Kutoka Chato: Rais Magufuli amwapisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Kwanini Mbuzi, papai, fenesi na Kware wawe na Corona?

Umeenda chaka kidogo lakini kwa sehemu kubwa uko sahihi. Ndani ya Ikulu pale Magogoni kuna makazi ya Rais aliye madarakani na familia yake kama anayo. Pia kuna ofisi ya Rais ya kwake kama mtumishi wa Serikali na ofisi ya Rais kama taasisi ambazo zinatumiwa na watumishi wengine wa taasisi hiyo ikiwemo ofisi ya Makamu, Katibu Mkuu na wengine wengi. Pamoja na makazi ya Rais kuwepo ndanj ya Ikulu, Rais kwa uamuzi wake mwenyewe anaweza kuishi popote nchini, inaweza kuwa Msasani (Nyerere) au karibu na Agha Khan Hospital (Mkapa) au Chato (Magufuli). Makazi haya si Ikulu bali ni nyumbani kwa marais hawa na wataendelea kuishi humo wakistaafu. Zile Ikulu ndogo za mikoani zinatumika kama nyumba za kuishi Rais akiwa safarini huko. Kwa taratibu zetu zilizopo, ofisi za Rais zipo Ikulu Magogoni, Dar mpaka zitakapohama rasmi kwenda Chamwino, Dodoma na kuacha nyumba ya Magogoni kwa matumizi mengine. Kenya wao Ikulu ni makazi ya Rais tu, ofisi zake zikiwa kwingineko mtaani ili hata wanyonge wazifikie kwa urahisi kumwona mpendwa wao waliomchagua wenyewe.
 
Unaweza kujuaje haviko contaminated na haupo maabara? Uraisi ni taasisi lakini kwa regime hii sio taasisi ni MTU! Na sehemu nyingi maraisi wanakuwa watu si taasisi, kama the then Germany under nasisim, Kamuzu banda wa malawi, USSR etc, Labda hujagundua!

Huyo muapishwaji hataki takwimu inamaana mkuu nae hapendi takwimu sasa nasikia tuna vifo 16! Kweli uraisi ni taasisi kwa kigezo cha vifo 16! Na wafiwa wenyewe tupo!
 
Mkuu Retired, big names make news!, Rais wa nchi ndio the biggest name in the country, ukisikia anafanya jambo lolote live on national TV, this is big news!.

Hili la kusema Tanzania hatuna waandishi wa habari, ni kutudharau tuu!. Tanzania tuna media zaidi ya 1000 na zote zinahudumiwa na waandishi wa habari, hivyo huwezi kusema kuwa Tanzania hatuna waandishi!, Tanzania tuna waandishi tena wengi wa tuu kuliko vyombo vya habari tulivyonavyo!, ila kitu cha kweli ni kuwa waandishi wetu sio Tanzania sio wazuri saana kivile kama waandishi wa wenzetu.

Hili la Ikulu ya Chato ni kweli mimi ndio mwanzilishi wa jina hili, wala huna haja ya kuombea msamaha kama sitapenda, kwasababu hujafanya kosa lolote. Msamaha uombwe unapokosea na sio kwa mtu kutofurahishwa na mchango wako.
Kuhusu Ikulu ya Chato, elimu ya bure hii.
Kiswahili cha Kisiasa Kwa Watanzania: Ikulu sio Eneo Specific, ni Makazi ya Rais, Tuna Ikulu ya Magogoni, Chamwino, Sasa Hadi Ikulu ya Chato! - JamiiForums
P
 
Mzee vitu vingine bora akaushe asiongee
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yule Rais wa Russia iliyosemekana amepandikizwa na nchi zingine ili Urusi uvurugike na ikavurugika alianza namna hii. Tusipochukua hatua mapema tutajikuta pabaya; jamaa ni pandikizi kabisa.
Inaelekea una hoja sijakuelewa. Rais yupi alipandikizwa? Yelsin? ???? (spelling)
 
Msomaji mzuri, Korona wanaweza kuwa ndani ya Papai na ndani ya Fenesi pia? Au sikumsikia Rais vizuri😂😂😂
 
Meko kanikumbusha yule spokesperson wa Iraq wakati US ilipovamia Iraq. Alikuwa akiitwa Tariq Aziz nadhani.

Marekani anawaua wairaq lakini Tariq anasema "tumewashinda wamarekani, hawatuwezi hata kidogo".

Mohammed Al Sahhaf [emoji106]


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…