Kutoka kwa Chambi Chachage: Marejeo ya maisha ya Abdulwahid Sykes na harakati za kuunda tanu

Kutoka kwa Chambi Chachage: Marejeo ya maisha ya Abdulwahid Sykes na harakati za kuunda tanu

Kilichonikosha kwenye hii habari ni kuwa MWAKA 1967 kuna watanzania walikuwa wameanza kukata keki aseee...
Perfect,
Kumbuka kuwa huyo aikuwa ni mtoto wa chief.

Mimi binafsi hiyo ndiyo ilikuwa ni party yangu ya kwanza kuhudhuria
maishani mwangu.

Huwa nikikutana na Chief Edward Makwaia sasa tu watu wazima
huwa tunakumbushana mengi ya utoto.

Huwa namwambia, ''Unajua Teddy wewe ndiye uliyeniingiza mimi
katika music wa James Brown nk. nk...''

Basi yeye huwa kimya.

Katika miaka ya 1960s kulikuwa na ''music craze,'' inaitwa, ''Soul Music.''
Vijana tuliingia wazimu.

Bingwa wa muziki huu alikuwa James Brown.

Baadhi yetu vijana wa Kariakoo tulichelewa kupokea muziki huu tulikuwa
bado na Elvis Presley na Cliff Richard.

Huwa simwachi Teddy nitamwambia jambo jingine ambalo mimi sikuwanalo
kabla ya kukutanane.

Basi sasa atacheka kisha atasema, ''Oh! unajua Sidney mimi nimejifunza
mengi pia kutoka kwako...''

Ninachotaka kukuambia kuwa kulikuwa na utamaduni mpya mara tu baada ya
Waingereza kuondoka ingawa mizizi ya utamaduni huu mizizi yake ni ukoloni
wa Waingereza.

Utamaduni huu uliingiza katika jamii tabaka jipya la Waafrika walionufaika kwa
kushika nafasi za Waingereza pale walipoondoka.

Wazazi wetu waliathirika na mageuzi haya mapya na sisi watoto hatukusalimika
pia.
 
Perfect,
Kumbuka kuwa huyo aikuwa ni mtoto wa chief.

Mimi binafsi hiyo ndiyo ilikuwa ni party yangu ya kwanza kuhudhuria
maishani mwangu.

Huwa nikikutana na Chief Edward Makwaia sasa tu watu wazima
huwa tunakumbushana mengi ya utoto.

Huwa namwambia, ''Unajua Teddy wewe ndiye uliyeniingiza mimi
katika music wa James Brown nk. nk...''

Basi yeye huwa kimya.

Katika miaka ya 1960s kulikuwa na ''music craze,'' inaitwa, ''Soul Music.''
Vijana tuliingia wazimu.

Bingwa wa muziki huu alikuwa James Brown.

Baadhi yetu vijana wa Kariakoo tulichelewa kupokea muziki huu tulikuwa
bado na Elvis Presley na Cliff Richard.

Huwa simwachi Teddy nitamwambia jambo jingine ambalo mimi sikuwanalo
kabla ya kukutanane.

Basi sasa atacheka kisha atasema, ''Oh! unajua Sidney mimi nimejifunza
mengi pia kutoka kwako...''

Ninachotaka kukuambia kuwa kulikuwa na utamaduni mpya mara tu baada ya
Waingereza kuondoka ingawa mizizi ya utamaduni huu mizizi yake ni ukoloni
wa Waingereza.

Utamaduni huu uliingiza katika jamii tabaka jipya la Waafrika walionufaika kwa
kushika nafasi za Waingereza pale walipoondoka.

Wazazi wetu waliathirika na mageuzi haya mapya na sisi watoto hatukusalimika
pia.
Mkuu unasema kweli?Asee hongera sana kaka maana miaka hiyo kula keki kubwa kama hiyo ilikuwa ni nadra sana.
 
Mkuu unasema kweli?Asee hongera sana kaka maana miaka hiyo kula keki kubwa kama hiyo ilikuwa ni nadra sana.
Perfect,
Kuna mengine makubwa zaidi ya cake naona yamekupita.
Angalia hiyo picha na ''caption,'' yake.
 
Maalim Faiza,
Nami ndipo nikaona hebu nililete hili jambo Majlis.

Lakini haya yote kijana anachomwa na ule ukweli kuwa hiyo TANU
hapo kwa Hamza na Abdul ndipo kwake.

