Kusingiziwa kunauma jamani asikwambie mtu

Kusingiziwa kunauma jamani asikwambie mtu

Habari ya weekend wana Jf,.
Waswahili huwa tuna msemo mmoja eti 'ukweli unauma'... Kwamba ukiongea jambo ukaona mhusika amekasirika basi hilo jambo ni la kweli. Mimi nakataa jamani jambo la kusingiziwa linauma sana, mimi binafsi mtu akikomaa kuning'ang'aniza nimefanya kitu ambacho sijafanya naweza kumchapa makofi na kama ni mtu ambae siwezi kumpiga wala kugombezana nae huwa najikuta nalia tu.
Mimi binafsi katika kukua kwangu nimesingiziwa mengi sana ila yapo mengine hadi leo hayafutiki. Nikiwa darasa la saba kuna mtu alipeleka taarifa kwa walimu kwamba natoka na wakaka fulani hivi wawili (msishangae enzi zetu tulikuwa tunamaliza la saba tukiwa wakubwa sio kama siku hizi watoto form three ndo anavunja ungo). Ni stori ndefu ilikuwa ila habari ilikuwa ndio hiyo, tulitajwa wengi tuliokuwa tunatuhumiwa kujihusisha na mapenzi tukaitwa kwa mwalimu mkuu akawa anatupatia nasaha eti 'kuweni makini siku hizi magonjwa mengi ikibidi basi mtumie kondom' lahaulaa mimi hakuna siku nililia kama siku ile nilijiapiza aliyefanya hivyo lazima nimkomeshe japo mwisho wa siku sikumfanya chochote. Ninachomshukuru Mungu mzazi wangu alinielewa na hakuwa na nongwa na hiyo ilitosha sana kunipa amani. Cha ajabu yule mwendawazimu baada ya kuingia sekondari form one tu kafukuzwa shule kwa kashfa ileile aliyonizushia mimi nikasema malipo hapahapa duniani pambaf.
Jambo lingine ninalokumbuka nikiwa form four kuna mtu alimpelekea maneno rafiki yangu wa karibu kuwa mimi nilikaa nilisema eti yeye anatembea na mkaka mwenye UKIMWI, Nilishangaa tu yule rafiki yangu anajiweka mbali na mimi hanichangamkii wako busy tu na rafiki yetu mwingine, siku anakuja kuniambia hayo nilishangaa sana maana kwanza sikuwahi kusema, pili sinaga tabia ya kumsema mtu wangu yeyote wa karibu iwe rafiki,ndugu,mpenzi or whatever kwa watu baki, lakini baadae nilikuja kuhisi labda ametunga tu mwenyewe kwa lengo la kukata urafiki.
Lingine nikiwa mdogo kuna dada yangu mmoja alinisingizia nimemuibia mia yake aliweka mezani na mimi ni mtu pekee nilikuwepo humo ndani, alinikomalia kuwa nimeichukua akaanza kunipiga kadri ninavyokataa sijachukua ndivyo kipigo kinazidi, baadae nilipoona kipigo kimenielemea ikabidi nikubali kuwa nilichukua ila mimi pia nimeipoteza nilikokuwa ninacheza ndio kuniacha. Kesho yake asubuhi akiwa anapiga deki akaiona uvunguni mwa kitanda. Akaniita tena nikasema si unaona, mimi sikuchukua akataka kunishushia tena kipigo kwa kuogopa kipigo na fimbo za jana yake hata hazijapona nikasema niliidondosha mwenyewe baada ya kuchukua sikujua imedondokea hapo. Hili tukio huwa linaniumiza na kila nikikumbuka machozi yanadondoka ila nimepanga ipo siku nitamkumbusha mhusika najua ye kasahau.
Kama umewahi kusingiziwa tupatie kisa na wengine wajifunze.
Mbona hujaisema ile waliyokusingizia eti mimi na wewe tulikuwaga tunabanjuana kwenye shamba la mihogo unapokwenda kuchota maji ziwani au umesahahu!!!!
 
Mimi nilikuwa mkorofi tena mkorofi haswa, jeuri, ukinizingua mchana usiku lazima upite mitaa ya kwetu uchezee mawe au kipigo kama nakuweza, kuvunja vioo vya shule , kugomea waalimu , na mengine mengi ambayo nitakuja kuyajumuisha siku moja kwenye struggle to success stori yangu/zangu,.

nirudi kwenye mada ,vya kusingiziwa vingi ila hiki ndo kinaniumaga zaidi, ilikuwa ndo kipindi smartphones zimetoka , kuna sehemu me napaita safe place/zone nikipiga mtu, nkizingua skani naenda kuchill na wadau kihvyo ani , sasa kuna dogo akaiba smartphone ya mzee wa jirani na safe zone , siku hyo natoka skuli mzee huyu hapa alikuwa mshkaji wangu hatari kanambia dogo njoo nielekeze ishu fln kwenye cm sielewi , nlikuwa na miaka kumi na tano kipindi hiko, nikaenda ghafla kanikwida mtama chali anaanza kuuliza simu yangu iko wapi 😭😭 me machozi tuu, sina majibu na school uniforms zangu nachezea kipigo.
Akasema hutaki kujibu sasa utaona nitakachowafanya alikuwa na kijana wake wa kazi kanipakiza kwenye toyo hao tukaenda somewhere kunishusha wakanipeleka kwenye banda la kuku ghafla nawakuta machalii tunaokutanaga safe zone wamepigika hatari wote wamenitaja me kisa sikiwepo isipokuwa mwanangu sana Mr A popote ulipo mungu akubariki kama upo humu me ni E kaka, .

machalii kuulizwa tena wakakana wakasema siyo huyu ila isipokuwa mmoja ambaye ni sbd b , akawa anakazia me nlichukua nkamshirikisha ani hapo nalia kama my mother ndo kafa ani alafu dogo anakazia si mnaona anavyolia ukweli unauma,
nikavuliwa nguo nkapigwa shoti , me sikukubali coz sijafanya , damu puani manundu kila kona sikukubali ikafika zamu ya sbd B kupigwa shoti mbona alikubali kuwa yeye ndo kaiba simu akaenda kuitoa kwenye banda la majani dooh nlishindwa kumpiga nlikuwa hoi , granny alifanya kuja kunibeba kunipeleka hospitali , kesi ilienda ishia mahakamani
naumiaga hadi today , nlipokuwa nakuja kusalimiwa hospitali mtu akiniambia pole ndo uache kuhang na wezi machozi na uchungu kama wote , ila yule dogo hajafikaga mbali alikuja kufungwa 2 years kwa kosa la wizi na uuzaji wa bangi.

ILA MPAKA LEO HUWA NINAE KOVU LA HYO MSALA KILA NIKILIONA LAZIMA NILIE AU NIKOSE AMANI
 
Hili jambo ni uduwanzi kweli yaani mtu sijui anapata faida gani kukusingizia yaani nina visa vingi vya kesi ya kusingiziwa
 
Back
Top Bottom