John Magongwe
Member
- Jan 4, 2024
- 71
- 119
Kutoa na Kupokea
Biblia inasema nini kuhusu kutoa
Biblia inatutia moyo kutoa kwa hiari na kwa nia nzuri. Inaonesha kwamba kutoa kwa njia hiyo kunamnufaisha anayepokea na anayetoa pia. (Methali 11:25; Luka 6:38). Yesu mwenyewe alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea” (Matendo 20:35). Ukitoa utasababisha aliyepokea amshukuru Mungu na jambo hilo kukuongezea kitu wewe mtoaji maana wewe ndiye chanzo cha shukrani hiyo. Utoaji wako utakupa sifa na heshima.
Ni wakati gani ambapo Mungu anafurahi tunapotoa
Mungu anafurahi tunapotoa kwa hiari. Biblia inasema hivi: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si bila kutaka wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu” (2Wakorintho 9:7).
Kutoa kwa hiari ni “namna ya dini” ambayo Mungu anakubali. (Yakobo 1:27). Mtu anayewasaidia wengine kwa ukarimu anafanya kazi pamoja na Mungu, ambaye anaona ukarimu huo kuwa mkopo kwake (Methali 19:17). Biblia inafundisha kuwa Mungu atamlipa yule anayetoa (Luka 14:12-14).
Ni wakati gani ambapo Mungu hafurahi tunapotoa
Hii hutokea tunapotoa kwa nia mbaya. Hii ni kama vile:
Ili tulipwe kwa njia fulani (Luka 14:12-14).
Tunapolenga kupata kusifiwa na watu (Mathayo 6:2).
Tunapojaribu kununua wokovu (Zaburi 49:6-7).
Wakati ambapo kutoa kunaingilia majukumu tuliyopewa na Mungu. Biblia inafundisha kuwa vichwa vya familia wanapaswa kuandaa mahitaji ya familia zao (1Timotheo 5:8). Si jambo linalofaa kwa kichwa cha familia kuwapa wengine kupita kiasi, hivi kwamba familia yake inateseka. Vivyo hivyo, Yesu aliwashutumu wale waliokataa kuwaandalia wazazi wao waliozeeka kwa kudai kwamba mali zao zote zilikuwa “zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu” (Marko 7:9-13).
Ikiwa zawadi yetu itatumiwa kuunga mkono utendaji na mitazamo ambayo Mungu anashutumu. Yaani, lingekuwa kosa kumpa mtu fedha kwa ajili ya kucheza kamari au kutumia kileo vibaya au dawa za kulevya (1Wakorintho 6:9-10; 2Wakorintho 7:1). Vivyo hivyo, si sawa kumpa fedha mtu ambaye anaweza kujitegemea lakini anakataa kufanya kazi (2Wathesalonike 3:8-10).
Maandiko mengine kuhusu kutoa
Methali 11:25: “Mtu mkarimu atapata ufanisi, na yule anayewaburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa”. Hii ni kwa sababu kutoa humnufaisha anayepokea na anayetoa.
Methali 19:17: “Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, naye Atamlipa kwa anayotenda”. Sababu ni kuwa Mungu anaona kwamba ana deni kwa wale wanaowasaidia wenye uhitaji, na anaahidi kuwalipa kwa ukarimu wao.
Mathayo 6:2: “Unapotoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki, ili wasifiwe na watu”. Hii ni kwa sababu hatupaswi kutoa ili watu watutambue. Hii ni kutafuta sifa na kujikweza.
Matendo 20:35: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea”. Ni kwa vile ukarimu unaotoka moyoni huleta furaha.
2Wakorintho 9:7: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu”. Kutoa kwa hiari humfurahisha Mungu.
Nawe toa kwa hiari na upendo ili Mungu afurahi, liwe deni kwake la kukufungulia milango. Usitoe kwa majivuno, kujikweza na dharau. Hiyo itakuwa ni kutafuta hasira ya Mungu ikushukie na kukuzibia milango yako ya mafanikio.