Hana jingine la kufanya ila achokonoe hata pale alipopewa jibu na
mwenye mali.

Mzee Said, maswali yangu kwako huwa nayauliza kwa nia njema ili yanisaidie kwenye utafiti wangu. Balozi Juma hadhani kama hiyo mikutano ilikuwa inafanyika kwenye nyumba yao ya Ilala Quarter maana ilikuwa ndogo sana. Pia hana uhakika kama ilifanyika kwenye ofisi ya Ilala Boma maana ilikuwa ni ya Serikali.

Kwa ufupi, sote tunakubaliana kwamba mikutano ilifanyika. Tunachotoka - ama ninachotaka mimi - kujua ni wapi hasa, nyumbani kwa Hamza, ofisini kwake au sehemu nyingine ya mafichoni huko Ilala kama Balozi anavyohisi?

Msaada tafadhali, kama nilivyosema, yote nauliza kwa nia njema - naona safari hii hata Maalim Faiza kaliona hilo.
 
Mzee Said, maswali yangu kwako huwa nayauliza kwa nia njema ili yanisaidie kwenye utafiti wangu. Balozi Juma hadhani kama hiyo mikutano ilikuwa inafanyika kwenye nyumba yao ya Ilala Quarter maana ilikuwa ndogo sana. Pia hana uhakika kama ilifanyika kwenye ofisi ya Ilala Boma maana ilikuwa ni ya Serikali.

Kwa ufupi, sote tunakubaliana kwamba mikutano ilifanyika. Tunachotoka - ama ninachotaka mimi - kujua ni wapi hasa, nyumbani kwa Hamza, ofisini kwake au sehemu nyingine ya mafichoni huko Ilala kama Balozi anavyohisi?

Msaada tafadhali, kama nilivyosema, yote nauliza kwa nia njema - naona safari hii hata Maalim Faiza kaliona hilo.
Companero,
Nijuavyo mimi na nimeandika kwingi kuwa mikutano ikifanyika Ilala Welfare Centre.
Mimi sijapata kusema ikifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu.

Wala mimi sijasema mikutano ilikuwa ikifanyika Ilala Boma.

Mikutano mingine ilikuwa ikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na
Sikukuu.

Hii nyumba naifahamu vizuri sana ni nyumba yenye nafasi na hadhi kwa wakati ule.

Katika Nyaraka za Sykes nimekuta dondoo za mkutano wa Tanganyika African
Government Servants Asociation (TAGSA) uliofanyika hapa uliohudhuriwa na
Ally Sykes, Thomas Marealle, Rashid Kawawa, Stephen Mhando, Othman
Chande
na Leonard Bakuname.

(Ally Sykes TAGSA Honorary Secretary, to The Honourable Chief Secretary to the
Government; Ref. No. 1/52/3 10 January, 1952).

Sasa huyu aliyeniambia kuwa wakifanya mikutano nyumbani kwa Abdul Sykes ndiye
huyu aliyeniambia kuwa mikutano mingine wakifanya Ilala Welfare Centre.

Kuna mikutano mingine ikifanyika Mtaa wa Pemba lakini sikuweza kujua khasa ni
katika nyumba ipi ingawa nahisi inaweza ikawa kwa Maalim Sakina Biti Arab.

Ninaloweza kusema ni kuwa mkutano muhimu uliohudhuriwa na Sheikh Hassan bin
Amir, Sheikh Abdallah Chaurembo, Sheikh Nurdin Hussein, Rajab Diwani

ulifanyika usiku hapo Mtaa wa Pemba na ni katika mkutano huu ndipo Sheikh
Hassan bin Amir
alieleza umuhimu wa kufuta ''symbols'' zote za Uislam katika TANU ili
TANU iepukane na haiba ya kuwa ni chama cha Waislam.

Nyumba ya Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu ni hiyo hapo chini ingawa
imefanyiwa mabadiliko kidogo kwa kuwekwa milango ya maduka katika miaka
ya 1980s:

19875631_2266299993396351_3581677469312723942_n.jpg
 
Very interesting! Majina mengi nimewahi kusikia kutoka kwa kaka zangu waliokulia kariakoo.Nilikuwa sijui kama mzee cha urembo alikuwa na mchango kwenye kupigania uhuru,nilijiwa alikuwa na Alwatani tu mitaa ya narung'ombe kumbe duh!.Tumeunga damu na huu ukoo,maskini kariakoo ya wazaramo imepotea.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom