Uchaguzi 2020 Kutangaza maandamano pekee hakutoshi, kunahitaji maandalizi. Tujiulize kwanini maandamano ya Seif Zanzibar hayakufanikiwa

Uchaguzi 2020 Kutangaza maandamano pekee hakutoshi, kunahitaji maandalizi. Tujiulize kwanini maandamano ya Seif Zanzibar hayakufanikiwa

Kama haupo nchini rudi uyaone. Na kama upo nchini utakuwa ushajionea mwenyewe. Usinipotezee muda kuyarudia. Soma hata humu JF Kuna threads kibao zimeyaeleza.
Hakuna pahala panaonesha dhuluma bali watu wana lalama tuu
 
Kuandaa maandamano ni fani kunahitaji mipango madhubuti, hata kama una ajenda muhimu huwezi kukurupuka na kutangaza leo au kesho kuna maandamano, Seif alikuwa na ajenda lakini hakuwa na mipango madhubuti aliongozwa na mihemuko, hasira na jazba.

Wataalamu wa mipango ya maandamano wanasema ili maandamano yafanikiwe kuna hatua muhimu lazima zizingatiwe.

  1. Lazima kuwe na sababu (issue) inayogusa jamii. Unaweza kutangaza maandamano ukakuta watu hawana interest nayo.
  2. Chagua ‘theme’ kauli mbiu itakayokuwa common kwa wote itakayotoa hamasa mfano, uonevu sasa basi au wimbo wa ujasiri.
  3. Toa taarifa kwa taasisi za misaada kama Red Cross na andaa utaratibu wa misaada ya haraka kwa waandamanaji watakaozidiwa wakati wa maandamano mfano maji na huduma ya kwanza.
  4. Tayarisha eneo mwafaka destination la kutolea matamko yako (open space, ofisi za serikali, nk) usitoe matamko ofisini kwako.
  5. Alika ‘known public speakers’ watakaotoa hotuba fupi fupi zisizochosha mfano viongozi wa dini, wasanii nk.
  6. Andaa mziki na wasanii watakaoburudisha.
  7. Andaa shelters mahema, jukwaa kama kuna ulazima.
  8. Andaa mabango yenye kuvutia na kufikisha ujumbe mfupi (inclusive) usibague kundi lolote la jamii.
  9. Kama lazima pata vibali au toa taarifa kwa mamlaka husika.
  10. Alika vyombo vya habari vya ndani na vya nje ikiwezekana vipe taarifa mapema kwa simu ama maandishi, email nk.
  11. Tumia mitandao ya kijamii kama Twitter, Facebook, Instagram, You Tube nk kuhamasisha watu.
  12. Ijulishe jamii ya kimataifa, mashirika ya haki za binadamu na marafiki kusudio lako la kufanya maandamano ya amani ukinukuu vifungu vya sheria vinavyo kusapoti.
  13. Mwisho kabisa hakikisha wafuasi na waandamanaji hawavunji sheria wala kufanya fujo.

HATURUHUSU MAANDAMANO
 
Waandamanaji hapa kwetu Tz walio na nia ama uwezo wa kuacha shughuri zao kwa ajili ya maabdamano ni wachache mno,
Unaweza kujitoa kuandamana ukajikuta upo na watu wasiofika mia.
Haya ni mazungumzo yatakayoishia hapahapa,
Na mambo mengine yataendelea kama siku zote.
 
Hapa sioni maandamano yakitokea,
Uchaguzi umeisha na maisha yataendelea kama kawaida!
Lakini pia ieleweke wanaohitaji maandamano ni wachache kuliko wasioyahitaji!
 
Watanzania waishio nje ya nchi (TANZANIA DIASPORA) wameanza kuandamana kupinga UCHAFUZI uliofanyika juzi hapo nyumbani Tanzania!

Hawa ni ndugu zetu kutoka Ulaya ya Kaskazini (Sweden 🇸🇪, Norway 🇳🇴 na Denmark 🇩🇰) ambao tayari wameanza maandamano yao nje ya Ubalozi wetu uliopo Stockholm, Sweden...

Watanzania waishio nchini Ufaransa 🇫🇷 wanaandaa maandamano hayo kesho Jumatatu, November 2, 2020 nje ya Ubalozi wa Tanzania 🇹🇿 nchini Ufaransa 🇫🇷.

Maandamano yataanza saa 2 asubuhi na kumalizika saa 6 mchana!

Baada ya maandamano, WAZANZIBARI waishio nchini hapa, kwa kuongozwa na Balozi wetu (BABU MZANZIBARI), watazindua Ubalozi wetu (Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar nchini Ufaransa)... Ofisi za Ubalozi wetu zipo mitaa ya TROCADÉRO, karibu sana na mnara wa EIFFEL...

Kwa niaba ya Wazanzibari wote waishio nchini hapa Ufaransa, mimi, BABU MZANZIBARI, Balozi wa Zanzibar nchini Ufaransa, natumia fursa hii kuwakaribisha ndugu zetu Watanzania waishio nchini hapa, katika uzinduzi wa Ubalozi wetu!

Usafiri, kula, kunywa ni kwa gharama yangu mwenyewe!...

Kwa kauli moja, tumekubaliana kuwa hatuitambui serikali haramu ya John Pombe Joseph Magufuli! Hatuitambui serikali haramu ya Hussein Ali Hassan Mwinyi!

Rais wa Zanzibar tunayemtambua ni Maalim Seif Sharif Hamad aliyechaguliwa na wananchi wa Zanzibar!... Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunayemtambua ni Tundu Antipas Lissu, aliyechaguliwa na Watanzania!...