Biblia inasema nini kuhusu kutoa
Biblia inatutia moyo kutoa kwa hiari na kwa nia nzuri. Inaonesha kwamba kutoa kwa njia hiyo kunamnufaisha anayepokea na anayetoa pia. (Methali 11:25; Luka 6:38). Yesu mwenyewe alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea” (Matendo 20:35). Ukitoa utasababisha aliyepokea amshukuru Mungu na jambo hilo kukuongezea kitu wewe mtoaji maana wewe ndiye chanzo cha shukrani hiyo. Utoaji wako utakupa sifa na heshima.
Ni wakati gani ambapo Mungu anafurahi tunapotoa
Mungu anafurahi tunapotoa kwa hiari. Biblia inasema hivi: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si bila kutaka wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu” (2Wakorintho 9:7).
Kutoa kwa hiari ni “namna ya dini” ambayo Mungu anakubali. (Yakobo 1:27). Mtu anayewasaidia wengine kwa ukarimu anafanya kazi pamoja na Mungu, ambaye anaona ukarimu huo kuwa mkopo kwake (Methali 19:17). Biblia inafundisha kuwa Mungu atamlipa yule anayetoa (Luka 14:12-14).
Ni wakati gani ambapo Mungu hafurahi tunapotoa
Hii hutokea tunapotoa kwa nia mbaya. Hii ni kama vile:
Ili tulipwe kwa njia fulani (Luka 14:12-14).
Tunapolenga kupata kusifiwa na watu (Mathayo 6:2).
Tunapojaribu kununua wokovu (Zaburi 49:6-7).
Wakati ambapo kutoa kunaingilia majukumu tuliyopewa na Mungu. Biblia inafundisha kuwa vichwa vya familia wanapaswa kuandaa mahitaji ya familia zao (1Timotheo 5:8). Si jambo linalofaa kwa kichwa cha familia kuwapa wengine kupita kiasi, hivi kwamba familia yake inateseka. Vivyo hivyo, Yesu aliwashutumu wale waliokataa kuwaandalia wazazi wao waliozeeka kwa kudai kwamba mali zao zote zilikuwa “zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu” (Marko 7:9-13).
Ikiwa zawadi yetu itatumiwa kuunga mkono utendaji na mitazamo ambayo Mungu anashutumu. Yaani, lingekuwa kosa kumpa mtu fedha kwa ajili ya kucheza kamari au kutumia kileo vibaya au dawa za kulevya (1Wakorintho 6:9-10; 2Wakorintho 7:1). Vivyo hivyo, si sawa kumpa fedha mtu ambaye anaweza kujitegemea lakini anakataa kufanya kazi (2Wathesalonike 3:8-10).
Maandiko mengine kuhusu kutoa
Methali 11:25: “Mtu mkarimu atapata ufanisi, na yule anayewaburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa”. Hii ni kwa sababu kutoa humnufaisha anayepokea na anayetoa.
Methali 19:17: “Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, naye Atamlipa kwa anayotenda”. Sababu ni kuwa Mungu anaona kwamba ana deni kwa wale wanaowasaidia wenye uhitaji, na anaahidi kuwalipa kwa ukarimu wao.
Mathayo 6:2: “Unapotoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki, ili wasifiwe na watu”. Hii ni kwa sababu hatupaswi kutoa ili watu watutambue. Hii ni kutafuta sifa na kujikweza.
Matendo 20:35: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea”. Ni kwa vile ukarimu unaotoka moyoni huleta furaha.
2Wakorintho 9:7: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu”. Kutoa kwa hiari humfurahisha Mungu.
Nawe toa kwa hiari na upendo ili Mungu afurahi, liwe deni kwake la kukufungulia milango. Usitoe kwa majivuno, kujikweza na dharau. Hiyo itakuwa ni kutafuta hasira ya Mungu ikushukie na kukuzibia milango yako ya mafanikio.