Kutembelea, kulia kwenye kaburi la ndugu kuna ubaya?

Kutembelea, kulia kwenye kaburi la ndugu kuna ubaya?

flulanga

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2016
Posts
4,860
Reaction score
6,390
Jana nikiwa kazini nikawaza 'Nina siku sijaenda kumsalimia bibi, sijui lini niende' Duh aisee nikakumbuka alishafariki mwaka huu miezi yamwanzoni kabisa.

Bibi yangu alinipenda sana nayeye ndie kwa asilimia kubwa alinilea. Jana hiyo nilijikuta machozi yananitiririka kazini maana nilimkumbuka. Nilikuwa nikikaa kimya bila yakwenda kumuona basi alipita kazini kwangu kuniulizia na kunijulia hali kwa madai kuwa kwenye simu haitoshi . Ila leo hii simuoni ndugu yangu yoyote anayenikumbuka hata kwa simu.

Ndugu akinipigia simu basi ujue ananitolea shida fulani. Toka bibi yangu afariki sijaona ndugu mwingine wakuja kuniulizia kazini. Hakika bibi yangu ulinipenda sanaaa....

Nilimzoea bibi yangu maana nilikuwa hata nikipata changamoto yoyote iwe kiafya au kikazi hata kimahusiano basi nilifunga safari kwenda kumueleza na hakika alikuwa ananipa nguvu sana, alikuwa ananiliwaza sana na kuniombea.

Jana hiyo kiukweli nilifunga safari mpaka makaburini nikapiga goti nakuomba huku machozi yakinitoka. Yaani nilijikuta nikilia sana juu ya kaburi nikiwa peke angu. Sijui kama huko alipo aliniona ila ipo hivyo. Upendo wa bibi juu yangu ni zaidi ya upendo wababa hakika.

Nakumbuka kuna kipindi niliitwa nyumbani kwamadai eti nimetafutiwa mchumba kitu ambacho sikukubaliana nacho ila bibi yangu alisimama upande wangu na kunitetea huku akifoka kuwa nisilazimishwe kitu ambacho sikubaliani nacho na hakika walimuelewa. Hakika bibi ulinipenda sana.

Sikuwahi kusikia wala kuhadithiwa kuwa ulishawahi nisema vibaya au kuniteta. Aisee bibi ulinipenda sanaaaa kuliko mimi nilivyokupenda.

Kuna kipindi nilipitia magumu fulani ila yale magumu yalikuwa kama yakwako maana ulipata mawazo sana nahata watu walikuwa wakikuuliza nini tatizo basi uliwajibu 'unamuomba sana Mungu mjukuu wangu flulanga awe na maisha mazuri yenye amani yeye na familia yake' ndicho ulichowajibu hicho. Pumzika kwa amani bibi yangu mpendwa.

Mimi kwenda kaburini nakulia machozi, naweza kuwa nilifanya makosa au naweza kuwa nimekufuru?
 
U got me into tears either[emoji26]
Apumzike kwa Amani bibi.
Mwenyezi Mungu akawe faraja kwako na akuletee zaidi ya bibi. Yeye ni baba wa Yatima. Ukiweza hata kujigaragaza just do it. Usiwaze mara mbili.
 
U got me into tears either[emoji26]
Apumzike kwa Amani bibi.
Mwenyezi Mungu akawe faraja kwako na akuletee zaidi ya bibi. Yeye ni baba wa Yatima. Ukiweza hata kujigaragaza just do it. Usiwaze mara mbili.
Aminaaa
 
Nimejifunza kitu.. mama yangu hinipigia simu Mara nyingi kuliko watu woote .. sometime nachoma eti Ni usumbufu.. mungu anisamehe..
Asubuhi huniambia umeamkaje mwanangu?
Mchana haachi kunisalimia
Lakini Ni Mara chache Sana nimewahi kumtangulia mama kupiga simu kumsalimia..
Narudi ngoja nimpigie kwanza
 
Nimejifunza kitu.. mama yangu hinipigia simu Mara nyingi kuliko watu woote .. sometime nachoma eti Ni usumbufu.. mungu anisamehe..
Asubuhi huniambia umeamkaje mwanangu?
Mchana haachi kunisalimia
Lakini Ni Mara chache Sana nimewahi kumtangulia mama kupiga simu kumsalimia..
Narudi ngoja nimpigie kwanza
Mkuu thamini sana hicho kitu anachofanya mama.
Me pia nilikuwa namshangaa sana bibi yangu alipokuwa ananifata kazini ila kwasaaa ndio nimegundua kuwa kumbe nilikuwa ndani yamoyo wake dhahiri kabisa.

Jitahidi nawewe pia kuwa wakwanza kumpigia simu bimkubwa.
 
Jana nikiwa kazini nikawaza 'Nina siku sijaenda kumsalimia bibi, sijui lini niende' Duh aisee nikakumbuka alishafariki mwaka huu miezi yamwanzoni kabisa.

Bibi yangu alinipenda sana nayeye ndie kwa asilimia kubwa alinilea. Jana hiyo nilijikuta machozi yananitiririka kazini maana nilimkumbuka. Nilikuwa nikikaa kimya bila yakwenda kumuona basi alipita kazini kwangu kuniulizia na kunijulia hali kwa madai kuwa kwenye simu haitoshi . Ila leo hii simuoni ndugu yangu yoyote anayenikumbuka hata kwa simu.

