Kutoka maktaba: Hakimu aliyechunwa ngozi kwa ufisadi

Kutoka maktaba: Hakimu aliyechunwa ngozi kwa ufisadi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Mchoro wa karne ya 16 unaoonyesha kuchunwa ngozi akiwa hai kwa hakimu fisadi, Sisamnes, katika mwaka wa 500BC.

Sisamnes alikuwa hakimu wa kifalme fisadi wakati wa Cambyses ll katika taifa la Uajemi. Iligundulika kuwa alichukua hongo/rushwa mahakamani na akatoa hukumu isiyo ya haki. Kwa sababu hiyo mfalme akaamuru akamatwe kwa ufisadi wake na akaamuru achunwe ngozi akiwa hai.

Kabla ya kutoa hukumu mfalme alimuuliza Sisamnes ni nani alitaka kumteua kama mrithi wake. Sisamnes, kwa uchoyo wake, alimchagua mwanawe, Otanes.

Mfalme alikubali na kumteua Otanes kuchukua nafasi ya baba yake. Baadaye alitoa hukumu na kuamuru kwamba ngozi iliyoondolewa ya Sisamnes itumike kuwamba kiti ambacho hakimu mpya angekalia kortini ili kumkumbusha madhara yanayoweza kusababishwa na ufisadi.

Otanes, katika mashauri yake, alilazimika kukumbuka daima kwamba alikuwa ameketi kwenye ngozi ya baba yake aliyeuawa. Hii ilisaidia kuhakikisha haki na usawa katika vikao vyake vyote, mijadala na hukumu

Somo la haki kwa watoa hukumu wetu.. Je umejifunza kitu hapa?

Screenshot_20220803-083837.jpg
 
Hii dunia imetoka mbalii sana

Kuna mabadiliko makubwa sana yamefanyika kwenye kila sector

tushukuru sana tupo karne hii ukiguswa kidogoo unapi yoweee dunia zima inasikia..
 
Hii inaonesha jinsi dunia ya sasa hivi ilivyojisogeza karibu sana na udhalimu kiasi kwamba ubaya wake hauonekani kabisa. Those days watu hao (waadilifu) walichukia hasa huo ubaya.
 
Laiti wabakaji na wanaodhulumu wajane wangefanyiwa hivi, dunia ingekuwa salama.

Asante, napenda vile Mshana Jr unavyozidi kuzeeka na mada zako zinakuwa fupi fupi,
 
Zama zile rushwa, ufisadi hatukuuonea haya kabisaaa, tulimshughulikia mlarushwa kisawasawa hatukuwa na masihara juu ya suala hili.
 
Dunia Imekuwa salama kwa watu wa bara Amerika bara ulaya na wachache Africa.. hali bado ni ya majuto kwa wenzetu Arabu. Viongozi wakubwa wananyongwa(2007) viongozi wanakufa kwa kuburutwa na kutundikwa kama mbwa(2011) viongozi wanapigwa makombora kama mwangosi na miili yao inasambaratika kama majivu na kukosa maziko (2022)
RIP Dr Ayman
IMG-20220802-WA0016.jpg
 
Dunia Imekuwa salama kwa watu wa bara Amerika bara ulaya na wachache Africa.. hali bado ni ya majuto kwa wenzetu Arabu. Viongozi wakubwa wananyongwa(2007) viongozi wanakufa kwa kuburutwa na kutundikwa kama mbwa(2011) viongozi wanapigwa makombora kama mwangosi na miili yao inasambaratika kama majivu na kukosa maziko (2022)
RIP Dr Ayman View attachment 2312749
Duh.. Huko ni jino kwa jino
 
Ingekuja TZ nakuapia
1. mahakimu woooote
2. Ma-Jaji karibu wote hasa (wale wa michongo)
3. Traffics wooooooooote 😀
 
Mchoro wa karne ya 16 unaoonyesha kuchunwa ngozi akiwa hai kwa hakimu fisadi, Sisamnes, katika mwaka wa 500BC.

Sisamnes alikuwa hakimu wa kifalme fisadi wakati wa Cambyses ll katika taifa la Uajemi. Iligundulika kuwa alichukua hongo/rushwa mahakamani na akatoa hukumu isiyo ya haki. Kwa sababu hiyo mfalme akaamuru akamatwe kwa ufisadi wake na akaamuru achunwe ngozi akiwa hai.

Kabla ya kutoa hukumu mfalme alimuuliza Sisamnes ni nani alitaka kumteua kama mrithi wake. Sisamnes, kwa uchoyo wake, alimchagua mwanawe, Otanes.

Mfalme alikubali na kumteua Otanes kuchukua nafasi ya baba yake. Baadaye alitoa hukumu na kuamuru kwamba ngozi iliyoondolewa ya Sisamnes itumike kuwamba kiti ambacho hakimu mpya angekalia kortini ili kumkumbusha madhara yanayoweza kusababishwa na ufisadi.

Otanes, katika mashauri yake, alilazimika kukumbuka daima kwamba alikuwa ameketi kwenye ngozi ya baba yake aliyeuawa. Hii ilisaidia kuhakikisha haki na usawa katika vikao vyake vyote, mijadala na hukumu

Somo la haki kwa watoa hukumu wetu.. Je umejifunza kitu hapa?

View attachment 2312625
mwamba mwenye kofia ni fundi wa kuchuna.!
 
ZAMANI WATU WALIKUWA WAKATILI DUUUH
Sasa hivi wamezidi sana naomba kunukuu kauli,

1. "Wapigwe tu"
2. "Tukio hili limefanywa na watu wasiojulikana"
3. " asante nimepokea hela, ila nimepewa kazi nyingine sitakuja"
4. " tumeongeza mshahara kwa asili 23%"
5. " maombi yako ya kazi yamepokelewa - sensa ishu"
6. Wabunge kulalamika hela wanayolipwa ni ndogo wanataka kuongezewa
7. " ndege ya Raisi lazima inunuliwe, tufunge mikanda"
8. " njoo na kadi ya bima ya afya ndo tumumpatie huduma, au lipa pale cash ndo tukuhudmie"
....
 
Back
Top Bottom