Simba na Yanga iwe kwa Wachezaji au Makocha hasa wa Kigeni.Pia tumekuwa tulisikia wachezaji au Makocha wa kigeni wanasajiliwa lakini baadae wanaondoka au kusitishiwa mikataba na kutokulipwa mishahara yao na kupelekea kushtaki FIFA ili walipwe stahiki zao.Tunavishauri vilabu vya Simba na Yanga wachezaji na Makocha wazuri ni gharama hivyo wanapowahitaji ni vema wakawa na Bajeti ya Mishahara yao ya kutosha ,wasitegemee michango ya Mashabiki ndio ilipe Mishahara yao ipo siku FIFA itavifungia vilabu hivi na kuwa Aibu kwa Nchi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app