Kusema ukweli mabasi mengi ya shule (school bus) ni skrepa, tusisubiri hadi majanga yatokee ndio tushtuke

Kusema ukweli mabasi mengi ya shule (school bus) ni skrepa, tusisubiri hadi majanga yatokee ndio tushtuke

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
1720651268941.png

Wakuu,

Mabasi haya si mageni kwetu, baadhi yanabeba watoto wetu, wa jirani zetu na wengine watoto wetu ndio madereva kwenye magari haya, nina imani wote tutakubaliana kuwa magari haya hasa kwa hapa Dar ambako nimeshuhudia, mengi yanapumulia mashine, hayafai hata kidogo kutumiwa na na watoto wetu.

Na mbaya zaidi madereva wengi wa mabasi haya hawajali, unakuta dereva anaendesha kwa mwendokasi na ku-overtake kama mwehu, mpaka ujiuliza huyu hajui kama yuko na watoto kwenye basi?

Trafiki na polisi kwa ujumla simamieni hili, msisubiri mpaka itokee ajali ndio mje mshtuke, na neno kutaka mtaani ni kuwa madereva wengi wa mabasi hayo hawana sifa wala ujuzi wa kuendesha wanafunzi.

Mkiendela na mpango wenu wa kureact baada ya tatizo kuwa limefanyika na kisha kuzuga siku mbali tatu na kuacha utaratibu mbovu uendelee kufanyika, tutaendelea kupoteza maisha ya eatu kila siku. Polisi amkeni na kufanyia kazi suala hili, hali inazidi kuwa mbaua.

Na sisi wananchi ukikutana na school bus imechoka, wanafunzi wamejazwa kama magunia ya mkaa, dereva anaendesha rafu, tuwe wepesi kuripoti kwa mamlaka husika (askari wa barabarani au vituo vy apolisi ili hatua stahiki zihukuliewe tuepushe majanga makubwa mbeleni.

PIA SOMA
- Serikali: Hatuna mfumo wa ukaguzi wa madereva wa mabasi ya shule

- Tafsiri ya ‘School Bus’ Tanzania ni ipi? Vigezo gani vinazingatiwa ili gari litoe huduma ya kubeba wanafunzi?
 
Kuna baadhi ya shule wanatumia hadi gari binafsi za mmiliki/walimu wa shule kwenda beba wanafunzi kila uchao
Katika hili na kwa ujumla nitaanzishia uzi binafsi wamagari mabovu ya shule kwa hapa Dar hasahasa . Pia nitapokea na viswo na picha za mikoa mingineyo.
 
Hawa watu binafsi wanafanya biashara, wakijiingiza kwenye magari, biashara haitalipa, lazima watafute scrpers kukidhi hajua at the expense of children's life!
 
Kwan unafkr serikali haijui wanajua Sana sema ndo shimo Lao la marupurupu ndo maana unaona hawaongei
 
Inasikitisha sana. Tatizo binadamu wa siku hizi wabishi sana
Cc @_ephen
 
Back
Top Bottom