Kuteswa kwa Kibanda: Ridhiwani na Nape matatani!

Tuwaombee msamaha wale wote wanaotoa kauli za kejeli katika matukio mazito kama haya, Tunaomba jamii iwasamehe bure kwa kuwa pengine wengine ni utoto na wengine ni woga wa ki-siasa. Hii ni kwa kuwa "SIASA NI VITA PASIPO UMWAGAJI DAMU, NA VITA NI SIASA YA UMWAGAJI DAMU" ingawa wakati mwingine hata siasa huingiza element za umwagaji damu.
"TUSAMEHEANE TUNAPOPOTOKA KATIKA USEMI" Igawa heri kujikwaa kidole kuliko kujikwaa ulimi. "HAWA WAMEJIKWAA ULIMI"
 
Gazeti la kufungia maandazi hata sisumbui akili yangu
 
Ahaa vyombo vya habari vya tanzania aibu sana,mtu aliye jiandikisha kwa jin lariziwani kikwete ,ha kumbe ni mtu aliyejiandikisha na siyo muhusika mwenye jina,sasa shida iko wapi kumbe ni mtu anaye jiita jina la mtu mwingine.
 

Nime sign in kwa ajili ya kukupa like tu mkuu nilikuwa napita kama visitor. Umeongea points na ukweli ambao Thatha alijaribu kuuficha eti "si unajua mambo ya vijana?" Nashawishika kuamini kuwa maadui wa EL wana mkono wao katika hii kitu ndio maana wale waliotoa tamko kuwa rais ajaye hawezi kutoka kaskazini ndio wamekuwa wa kwanza kutaka kuaminisha uma kuwa mwajiri wake wa zamani amehusika kwa visasi, wanatakiwa wajue kuwa You can fool some people some time but not all people all the time.
 
Afisa Mtendaji mkuu wa New habari corparation,kampuni inayomiliki gazeti la Mtanzania ambalo bwana Absalom Kibanda ndie mhariri mkuu wa gazeti hilo ametoa maneno makali kwa mtoto wa raisi Ridhiwan Kikwete kufuatia kauli ya kejeli aliyoitoa mtoto huyo wa raisi katika ukurasa wake wa facebook juu ya kutekwa,kupigwa na kujeruhiwa kwa mwenyekiti wa jukwaa la wahariri bwana Absalom Kibanda.

Katika ukurasa wake wa facebook Ridhiwani aliandika:"Je,hii nayo ni kazi ya Rama?"Rama Ighondu mtumishi wa Ikulu ndie alietajwa na gazeti la mwanahalisi kuhusika katika kumteka na kumtesa Dr.Ulimboka.

Kauli hiyo ya Ridhiwan ndio imeibua kauli tata ya Bashe ambayo ni "Nakuonya iwe mwanza na mwisho,usilete kebehi katika jambo hili.Nakuonya,nakuonya,nakuonya usijaribu!tumekaa kimya....".

Sasa wadau inabidi tutafakari na kuhoji maneno haya ya Hussein Bashe "....nakuonya,nakuonya,nakuonya,usijaribu! tumekaa kimya".Hapa swali ni wamekaa kimya kwa kipi?

Penye ukweli uongo hujitenga!
 
Yeyote anayehubiri amani na awe wa kwanza kutoa haki kwa usawa vinginevyo amani itabaki kwenye maandishi. Haya yanayoendelea ni mizizi ya fujo na upotevu wa amani.
 
fbi wasubiri kidogo hawa jamaa wakichokonoana kama hivi twaweza pata majibu kwa zero cost
 
Totally forgoten that oned day they will all come where they previously belonged. Bashe amekasirishwa tu nakauli za hawa watoto wa Ikulu labda anacho anachokijua kuhusu hilo. Pole sana Kibanda.
 
Sasa wadau inabidi tutafakari na kuhoji maneno haya ya Hussein Bashe "....nakuonya,nakuonya,nakuonya,usijaribu! tumekaa kimya".Hapa swali ni wamekaa kimya kwa kipi?

Penye ukweli uongo hujitenga!

Inaonyesha jinsi Bashe alivyo kasirika juu ya utani huo
 
Hivi Riz nae anategemea baadae apew nafasi ya kugombea kama Uhuru. ? Kauli zake utadhani kiongozi wa nchi
 
Wamekaa kimya lakini ukweli wanaujua, he he heee!
 
Jambo hilo liko kwenye mchakato wa kipolisi na bado uchunguzi wake ni endelevu... nadhani ndiyo sababu kijana ameonywa akae mbali na suala hilo.
Kauli za Ridhwan zinaweza kuathiri kazi ya polisi.
 
ameelezea kilichopo moyoni, kuna mengi hatuyajui so lets wait and see
 
Mkuu nashukuru kwa kunipa 'like', lakini ukweli ni kwamba tunafahamu au nayafahamu mengi zaidi ya ninayoandika hapa, lakini mara nyingi nahofia 'BAN' na usalama wangu. JamiiForums si mahali ambapo waweza andika kila kitu unachokijua, nashukuru Mungu nimeligundua mapema hilo. Baada ya 'mzee' wangu kufariki nilipata makaratasi na barua za rafiki yake ambaye alikuwa balozi wa TZ katika nchi fulani zilizoelezea vitisho vya kifo kwa huyo balozi, na kwamba anawarudisha nyumbani watoto wake ili wasije wakapatwa na maswahiba huko ughaibuni na nzee ajitahidi kuangalia usalama wao. Mzee wangu na huyo balozi wote walifariki mwaka huo huo, yale makaratasi ulitokea wizi na kuibiwa. Mkuu, mambo ni mazito kuliko wengi tunavyofikiria.
 
Kikwete na familia yake ni hatari kubwa kwa mustakabali wa taifa letu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…