Kusoma nje ya Nchi, Is it worth it?

Mkuu unapataje zile TOEFL na IOLETS??
 
Aisee nashukuru, nataka nikasome kule huku napiga vibarua, hasa ulaya
 
Kwa mtu aliyesoma degree ya kwanza SAUT then masters Mzumbe evening class.

Huyu exposure yake si inatia huruma sana.
 
Sijasoma nje ila watu wote niliokutana nao waliosoma nje huwa wanakuwa na kitu cha ziada ambacho naona kabisa tofauti kifikra, mtazamo na utendaji,
Miaka miwili sasa baada ya kumaliza degree yangu, nafanya kazi nipate experience ndogo ya kujaza CV niombe scholarship Ulaya au USA, waliosoma Asia huwa hawafanani na waliosoma hizi sehemu mbili kwa utafiti wangu mdogo niliofanya.

Naomba hints kdg
 
Uko sahihi kabisa!

Mfano, hata kwa Wamarekani ambao wamesoma nje walau semester moja au mwaka mmoja, huwa wana kitu cha ziada ambacho wale ambao hawajatoka nje ya nchi, hawana.
 
Mimi naamini nilifelishwa na system ya elimu ya bongo japo nilikuwa napenda sana elimu hasa sayansi..
Baada ya hapo nikachukia elimu na nikaichukia nchi pia...

Nikaanza mchakato wa kuondoka bongo kabisa, miaka ile ndio makampuni ya mining yanaanza kuingia bongo, Nikaenda maporini huko Kahama, na kufanikiwa kupata kazi ya kutumia nguvu, bahati ilikuwa inalipa vizuri.

Nikajichanga na kupata nauli yangu ambayo lengo lilikuwa ni ya kutoka nje ya bongo, iwe nchi yoyote ya hata kama ni ulaya choka mbovu lakini lengo langu ni kufika kwa Bi Mkubwa....

Nikapata bahati ya viza ya Spain, nikatumbukia na kupotelea ndani, nikapita border kwa border mpaka Holland,
Napo sikukaa sana nikaweza kumlipa mtu akanifikisha kwa Bi Mkubwa.

Maisha yakaanza hapo, nikiwa mbeba box, nikapiga box kama miaka kadhaa, nikachoka, nikasema hapana, mimi nina uwezo wa kiakili nikiamua kusoma.

Safari ikaanza, nikajiunga foudation year ya college ya Electrical/Electronic engineering kwa mapenzi yangu ya elimu ya sayansi ili niweze kuingia University, nikapasua kwa Distinction...
Nikaanza chuo , sikusimama nikapitiliza mpaka Masters.

Sasa huwa najiuliza, ningebaki bongo, maana yake hatima ndio ingekuwa imeishia hapo....
Hapa ndio nikajua tofauti ya elimu ya tia maji na elimu za wenzetu hasa nchi za Ulaya.
Huku mtu akiamua kusoma, unasoma chochote unachotaka kama una uwezo wa kiakili kukimudu, hakuna mambo ya sijui, wewe ulisomea huu mchepuo kwahiyo hii kozi unayotaka huwezi kusoma, ni ujinga mtupu wa elimu ya kibongo.

Ninapofanya kazi, kuna mmoja ambaye ni kati ya executives, amesoma digrii ya Finance, Master ya Engineering Management, na sasa ana Phd ya Medical Physics........
 
Duuuh hongera sana mkuu
 
Changamoto sana
 
Elimu na kuelimika. sasa tunamtambuaje aliyesoma akapata elimu na kuelimika.

Elimu ni uwezo wa kuongea na kuandika lugha za kigeni au kufanya kazi za taaluma ngumu, kama vile A.I, au kuwa na uwezo kutoa matokeo mazuri ya kazi uifanyayo?

Nini kinafanya tuseme fulani kaelimika, ni busara, muonekano, chuo alichosoma, au kozi aliyosoma, au ubora wa chuo na elimu?, na ubora tunaupimaje?
 
Waliosoma Asia hawafanani na wapi mkuu?
 
Madini sanaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…