We Barbarosa acha uchuro kama huwezi kujenga hoja za msingi.
Mosi wanasheria hawajiiti wanasheria ila ni wanasheria kweli.
Mbili, sheria siyo za Uingereza tu ambazo waafrika wanasomea.
Hii inayoita sheria ya Uingereza ni mfumo unaoitwa Common Law Legal system ambayo inatumiwa na nchi zote zilizotawaliwa na Mwingeza, siyo nchi za Africa tu bali hata za mabara mengine.
Pia kuna mfumo mwingine unaoitwa Civil Law legal system ambao ni mfumo wa sheria wa nchi has za continental Europe na hata baadhi ya nchi za Asia na Latin Amerika. Na nchi nyingi za Kiarabu wanao mfumo wao wa sheria. Je wewe ulitaka tuwe na mfumo upi?