Rai Pazzy
JF-Expert Member
- Jul 6, 2015
- 493
- 187
Mkuu wa mkoa au waziri au authority yoyote ya serikali kuu haiwezi tunga sheria mpaka wapewe nguvu na sheria ya bunge isipokuwa raisi ambaye yeye amepewa mamlaka na katiba.Hivi jamani wadau huu usafi wa jumamosi umekuwaje? Ni kila jumamosi ama?
Leo naelekea kazini nasimamishwa kwanini huendi kwenye usafi na kweli watu wengi walikuwa wanafyeka.
Nikazozana nao kidogo ndo wakaniachia maana niliwaambia nina funguo za ofisi hivyo nitawaweka watu nje muda mrefu.
Hivi hizi sheria huwa zinapitishwa na chombo gani au mkuu wa wilaya au mkoa akijiskia tu basi anatoa tamko.
Hivi kodi zetu zinafanya nini? Asubuhi kweli nikafyeke? Sasa shule nilienda kufanya nini? Hizo kodi zetu kwanini zisilipie watu watakaofanya kazi hizo tena sasa hivi ni kila wiki.
Ukiona waziri katunga sheria ujue kuna sheria ya bunge na immempa madaraka ya kufanya hivyo.