Kutoka Mtwara katika Picha








Angalia wakina mama hawa walivyo busy wakitafuta vitoweo. Jambo lililonishangaza ni kwamba sikuona wakina baba wengi katika zoezi hili la uvuvi wa aina hii bali wakina mama walikuwa wengi sana. Kweli wamama ujituma kazi nyingi sana na kipato chao huwa juu sana. Kwa nini wakina baba hawaonekani sana zaidi ya kuwakuta kwenye mnazi!? hiyo wanaweza kujibu wenyewe!


Hii ni barabara nilipita nikienda Msimbati.
 

Hii ni barabara ya kwenda Msimbati. Eneo hili ndilo lililo na utajiri wa gesi. Hapa pamefanywa kama hifadhi ya taifa. Lakini barabara sijui kwa nini hawakuijenga vizuri maana kule baharini pana utajiri mzuri ajabu. Paweza kuwa sehemu nzuri sana kitalii. Hata hivyo kama kawaida serikali zetu hazijaona umuhimu huo pamoja na kwamba kuingia eneo hilo unalazimishwa kulipa shilingi 2,000.= kama wewe ni mtz.


Huu ni ufukwe nilikutana nao wakati nakwenda Msimbati. Angalia mikoko ilivyopamba ufukwe wenyewe. Sehemu nyingine za fukwe niliona wakivuna chumvi. Katika kuvuna chumvi wao utengeneza mataruma kama yale ya kulimia mpunga😀

Hiki ni kituo cha Polisi pale Msimbati. Eneo hili ni mali hivyo ulindwa sana. Hongera jeshi la polisi.




Pamoja na utajiri wote uliowazunguka wakazi hawa wa Msimbati wanaishi maisha ya kifukara tu kama unavyoona. Sijui kama wanajua ni utajiri kiasi gani unachotwa jirani tu na maeneo yao. Angalia tu nyumba wanazoishi!
 



Hapa ndio sehemu ya Msimbati. Maeneo jirani na Mnazi bay.


Hii ni barabara iliyo ndani ya hifadhi. Pamepandwa minazi na mikorosho ndani ya hifadhi. Eneo zima ni mchanga mtupu na kama si juhudi za wawekezaji kuweka wavu maalum juu ya mchanga magari yasingepita. Lakini hapa ni barabara ya mchanga iliyowekwa wavu kama kilometa ishirini na huna haja ya kutumia 4wheel. Safi sana wawekezaji.




Hizi ni beach pale mnazi bay jirani kabisa na kituo cha kuzalishia gesi toka baharini. Ni moja ya fukwe nilizopenda na kutamani sana. Huwezi kulinganisha na fukwe za Dar zilizojaa uchafu na harufu kali kabisa. Kama zingeweza kuamishiwa Dar hizi jinsi zilivyo nzuri na safi..........!?!@&

 
Huu uzi ni wa mwaka 2009 miaka kama 11 hivi iliyopita. Wakati huo Mtwara ilikua inachipukia kuja juu. Leo siyo haba japo kumedidimia tena baada ya mambo ya gesi kupoa kabisa.
Kama mdau au wadau ikiwemo mleta mada akienda tena anaweza kuwa na picha nyingi na nzuri kuliko hizo. Kwa sasa anaweza kupata BNN ROYAL Hote,Cashewnut Hotel,LUWA EVERGREEN HOTEL,TIFFANY DIAMOND HOTEL,KIWANDA CHA DANGOTE, Vinu vya kuchakata Gesi kwa ajili ya Mtwara kule Kilambo,KIWANDA CHA CHEMICAL ZA WATAFUTA GESI,BUSTANI/MANDHARI NZURI PALE MZUNGUKO MNARANI,TAA ZA KUONGOZA MAGARI PALE BIMA(ingawa siyo issue sana,ila kwa kuwa ipo miji haina hata moja,nasi nayo siyo haba) nk nk nk.
Tutashukuru kama mtu atajitolea kuziweka humu.
Hii itasaidia kuwaelimisha watu ambao hawajafika Mtwara wapate elimu ya nini hasa kipo Mtwara

Ni matumaini tutapata mwendelezo wa picha kati ya zile za mwaka 2009 na leo hii 2021.
Enzi hizo Mashujaa Park, Tilla Park hazikua nzuri kama leo, hakukua na Naf Beach, Tiffany, BNN Royal, Shangan Apartments, Chuno road, Dangote, Luwa Evergreen, Shooters nk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bahati mbaya mimi ni mzee wa miaka 70 na nina kora ya kichungaji shingoni! hivo vibinti vidogo vyote vilikuwa vinanikimbia. Nisingeweza kupata picha zao.
Kwa hiyo sahiv utakuwa na 80 sio?
 
Admin mbona picha hazifunguki?
Au zilipata virus?
Tunaomba muzirejeshe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii kitu ipo kweli pale Chikongola hadi leo? Mkuu ndo nasikia leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo, kuhusu muda kwa mabasi yanayoenda Mtwara mjini na baashi Masasi unayapata mpaka saa 8 pale Temeke Sudan
 
Hii dude ilianzishwa miaka 13 iliyopita. Muanzisha uzi hatujui hali yake ila abarikiwe sana. Bahati mbaya picha nyi gi ziliziwekwa miaka hiyo hazifunguki tena. Kwa sasa twaongeza Kutoka Mtwara katika Video:

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…