Mungu ibariki Zanzibar yenye mamlaka kamili, Mungu ibariki Tanzania!... 🙏🏾

👉🏾👉🏾👉🏾 Sambaza ujumbe huu umfikie kila Mtanzania mpenda haki!...👍🏾
 
Watanzania waishio nje ya nchi (TANZANIA DIASPORA) wameanza kuandamana kupinga UCHAFUZI uliofanyika juzi hapo nyumbani Tanzania!

Hawa ni ndugu zetu kutoka Ulaya ya Kaskazini (Sweden 🇸🇪, Norway 🇳🇴 na Denmark 🇩🇰) ambao tayari wameanza maandamano yao nje ya Ubalozi wetu uliopo Stockholm, Sweden...

Watanzania waishio nchini Ufaransa 🇫🇷 wanaandaa maandamano hayo kesho Jumatatu, November 2, 2020 nje ya Ubalozi wa Tanzania 🇹🇿 nchini Ufaransa 🇫🇷.

Maandamano yataanza saa 2 asubuhi na kumalizika saa 6 mchana!

Baada ya maandamano, WAZANZIBARI tuishio nchini hapa, kwa kuongozwa na Balozi wetu (BABU MZANZIBARI), tutazindua Ubalozi wetu (Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar nchini Ufaransa)... Ofisi za Ubalozi wetu zipo mitaa ya TROCADÉRO, karibu sana na mnara wa EIFFEL...

Kwa niaba ya Wazanzibari wote waishio nchini hapa Ufaransa, mimi, BABU MZANZIBARI, Balozi wa Zanzibar nchini Ufaransa, natumia fursa hii kuwakaribisha ndugu zetu Watanzania waishio nchini hapa, katika uzinduzi wa Ubalozi wetu!

Usafiri, kula, kunywa ni kwa gharama yangu mwenyewe!...

Kwa kauli moja, tumekubaliana kuwa hatuitambui serikali haramu ya John Pombe Joseph Magufuli! Hatuitambui serikali haramu ya Hussein Ali Hassan Mwinyi!

Rais wa Zanzibar tunayemtambua ni Maalim Seif Sharif Hamad aliyechaguliwa na wananchi wa Zanzibar!... Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunayemtambua ni Tundu Antipas Lissu, aliyechaguliwa na Watanzania!...

Mungu ibariki Zanzibar yenye mamlaka kamili, Mungu ibariki Tanzania!... 🙏🏾

👉🏾👉🏾👉🏾 Sambaza ujumbe huu umfikie kila Mtanzania mpenda haki!...👍🏾
Hahah!


Endelea kujidanganya
 
Hivi ninyi wapinzani akili huwa mnaweka wapi?Maana tayari kitendo cha ccm kujikuta wako wao peke yao,kimewafanya waanze kufedheheka.Hawana furaha kamwe.Tunaishi nao na tunawasikia.
Maana ushindi wao sio dhidi ya wapinzani,ila ni dhidi ya Tanzania.
Akili za kuku hizi..!!!
 
Kuandamana ni mbinu ya kipuuzi sana kutumika hapa kwetu.

Kwanza hakuna mtu anayeona aibu kuona anapingwa kwa njia ya maandamano.Pili kuna watu watauwawa,wataumizwa na kuwa vilema wa maisha,na wengine kufungwa na bado hakuna hata mtu mmoja mwenye uwezo atakayechukua hatua za kutetea watu hao.

Mambo haya ndiyo yanasababisha hawa waoinzani waonekane hawana maana.Maana njia hii ni kama kuwapa nafasi ccm ya kufurahia walichokifanya.Mnataka tu muwape maneno ya kuongea huko bungeni huku mkizodolewa.

Hivi ninyi wapinzani akili huwa mnaweka wapi?Maana tayari kitendo cha ccm kujikuta wako wao peke yao,kimewafanya waanze kufedheheka.Hawana furaha kamwe.Tunaishi nao na tunawasikia.
Maana ushindi wao sio dhidi ya wapinzani,ila ni dhidi ya Tanzania.

Kwa nini msikae kimya kwanza kuliko kuanzisha mapambano sasa?
Sisi huku Zanzibar tumechoka maandamano yasio na tija
tunaomba tuletewe silaha tupambane na hawa wanajeshi wa Burundi
tumechoka kona damu zetu zinamwagika

Kuna maelfu ya vijana wapo tayari kupambana mpaka wafe
 
Kama haupo nchini rudi uyaone. Na kama upo nchini utakuwa ushajionea mwenyewe. Usinipotezee muda kuyarudia. Soma hata humu JF Kuna threads kibao zimeyaeleza.
Pamoja na hayo yote je,huko mitaani kwa raia hali ikoje kwamba watu wana hasira au wako bize na mambo yao?
 
Hakuna jeshi la Burundi wala nn Burundi hawawez kutoa wana jeshi wake wakat wao mwenyewe wako hatarini jirani zao kongo kila uchao mambo hovyo na kumbuka wamepakana na majimbo ambayo hayako salama so lazma watie nguvu kulinda maeneo yao
Lugha zao mbona ni za kiswahili cha kifaransa?
 
Hamna na wala uwezo wa kumpinga Rais mteule. Kesho rasmi anaapishwa na viongozi wenu wajiandae
Kesho!!!
Hivi unafanya nn humu mtu mjinga kama wewe? JF siku hizi imejaa watu ambao ni less informed kama wewe?? Kesho anaapishwa yule mkuu wa mkoa kule visiwani.
 
Back
Top Bottom