Ndugu akinipigia simu basi ujue ananitolea shida fulani. Toka bibi yangu afariki sijaona ndugu mwingine wakuja kuniulizia kazini. Hakika bibi yangu ulinipenda sanaaa....

Nilimzoea bibi yangu maana nilikuwa hata nikipata changamoto yoyote iwe kiafya au kikazi hata kimahusiano basi nilifunga safari kwenda kumueleza na hakika alikuwa ananipa nguvu sana, alikuwa ananiliwaza sana na kuniombea.

Jana hiyo kiukweli nilifunga safari mpaka makaburini nikapiga goti nakuomba huku machozi yakinitoka. Yaani nilijikuta nikilia sana juu ya kaburi nikiwa peke angu. Sijui kama huko alipo aliniona ila ipo hivyo. Upendo wa bibi juu yangu ni zaidi ya upendo wababa hakika.

Nakumbuka kuna kipindi niliitwa nyumbani kwamadai eti nimetafutiwa mchumba kitu ambacho sikukubaliana nacho ila bibi yangu alisimama upande wangu na kunitetea huku akifoka kuwa nisilazimishwe kitu ambacho sikubaliani nacho na hakika walimuelewa. Hakika bibi ulinipenda sana.

Sikuwahi kusikia wala kuhadithiwa kuwa ulishawahi nisema vibaya au kuniteta. Aisee bibi ulinipenda sanaaaa kuliko mimi nilivyokupenda.

Kuna kipindi nilipitia magumu fulani ila yale magumu yalikuwa kama yakwako maana ulipata mawazo sana nahata watu walikuwa wakikuuliza nini tatizo basi uliwajibu 'unamuomba sana Mungu mjukuu wangu flulanga awe na maisha mazuri yenye amani yeye na familia yake' ndicho ulichowajibu hicho. Pumzika kwa amani bibi yangu mpendwa.

Mimi kwenda kaburini nakulia machozi, naweza kuwa nilifanya makosa au naweza kuwa nimekufuru?
Pole sana, sio rahisi kumsahau mpendwa wako aliefariki katika kipindi kifupi namna hii, na inaweza ikawa your entire life kila.ukikumbuka unapata machozi

Kwenda katika kaburi ni sehemu ya healing ya maumivu na uchungu wa kuondokewa na ni jambo zuri kwa sababu ni kumthamini huyo alieondoka

Kuhusu imani, sisi wakristo kila December huwa tunasafisha na kuweka maua kwenye makaburi ya wapendwa wetu,nadhani ni jambo ambalo kiimani pia linakubalika

Mungu akutie nguvu, bibi aendelee kuwa pema peponi
 
Pole sana, sio rahisi kumsahau mpendwa wako aliefariki katika kipindi kifupi namna hii, na inaweza ikawa your entire life kila.ukikumbuka unapata machozi

Kwenda katika kaburi ni sehemu ya healing ya maumivu na uchungu wa kuondokewa na ni jambo zuri kwa sababu ni kumthamini huyo alieondoka

Kuhusu imani, sisi wakristo kila December huwa tunasafisha na kuweka maua kwenye makaburi ya wapendwa wetu,nadhani ni jambo ambalo kiimani pia linakubalika

Mungu akutie nguvu, bibi aendelee kuwa pema peponi
Aminaa
 
Mkuu pole sana, mamaangu amefariki kama miaka mi3 sasa, alikuwa rafiki yangu mkubwa, alikuwa baba, babu, shangazi, bibi, mjukuu, alinipenda sana na kunijali, siku 1, nilimkumbuka SANA, kwakweli nilienda kaburini nikakaa juu, nikalala pale ilikuwa jioni tulivu, nikakumbuka mengi, nikalia sana!

Waliokuwa wakipita naamini walifikiri nawanga! 😅 Ila nilipotoka maumivu ya rohoni yalipungua, msiba wake sikuweza kumlilia si unajua mambo ya kujikaza!

Nenda psychologically itakusaidia.

Everyday is Saturday................................😎
 
Mkuu pole sana, mamaangu amefariki kama miaka mi3 sasa, alikuwa rafiki yangu mkubwa, alikuwa baba, babu, shangazi, bibi, mjukuu, alinipenda sana na kunijali, siku 1, nilimkumbuka SANA, kwakweli nilienda kaburini nikakaa juu, nikalala pale ilikuwa jioni tulivu, nikakumbuka mengi, nikalia sana!

Waliokuwa wakipita naamini walifikiri nawanga! [emoji28] Ila nilipotoka maumivu ya rohoni yalipungua, msiba wake sikuweza kumlilia si unajua mambo ya kujikaza!

Nenda psychologically itakusaidia.

Everyday is Saturday................................[emoji41]
Pole sana mkuu. Me pia bibi yangu huwa namkumbuka sana kwa matendo yake mema kwangu hakika sidhani kama atatokea kama yeye
 
The best Uzi,,, toka nimefiwa na wanangu wawili na baba yangu mzazi makaburi ni part ya maisha yangu yaaani nikihisi upweke huzuni muda wowote basi nnaenda zangu juu ya kaburi nalia naongea mpka kifua kinasinyaa na nikijihisi kulala nalala mpk nachoka then taratibu natoka nikiwa fresh kabisa

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom