Kutoka Algeria: MC Alger 4 - 0 Young Africans

py thon

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
2,476
Reaction score
4,448
April 15 2017 Yanga wanacheza mchezo wa marudiano wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la shirikisho dhidi ya MC Alger nchini Algeria.

Dakika ya 15 sasa hivi

Algiers 1-0 Yanga

April 15 nchini Algeria katika uwanja wa July 5 1962 mjini Al-Jaza’ir, Yanga ambao waliingia wakiwa wanahitaji sare ya aina yoyote ili waweze kupata nafasi ya kuingia katika hatua ya makundi ya Kombe la shirikisho barani Afrika, wamejikuta wakikubali kipigo cha magoli 4-0 na safari yao kuishia hapo.

Magoli ya MC Alger ambao waliingia uwanja wa July 5 1962 wakiwa na sapoti kubwa ya mashabiki wao yalifungwa na Aouadj dakika ya 14 na 91, Derrardja dakika ya 39 na Zerdab dakika ya 66, hivyo Yanga wanaondolewa katika michuano ya Kombe la shirikisho barani Afrika kwa jumla ya magoli 4-1.
 
Sina uhakika na Channel ambayo itathubutu ' kupoteza ' muda wake kuonyesha mechi ya Klabu mbovu duniani kote ya Yanga FC.
Nasikia Nancy pop katimuliwa Ofis za tff muda huu,jamaa wamechoka kubeba wagonjwa
 
Kama ni mbovu mbona haijatolewa?

Na mnaohitaji ' updates ' za mechi ya Yanga FC huko Algeria ni kwamba hadi hivi sasa ni dakika ya 21 Yanga FC ameshafungwa ' Kimoko ' yaani goli 1. Kwa mnaotaka kuufuatilia huu mpira just tune in to 94.5 Mhz Sibuka FM wanautangaza. Goli la MC Algiers limefungwa dakika ya 15 na Mchezaji aitwae Mohammed.
 
Mechi ya ubingwa mmechemsha Mwanza...jumanne mnapokwa points za kagera..Yanga bingwa tena 2017 kwa mara ya tatu mfululizo
 
Sina uhakika na Channel ambayo itathubutu ' kupoteza ' muda wake kuonyesha mechi ya Klabu mbovu duniani kote ya Yanga FC.
Kidogo kwa Comment hii nitajifariji kwa yaliyotokea leo kanda ya ziwa

Asante mkuu...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…