Kutoka kushauriwa na Prof Baregu, Prof Safari na Jasusi Nyaucho sasa Mbowe anashauriwa na Musician Sugu, Dalali Wenje na Kigaila. Chadema imejifia

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Fikiria Mwenyekiti wa Chadema aliyekuwa kazungukwa na Wasomi wabobevu kama washauri sasa Washauri wake ni Mwanamuziki wa kufokafoka Sugu Moto Chini, Mlanguzi wa mifugo ya Mpakani Dalali Wenje na mume wa mbunge wa COVID 19 Mzee Kigaila

Unaweza Kupata picha ya ugumu wa kisiasa anaokutana nao Freeman Mbowe Kwa sasa

Na ndio sababu Katibu mkuu Mh Mnyika kazi zake anafanyia Kanisani na ushauri anapata huko huko Kanisa Moja Takatifu la Mitume

Na uwezekano mkubwa Lisu akiondoka na Mnyika atashauriwa Aondoke na hawezi kukataa kulitii Kanisa

Nawatakieni Heri ya Mwaka Mpya 2025

Chadema ni Wapinzani wa Mchongo 😄🔥
 
Bwasheee sisi tutafia migombani kuliko kufia singida ni mwendo wa kuliwa na mafisi!
 
Hakika
 
Mbowe ametuchuuza muda mrefu sana.
Slaa aliondoka tukambeza sana.
Makamu wake yule mzee wa Sumbawanga tulimbeza pia
Zitto na Kitila
Baregu
Prof Safari
HAtukujua kinachoendelea...muda si mrefu Lissu atamalizia kazi ya kufunua blanketi nyeti za Mbowe zining'inie nje.
Kwaheri chama cha Chadema...sasa mnaungana kuzimu na Lipumba rasmi tarehe 21 Jan ikiwa mtafanya makosa.
 

Mr Freeman Mbowe safari hii kakumbana na "Kisiki Cha Mpingo" Tundu Lissu..

Nimefuatilia mahojiano ya Hezekiah Wenje Wasafi TV akijaribu kumfagilia na kumuosha Ndugu Freeman Mbowe na kumponda Tundu Lissu, actually Wenje kajidhalilisha na kumdidimiza zaidi boss wake..

Wenje kaboronga vibaya kwenye interview hiyo. Ama kweli NURU na GIZA kamwe haviwezi kupatana..!!
 
Mkuu na wewe ni wale wasiotaka kuwe na uchaguzi wa mwenyekiti CHADEMA? Au hutaki tu Mbowe agombee? Au hutaki vyote? Au unataka Lissu apite bila kupingwa na kukabidhiwa kiti moja kwa moja?

Uko wapi hasa? Au ndio unaendelea kudemka kwa raha zako ukiona CHADEMA inaangamia na kuwa “wapinzani wa mchongo”?
 
Daaah hii post ina ukweli fulani...

#MBOWE MUST GO
 
Kuna na wengine umewasahau:





Hao ndiyo Tanki la fikira lenyewe sasa!
 
Huyu ni mfitini tu,ukifatilia mada zake ni za kigeugeu uwenda ni project kabisa ya fitna na anafungu lake kaandaliwa.
 
Mantiki yako jini
 
Daaah ila wewe mzee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…