Kusema kweli Ada ya kufanyia miamala imepanda mara dufu

Na bado kila atakae chukua kadi ya kimachinga itamtokea puani
Kwa sasa hawatajitambua tena watakurupuka kweli kuchukua hizo kadi[emoji3]
Wasifkiri ni kama vitambulisho [emoji38]ukishachkua hio kadi tayari unakuwa ktk system,yaani umeshaii comit(ndoa)
Balaa lake sasa[emoji38]tutakumbushana humu humu[emoji1321]‍♂️
 
Kutuma pesa tu nayo ni matatizo, nimemtumia mtu wa Tigo from Vodacom wamenilima 1400! Nilishangaa kinoma wakati nilishazoeaga kumsogezea mtu hela ni tshs 300!

Luku ukinunua umeme wa laki 1 unakatwa elf 22 sawa umenunua umeme wa elf 78[emoji38]
Ukinunua umeme wa elf10 unakatwa elf mbili mia mbili sawa na umenunua umeme wa elf7800 unapata unit 28[emoji38]

Ukimchunguza saaana Bata huwezi kumla,wacha tusukume tu gurudumu la maisha[emoji1321]‍♂️
 
Kuna haja ya kuwa na mbadala wa hizi m-pesa na tigopesa. A new way to solve money transfer problems bila kuhusisha gharama kubwa namna hio.

System iwe inafanya kazi kwa gharama nafuu. It doesn't make sense unachukua 1,400 yangu kwa sababu ya nini hasa kikubwa maana ni kuhamisha pesatu sio kama wanaitengeneza wao. Tutaanza kutuma hela kwa mabasi sasa kama enzi za ujima.
 

Unaongelea haja ya kubadili mfumo wa mpesa
Wakati hadi wauza ndizi ktk standi za mabasi wanalizimishwa walipie elf20 vitambulisho vya kimachinga
Ije kuwa mpesa wakat hio ilishaongelewa na mkulu mwenyewe wakt akizindua CRDB Bank branch huko chato[emoji1321]‍♂️
 
Kwa kitambulisho ni sahihi wala sioni shida. Chagua kulipa Tshs.500 pamoja na maintainance fees za manispaa kwa siku 30 ndani ya mwaka mzima ama kulipa 20,000 mara moja kisha ukawa huru kufanya biashara mwaka mzima bila kero zingine.
 
Wanatuibia sana haya mabenki na makapuni ya simu......Ukitaka kutoa 1m inakulazimu utoe laki 2 mara 5 na hapo wanalima kati ya 900 hadi 1000 kwa kila transaction kwa hiyo hpo unalimwa Buku 5 Nzima.
Nimeona jana kwa CRDB WAKALA muamala wa shilingi 130,000/= ulinigharimu tozo ya shilingi 3,000/=.
 
Wanatuibia sana haya mabenki na makapuni ya simu......Ukitaka kutoa 1m inakulazimu utoe laki 2 mara 5 na hapo wanalima kati ya 900 hadi 1000 kwa kila transaction kwa hiyo hpo unalimwa Buku 5 Nzima.
Nimeona jana kwa CRDB WAKALA muamala wa shilingi 130,000/= ulinigharimu tozo ya shilingi 3,000/=.
 
Kiukweli sio tu makato ya kutuma na kutoa pesa kwenye mabank na mawakala wa simu Bali mpaka huduma za maongezi na vifurushi vya internet sio rafiki kwa maisha yetu ya sasa ......jamani hali ni tete tena tete mnoooooo huyu mzee afanye atuhurumie atafute alipokosea ajirekebishe vinginevyo hili zigo alilotubebesha kiukweli sio size yetu hii ni hatari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa kabisa naamini ktk hili maana wamejiwekea sheria zao utaona tu vigezo na masharti kuzingatiwa
 
Labda wanafidia ule upotevu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
WIZI MTUPU Kwa vile bado sie twashangailia kuwa na cmu!! badala ya kuangalia hidden costs!
Yes, wengi hatufuatilii wizi wa hizi taasisi za kifedha. Jana ndiyo nimegundua kuwa CRDB huduma zao za kutoa fedha kwa wakala "wanatupiga sana", WAKALA ukimuuliza gharama ya muamala atakwambia haizidi hata Elfu Moja, nadhani wale wanaopendekeza wawe wanahifadhi fedha zao ndani ya nyumba wako sawa kwa kutumia kigezo cha makato makubwa.
 
Mimi hua ka salary kangu kakiingia tu huko crdb nakwangua kote nakaa nazo kuepuk miamala ya Mara kwa Mara au nahamishia a tel or nmb au equity bank
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…