Kusema ukweli Zanzibar ndio ina mambo yasiyo ya Muungano na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mambo yote ni ya Muungano

Mimi nadhani njia nzuri ya kuulinda muungano wetu ni kuunda nchi moja na serikali moja (Tanzania) hapo hizi kero litakuwa zimekwisha.

USA ni muunganiko wa zaidi ya Mataifa 50 na hakuna tatizo la muungano wao sababu nchi zote zilizoungana zilikubali kupoteza uraiya wake
 
Zanzibar walipoteza uraia wao lakini wakabaki na utaifa wao!
 
Bunge ni la muungano?
Mbona Spika na Naibu wake wote wanatoka bara??
 
Yaani wewe source ya taarifa zako ni Wikipedia

Mkuu siku nyingine usitumie Wikipedia kama source ya taarifa zako maana uko taarifa inaweza kuhaririwa na mtu yeyote muda wowote
 
Yaani wewe source ya taarifa zako ni Wikipedia

Mkuu siku nyingine usitumie Wikipedia kama source ya taarifa zako maana uko taarifa inaweza kuhaririwa na mtu yeyote muda wowote
Nalijua hilo ila Mwinyi (Mzee Rukhsa), Jumbe wote sio Wazenji na Walitawala kule. Hata Karume baba si Mzenji...

Mbona zinajulikana historia hizo.
 
Uraia ni wa JAMHURI, hamna raia wa Zanzíbar n.k (ndio maana paspoti moja tu). Au ndo itakuwa ya Salim Ahmed Salim, alipokuwa OAU alikuwa Mtanzania na tulijisifu, ila alipotaka kugombea uraisi zikapikwa fitina za mwarabu, Mzanzibari n.k (historia hujirudia, na huyu mamá nahisi atakuwa kama Mwinyi alivyochukua madaraka kutoka kwa Nyerere) muda utasema.
Marekani wana majimbo na kila jimbo Lina sheria zake tofauti ,
Mengine bangi halali na mengine wanakataza na pia kuna serikali kuu ya shirikisho .....
 
Mbebano huu
 
Hata sasa Inawezekana wakiamua
 
Mbona kama ndiyo matoka usingizini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…