Kusoma Kiingereza muda mrefu bila kukimudu sawa sawa tatizo ni nini?

Kusoma Kiingereza muda mrefu bila kukimudu sawa sawa tatizo ni nini?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kusoma lugha mfano Kingereza kwa miaka 10 bila kuimudu lugha yenyewe vizuri inadhihirisha uduni wa wa mfumo wa elimu, attitude mbovu au IQ ndogo za wasomaji?

Screenshot_20241122-165129_X.jpg
 
Tatizo ni mfumo wa elimu na jamii inayotuzunguka.mfano Tanzania unafundishwa kiingereza na mwalimu ambaye hakijui vizuri na anakufundisha Kwa kiswahili halafu ukifika nyumbani unapiga kilugha na kiswahili mwanzo mwisho.Hapo lazima ze ze ze ziwe nyingi.
 
Mwalimu anayekufundisha sio fluent. Wewe mwenyewe ukitoka mazingira ya shule unakiweka kapuni. Ukiangalia movie basi mpaka iwe imetafasiriwa. Husomi (hasa novel). Nyimbo unazosikiliza sio za kiingereza hata ukisikiliza basi ni kwa ajili ya Melody na beat. Kinachoimbwa huzingatii. Mwisho kabisa, umeridhika.
 
Kitu chochote ukijifunza bila kupractice huwezi kukimudu. Ndio kingereza kinafundishwa ila kinaachwa darasani , wanafunzi wakiwa hata nje ya darasa hawakitumii.
Nafuu Iko kwa wale wa English Medium... Hao angalau Wana practice.....
 
1. Tatizo kinafundishwa kwa kiswahili.
2. Wengi wetu tunawaza kwa kiswahili na kuzungumza/andika kiingereza.
3. Kuna "common mistakes" za kutamka maneno, muundo wa sentensi kama hii "Juma he is at home", "Did you went to school yesterday" hazifanyiwi kazi na walimu wetu.
 
Kitu chochote ukijifunza bila kupractice huwezi kukimudu. Ndio kingereza kinafundishwa ila kinaachwa darasani , wanafunzu wakiwa hata nje ya darasa hawakitumii.
Nafuu Iko kwa wale wa English Medium... Hao angalau Wana practice.....
Mfano mzuri wazungu wakija Tanzania ukiwaongelesha kwa kimombo wao wanajibu kwa kiswahili ili wajifunze kiswahili
 
Back
Top Bottom